Thursday, November 16, 2017

Military takes over Zimbabwe

Military takes over Zimbabwe

Zimbabwe’s military has taken control of the capital and the state broadcaster, with President Robert Mugabe being held under house arrest. 
In what appeared to be a coup against the 93-year-old Mugabe – the world’s oldest head of state – the military insisted it had not staged a takeover, but was instead starting a process to restore the country’s democracy.

It comes after a power struggle over who would replace the aging leader, with his wife Grace seen as the most likely successor.
Her current whereabouts are unclear, although the military claims she is also under house arrest.
South African president Jacob Zuma said his country’s ministers of defence and state security are being sent to Zimbabwe to meet with Mr Mugabe and the military.

The night’s action triggered speculation of a coup but the military’s supporters praised it as a ‘bloodless correction’.
For the first time, the southern African nation is seeing the military oppose Mr Mugabe, the world’s oldest head of state and one of the longest-serving authoritarian rulers.


Mr Mugabe has been in power since Zimbabwe’s independence from white minority rule in 1980.
The move comes after Mr Mugabe last week fired vice president Emmerson Mnangagwa.
Mr Mnangagwa – who enjoyed the military’s backing – fled Zimbabwe last week but said he would return to lead the country.
More than 100 senior officials allegedly supporting him have been listed for disciplinary measures by a faction associated with Mr Mugabe’s wife Grace.

‘We are only targeting criminals around (Mugabe) who are committing crimes that are causing social and economic suffering in the country in order to bring them to justice.’
Mr Moyo added ‘as soon as we have accomplished our mission, we expect that the situation will return to normalcy’.

The army spokesman called on churches to pray for the nation.
He urged other security forces to ‘co-operate for the good of our country,’ warning ‘any provocation will be met with an appropriate response’.
All troops were ordered to return to barracks immediately, with all leave cancelled, said Mr Moyo. The broadcast was sent out from the ZBC headquarters in Pocket’s Hill near Harare’s Borrowdale suburb.
Overnight, at least three explosions were heard in the capital, Harare, and military vehicles were seen in the streets.

The military actions appear to put the army in control of the country.
Army commander Constantino Chiwenga had threatened on Monday to ‘step in’ to calm political tensions.
Mr Mugabe’s ruling ZANU-PF party responded by accusing the general of ‘treasonable conduct’. But now Mr Chiwenga appears to be in control.
The US Embassy closed to the public on Wednesday and encouraged citizens to shelter in place, citing ‘the ongoing political uncertainty through the night’.
The British Embassy issued a similar warning, citing ‘reports of unusual military activity’.



 

Friday, October 27, 2017

ORODHA YA KWANZA NA YA PILI YA MAJINA YA WALIOPATA MIKOPO 2017/2018

ORODHA YA KWANZA NA YA PILI YA MAJINA YA WALIOPATA MIKOPO 2017/2018

Waombaji wa Mwaka wa Kwanza

Tunapenda kuwafahamisha waombaji wa mikopo ya elimu ya juu kwa mwaka wa masomo 2017/2018 kuwa, baada ya uchambuzi wa maombi yao, Orodha ya Awamu ya Kwanza yenye wanafunzi 10,196 wa mwaka wa kwanza waliofanikiwa kupangiwa mikopo imekamilika.

Kiasi cha Tshs 34.6 bilioni kimetengwa kwa ajili ya wanafunzi hao 10,196. Kwa ujumla, Tshs 108.8 bilioni zitatolewa kwa wanafunzi 30,000 wa mwaka wa kwanza kwa mwaka wa masomo 2017/2018.
  
Orodha hiyo ya kwanza inapatikana kwenye tovuti ya Bodi ya Mikopo (www.heslb.go.tz) na itatumwa kwa vyuo husika. Orodha nyingine (batches) zitafuata kadri taratibu za udahili na uchambuzi zinavyokamilika. Lengo ni kutoa majina ya wote waliofanikiwa kupata mkopo kabla ya vyuo kufunguliwa mwishoni mwa mwezi huu wa Oktoba, 2017.

Orodha hii ya wanafunzi 10,196 imepatikana baada ya kupokea na kuchambua Awamu ya Kwanza ya majina ya wanafunzi 32,495 waliopata udahili katika chuo kimoja. Itakumbukwa kuwa moja ya sifa kuu za kupata mkopo ni mwombaji kupata udahili katika taasisi ya elimu ya juu inayotambuliwa na Serikali.

Wanafunzi waliopata udahili katika chuo zaidi ya kimoja na ambao wana sifa za kupata mikopo, watapangiwa mikopo baada ya kuchagua na kuthibitisha chuo watakachojiunga kwa ajili ya masomo.

Tshs 318 bilioni zatengwa kwa ajili ya wanaoendelea na masomo

Wakati huohuo, tunapenda kuwafahamisha wanafunzi wa elimu ya juu wanaoendelea na masomo na umma kwa ujumla kuwa tunatarajia kuanza kutuma vyuoni fedha za mikopo ya wanafunzi wanaoendelea na masomo ambao wamefaulu mitihani yao kuanzia leo, Jumatano, Oktoba 18, 2017.

Kiasi cha Tshs 318.6 bilioni kitatolewa kwa wanafunzi 93,295 wanaoendelea na masomo kwa mwaka wa masomo 2017/2018. Tayari Serikali imeshatoa fedha hizo na lengo la Bodi ni kuhakikisha fedha zinafika vyuoni kabla ya kufunguliwa kwa vyuo ili kuwaondoloea wanafunzi usumbufu.

Hitimisho
Bodi ya Mikopo inawasihi waombaji wa mikopo kuwa na subira wakati ikiendelea kukamilisha maandalizi ya orodha zinazofuata za wanafunzi waliopata mikopo. Tutaendelea kutoa taarifa kwa vyombo vya habari na tovuti ya Bodi mara kwa mara.
Kupata orodha kamili Orodha ya kwanza 
Kupata orodha kamiliOrodha ya pili

 

Friday, August 11, 2017

Uhuru Kenyatta wins Kenya presidential election

 Mr Kenyatta, in office since 2013, took 54.3% of votes, ahead of his rival Raila Odinga, with 44.7%.
After the announcement, Mr Kenyatta called for unity, telling opposition supporters: "I reach out to you... We are all citizens of the same republic".
But the opposition rejected the results even before they were declared, calling the process a "charade".
However it has been endorsed by international observers. Mr Kenyatta said they had ensured a "free, fair and credible election".
Earlier, Mr Odinga's supporters said he had won, and published their own figures. The electoral commission said this was "illegal and premature", and said basic mathematical errors had been made.
Many observers fear a repeat of the violence after the disputed election 10 years ago when more than 1,100 Kenyans died and 600,000 were displaced

Opposition rejection

Shortly before the results were announced, opposition members said they will reject it.
"We are not going to be party to it. Our issues have not been addressed. One can conclude they [electoral commission] are not keen on taking our concerns seriously," Musalia Mudavadi, a senior official of the National Super Alliance (NASA) and former Kenyan vice president, said.
James Orengo, another senior NASA official, called the election process a "charade" and a "disaster".
"You do not just hold an election for the sake of it. And the election is not about announcing winners and losers," he said.
On Wednesday, Odinga - a long time rival of Kenyatta who was running for the presidency for the fourth time - rejected the results of Tuesday's election.
He claimed the country's electronic voting system had been hacked and the results were doctored.
In a bid to unite the country after the heated campaign, Kenyatta reached out to Odinga and his supporters, saying, "We are not enemies".
"We are all citizens of one republic. As with any competition, there shall always be winners, and there shall be losers. But we all belong to one great nation called Kenya. I extend a hand of friendship."  

Previous disputes

Chebukati, the electoral commission chairman, said a hacking attempt had failed to manipulate the outcome of the vote. International observers including the African Union said the election was free and fair and called on disputes to be resolved through the courts.
In 2013, Odinga lost to Kenyatta and claimed the results were manipulated but Kenya's Supreme Court announced Kenyatta the winner.
.

Tuesday, July 25, 2017

KUJIUNGA NA DEGREE NIT ONLINE ADMISSION

BONYEZA HIYO LINK HAPO CHINI KWA KUJIUNGA NA NATIONAL INSTITUTE OF TRASPORT (NIT) KWA COURSE MBALIMBALI NGAZI YA DEGREE

 NIT OAS

MIFANO:
  • Human Resource Management
  •  Business Administration
  • Marketing and Public Relations
  •  Accounting and Transport Finance
  •  Aircraft Maintenance Engineering
  •  Education with Mathematics and Information Technology
  • Automobile Engineering
  • Mechanical Engineering
  • Procurement and Logistics Management
  • Information Technology
  • Computer Science
  • Logistics and Transport Management                 
NIT OAS 





HESLB yajipanga maombi ya mikopo 2017/2018

HESLB yajipanga maombi ya mikopo 2017/2018

Wakuu na maafisa wa Idara na Vitengo mbalimbali vya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu  wapo katika maandalizi ya mwisho ya kufanyia majaribio mfumo wake ulioboreshwa wa uombaji mikopo kupitia  olas.heslb.go.tz kabla ya kukaribisha maombi ya mikopo ya wanafunzi kwa mwaka wa masomo 2017/2018.

Kwa mujibu wa Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa TEHAMA Bw. Muze Ninkhambazi ambaye ameongoza mafunzo ya kuwapitisha idara na vitengo hivyo ili kuufahamu na kupata mapendekezo kutoka kwao kwa ajili ya kuboresha mambo muhimu yanayoingia katika mfumo huo kabla ya kukaribisha maombi ya mikopo kwa mwaka wa masomo 2017/2018.
Bw. Ninkhambazi amesema mabadiliko ya mfumo yanalenga kuufanya uwe wa kisasa zaidi na kuwarahisishia waombaji mikopo jinsi ya kuwasilisha taarifa zao Bodi. Aidha ameongeza kuwa maandalizi hayo yamewezesha kupata mchango mkubwa kutoka wa washiriki.

Miongoni mwa mabadiliko katika OLAMS ni pamoja na jinsi ya kufanya malipo, kuwasilisha viambatanisho muhimu kama cheti cha kuzaliwa, cheti cha kidato cha nne na saini za mwombaji na mdhamini wake.
Bodi ya Mikopo iliingia katika mfumo wa uombaji mikopo kwa njia ya mtandao mwaka wa masomo 2010/2011 na tangu wakati huo mfumo huo umekuwa ukiboreshwa ili kuendana na teknolojia mpya.

Thursday, July 20, 2017

Kuongezwa kwa muda wa uhakiki wa wanafunzi wanaotegemea kwenda vyuo.

BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI
(NACTE)

TAARIFA KWA UMMA
TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KUONGEZWA KWA MUDA WA MAOMBI KWA AJILI YA UHAKIKI WA TUZO MBALIMBALI KWA WALE WANAOKUSUDIA KUOMBA KUJIENDELEZA KATIKA NGAZI YA SHAHADA KATIKA VYUO VYA ELIMU YA JUU KWA MWAKA WA MASOMO 2017/2018


Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) linapenda kuwafahamisha wahitimu wa Stashahada wanaotaka kujiendeleza katika ngazi ya Shahada kuwa muda wa kufanya maombi ya uhakiki wa tuzo zao umeongezwa hadi tarehe 15 Agosti 2017.


Hivyo kwa wale ambao hawakufanikiwa kumaliza maombi ya uhakiki na wale ambao hawajaomba na wana nia ya kufanya hivyo, sasa wataweza kufanya uhakiki.


Baraza linapenda kutoa rai kwa waombaji kufanya uhakiki wa tuzo zao mapema ili kuondoa usumbufu unaoweza kujitokeza katika dakika za mwisho wa muda wa uhakiki.


Hakutakuwa na muda wa nyongeza baada ya Tarehe tajwa.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA KATIBU MTENDAJI
BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI (NACTE)
TAREHE: 19/07/2017

Sunday, July 16, 2017

ANGALIA HAPA MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2017












Kuangalia Matokeo ya Form six 2017/18 bonyeza hapo chini
Matokeo ya Form Six 2017/18


Kuangalia Matokeo ya Form six 2016/17 bonyeza hapo chini
kuangalia Matokeo Ya Form six 2016 bonyeza hapa


Kuangalia Matokeo ya Form six 2015/16 bonyeza hapo chini
Matokeo ya Form six 2015/16

Kuangalia Matokeo ya Form six 2014/15 bonyeza hapo chini
Matokeo ya Form Six 2014/15
                                                 
Kuangalia Matokeo ya Form six 2013/14 bonyeza hapo chini 
Matokeo ya Form six 2013/14
                          
Kuangalia Matokeo ya Form six 2012/13 bonyeza hapo chini
Matokeo ya Form six 2012/13

Saturday, June 10, 2017

Wanafunzi 96,018 wachaguliwa kidato cha tano

WANAFUNZI 96,018 sawa na asilimia 27.60 ya waliofanya mtihani wa Kidato cha Nne mwaka jana, na kupata ufaulu wa daraja la kwanza hadi la tatu, wamechaguliwa kujiunga na masomo ya Kidato cha Tano na vyuo vya ufundi vya serikali kuanzia mwezi ujao.
Aidha, ufaulu katika mwaka 2016 uliongezeka kwa asilimia 3.15 ikilinganishwa na ufaulu wa mwaka 2015. Kwa mujibu wa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Simbachawene, asilimia 27.60 imevuka lengo lililowekwa na Ilani ya Uchaguzi ya CCM inayoielekeza serikali kuhakikisha asilimia 20 ya wanafunzi wa elimumsingi wanachaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano.
Akitangaza uchaguzi na upangaji wa wanafunzi hao wa kujiunga na Kidato cha Tano jana ofisini kwake mjini hapa, Simbachawene alisema jumla ya watahiniwa wa shule 349,524 wakiwamo wasichana 178,775 (51.1%) na wavulana 170,749 (48.9%) walifanya mtihani wa kumaliza Kidato cha Nne mwaka 2016.
“Watahiniwa wa kujitegemea waliofanya mtihani huo mwaka 2016 walikuwa 47,751 wakiwemo wasichana 24,587 sawa na asilimia 51.5 na wavulana 23,164 sawa na asilimia 48.5,” alieleza Simbachawene.
Alisema wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano mwaka 2017 wanatoka kwenye shule za serikali na zisizo za serikali, na shule 351 zikiwamo shule 17 mpya zimepangiwa wanafunzi hao 96,018.
“Kati ya wanafunzi 96,018 ni wa wanafunzi 93,019 ndio wenye sifa za kuchaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo Vya Ufundi kwa kuwa wamefaulu vigezo vyote vya msingi kama vilivyoanishwa,” alifafanua.
Aliongeza kuwa kati ya hao, wanafunzi 92,998 ni wa shule na wanafunzi 21 walisoma chini ya Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW). Alivitaja vigezo vilivyotolewa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia vilivyotumika kuchagua na kupanga wanafunzi wa Kidato cha Tano kuwa ni AAA hadi CCD kama cut off point kwenye masomo ya tahasusi, alama tatu (credit) na pointi zisizopungua 25 kwenye Daraja, machaguo yaliyojazwa na mwanafunzi kwenye fomu maalumu na nafasi zilizopo katika shule husika.
“Napenda kusisitiza kwamba vigezo hivi ndivyo vinavyotumika kwa mwanafunzi kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo Vya Ufundi kwa mwaka huu. Nia ni kuinua kiwango cha elimu na ujuzi kwa elimu ya juu nchini,” alifafanua Simbachawene.
Kuhusu tarehe ya kuripoti shuleni, alisema muhula wa kwanza kwa wanafunzi wa Kidato cha Tano mwaka 2017, utaanza Julai 17, mwaka huu, lakini kwa wanafunzi wanaoingia Kidato cha Sita watafungua shule Julai 3.
“Kwa kuwa upangaji wa wanafunzi wanaoingia Kiato cha Tano kwa mwaka 2017 umezingatia machaguo ya wanafunzi wenyewe na nafasi zilizopo katika shule husika, hakutakuwa na fursa ya kufanya mabadiliko yoyote ya shule,” alieleza Waziri wa Tamisemi.
Aliwaagiza wanafunzi wote kuripoti katika shule walizopangiwa kwa wakati, na endapo mwanafunzi atachelewa kuripoti kwa zaidi ya siku 14 kuanzia tarehe ya kufungua shule, nafasi yake itachukuliwa na wanafunzi wengine.
Aidha, aliwaelekeza wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya, kuhakikisha kuwa shule zililizopelekewa fedha za kuongeza miundombinu ya Kidato cha Tano kupitia Mpango wa Elimu Lipa kulingana na Matokeo (EP4R) zinakamilisha ujenzi kabla ya Juni 30, 2017, na kuwapokea wanafunzi wa Kidato cha Tano.
“Napenda kuwapongeza walimu wote kwa juhudi walizozifanya katika ufundishaji na kuwezesha wanafunzi kufaulu vizuri. Hii imetokana na ushirikiano wa walimu, wazazi na walezi katika kuwapatia wanafunzi hao malezi bora,” aliongeza waziri.
Aliwapongeza wanafunzi waliochaguliwa, akiwahimiza kuendelea kuongeza bidii katika kujifunza ili wafanikiwe kujiunga na mafunzo ya elimu ya juu baada ya kuhitimu Kidato cha Sita.
Aidha, aliwashukuru wadau wa elimu kwa maana ya viongozi na watendaji wa mikoa, wilaya na halmashauri pamoja na wananchi kwa ujumla kwa kushiriki kikamilifu kuimarisha miundombinu ya shule, ikiwemo maabara na majengo mengine muhimu, yaliyowezesha shule kupokea wanafunzi wa Kidato cha Tano kwa mara ya kwanza.

Sunday, April 09, 2017

Msanii ‘Roma Mkatoliki' na wenzake wapatikana

MSANII wa muziki wa hip hop, Ibrahim Mussa, ‘Roma Mkatoliki’ na wenzake watatu wamepatikana wakiwa wazima wa afya huku bado kukiwa na maswali mengi yanayohitaji majibu juu ya kutoweka kwao kwa takriban siku tatu.
Msanii huyo akiwa na wenzake, Monii Central Zone, Bin Laden pamoja na Imma ambaye ni msaidizi wa kazi katika studio za Tongwe Records walitekwa na watu wasiojulikana na kushikiliwa kwa siku tatu bila ya taarifa zozote.
Hali hiyo iliibua taharuki kwa wasanii na familia zao na hasa mke wa Roma aitwae Nancy ambae amekuwa akizunguka kwenye vituo kadhaa vya Polisi kumsaka mumewe. Jana taarifa za kuonekana kwa msanii huyo akiwa na wenzake hao zilipatikana takriban saa nane mchana ambapo walishikiliwa kwa zaidi ya saa tano katika kituo cha Polisi Oysterbay.
Gazeti hili lilitumia zaidi ya saa sita kumngoja msanii huyo na wenzake kwa lengo la kujua ni nini kiliwakuta lakini hata hivyo hawakupata nafasi ya kuzungumza nao kituoni hapo.
Saa moja usiku aliwasili wakili wao Peter Kibatala ambae aliingia moja kwa moja kituoni humo kuzungumza na wasanii hao. Baada ya takribani dakika 10 walitolewa wasanii hao bila ya kuonana na waandishi wa habari na wakapelekwa moja kwa moja katika Hospitali ya Mwananyamala kufanyiwa vipimo.
Licha ya vyombo mbalimbali vya habari ‘kupiga kambi’ kituoni hapo tangu mchana lakini Polisi walishindwa kuzungumzia hilo.

Tuesday, February 14, 2017

UEFA LEO USIKU PSG VS BARCELONA HUKU BENIFICA VS DORTMUND


 UEFA LEO USIKU PSG VS BARCELONA HUKU BENIFICA VS DORTMUND


Michezo miwili ya michuano ya kombe la klabu bingwa ulaya katika hatua ya kumi na sita bora itachezwa leo nchini Ureno na Ufaransa.
Huko nchini Ureno Benfica watakua wenyeji wa Borussia Dortmund kutoka nchini ujerumani mchezo utakaochezwa katika uwanja wa Sport Lisboa e Benfica, na mwamuzi wa mchezo huo ni Nicola Rizzoli raia wa Italia.
Mchezo wa pili utawakutanisha Paris Saint Germain ya Ufaransa watakaokipiga na miamba wa Hispania Barcelona mchezo ukichezwa katika dimba la Parc des Princes Jijini Paris.

Champions League - Round of 16 February 14
22:45 Benfica vs Borussia Dortmund
22:45 Paris Saint Germain vs Barcelona

Jumatano zitachezwa mechi nyingine mbili Bayern Munich watachuana Arsenal na Real Madrid watatunishina misuli na Napoli ya Italia.
Mechi nyingine nne za michuano hii ya ulaya zitachezwa wiki ijayo

Madawa ya kulevya

MADAWA YA KULEVYA HAYAKUBALIKI VYUONI

Madawa ya kulevya ni kilevya chochote kinachoweza kufifisha uwezo wa kufikiri, uwezo wa kupambanua na kuona mambo, uwezo wa mwili kujikinga na maradhi na mengineo...ni hatari sana kwa mustakabali wa maisha yako, usitumie!
Kwa hapa kwetu Tanzania kuna madawa ya kulevya tuliyozoea kuyaskia kama vile..

1. *Bange na Gundi*
2. *Shisha na ugoro*
3. *Mirungi/Miraa*
4. *Heroine na Cocaine*
Na mengineyo mengi ambayo hutumiwa kwa kuvuta au kujidunga sindano mwilini. Duniani kote matumizi ya dawa za kulevya kwa namna yeyote ile hayakubaliki na serikali za dunia( Ikiwepo ya Tanzania),  taasisi za kidini na za kiraia na vyombo mbalimbali zimekuwa zikipiga kelele usiku na mchana kukataza matumizi ya dawa za kulevya kwani madhara yake huathiri mtu mmoja na kisha jamii nzima kwani tunaishi kwa kutegemeana duniani!

Katika vyuo vikuu wanafunzi pia wamekuwa miongoni mwa watumiaji na wasambazaji wa dawa za kulevya ili hali jamii inawategemea wao kutumia elimu yao na usomi wao kukomboa jamii zetu na kuleta ustawi bora haswa kwa nchi za dunia ya tatu ikiwemo Tanzania. Sasa kama wasomi wa elimu ya juu tunatumika kuuza/kusambaza na matumizi ya  dawa za kulevya, nani atasimama kulikomboa taifa letu na jamii zetu kutoka katika dimbwi la umaskini??

Tumeshuhudia kaka zetu, dada zetu, rafiki zetu, wanafunzi wenzetu wengi wakishindwa kuendelea na masomo yao vyuoni kutokana na matumizi ya dawa za kulevya simply kwa

1.Kukosa uelewa sahihi wa madhara yatokanayo na madawa haya

2. Kuishi kwa kufuata mkumbo, ulimbukeni wa mambo na kutamani vitu vya thamani na anasa au maisha fulani ilihali hauna uwezo nayo

3. Shinikizo la marafiki wanaokuzunguka.

4.Ulaghai wa kifedha toka kwa wafanya biashara hii na mengineyo mengi yanayowasukuma wanafunzi wa elimu ya juu kujihusisha katika biashara hii haramu na matumizi ya madawa haya dhalimu kwa taifa letu, kwa jamii yetu na kwa dunia hii tuliopewa na Mwenyenzi Mungu.

*Chonde! *Chonde* *Chonde* ewe ndugu yangu msomi wa elimu ya juu; matumizi ya dawa za kulevya hayakubaliki na yana madhara makubwa kama haya
1. *Huathiri mfumo wa ubongo kufikiri na udumaza akili*

2. *Huathiri mfumo wa chakula/digestion system na hupunguza na kuondoa hamu ya kula(mfano mirungi)*

3. *Huathiri mfumo wa uzazi / reproduction system(rejea mateja na watumia wa dawa za kulevya hupoteza hamu ya tendo la ndoa na kuzaa)*

4. *Husababisha magonjwa mfano. Tuberculosis (TB), magonjwa ya ngozi na mengineo mengi*

5. *Huathiri mwanadamu kisaikolojia na kimwili ( psychological and physiological problems) rejea mateja na watumiaji wa dawa za kulevya ona miili yao na uwezo wao wa kisaikolojia*

6. *Huathiri jamii kiuchumi, kijamii na namna zote kwani ukishakuwa teja au mtumiaji wa dawa hizi basi unaumiza wazazi,  ndugu na hata wategemezi wako*

6. *Hurudisha maendeleo ya taifa na jamii nyuma kiuchumi, kisiasa na kijamii na taifa laweza kuishia kuwa na raia mazezeta na wagonjwa hivyo litabaki kuwa maskini milele maana hakuna nguvu kazi ya kuzalisha na kulipa kodi kwa maendeleo yetu*

*WITO*
Kwanza waraka huu uwafikie wanafunzi wote wa elimu ya juu na wasomi ukianzia katika chuo kikuu cha Dar es Salaam (kama chuo mama na chuo cha taifa hili) na uwaendee wasomi wa elimu ya juu popote walipo Tanzania na Africa kwamba biashara na matumizi ya dawa za kulevya HAYAKUBALIKI NA TUYAPIGIE KELELE bila kujali changamoto zitazotukabili kama wasomi na watu ambao taifa linatutegemea

Pili, nitoe rai yangu kwa viongozi wa kitaifa, viongozi wa kidini na asasi za kiraia na kila RAIA mwenye akili timamu kwa nafasi yake aunge mkono kampeni/vita hii ya kupinga biashara na matumizi ya dawa za kulevya ili tuweze kulinusuru taifa letu sasa na vizazi vijazo kutoka katika madhara yatokanayo na matumizi ya madawa ya kulevya

Tatu, elimu itolewe kwa njia zote kwenye TV programs, radio, social media, makongamano na warsha na popote penye mikusanyiko ya watu mfano miskitini, makanisani ama iitishwe mijadala kutoa elimu kwa RAIA juu ya madhara makubwa yatokanayo na matumizi ya dawa hizi dhalimu kwa taifa letu na watoto wetu

NNE, wito kwa wanafunzi wenzangu wa elimu ya juu nikianzia na chuoni kwangu Udsm, tusikubali kuwa punda na kutumika vibaya kuwezesha biashara hii haramu ndani ya chuo chetu kwani wanaoathirika ni ndugu zetu, rafiki zetu na hata wasaka madesa wenzetu na wakishatumbukia na kuumia na madawa haya basi inakuwa ndio mwisho wa safari yao kupata elimu kwani hupoteza reasoning ability, performance hushuka na hupelekea Ku disco na kuondolewa chuoni( as a result psychological problems zinaanzia hapo na hatimae tunapoteza watu muhimu kwa taifa hili).

Tano, kumbuka ulipotoka, nini kimekuleta chuo na namna ambavyo wazazi wako wamejinyima na kukulipia ada hadi leo umefika chuo kikuu kisha urudi nyumbani ukiwa teja? Ukiwa zezeta? Ukiwa na GPA dhaifu? Upate discontinuation kwa madawa ya kulevya? Kumbuka ulikuja Mwenyewe usiruhusu marafiki wenye tabia mbaya wakaathiri tabia yako in negative way, simamia msimamo yako na ushike sana dini na uwe na ndoto kubwa za kupata first class GPA, epuka mabashi yasiyokuwa ya lazima sana na epuka ushiriki wako kwa namna yeyote katika biashara na matumizi ya dawa za kulevya kwani sheria na team ya Makonda watakukamata tu

*Mwisho*
*Tuungane na Rais wetu Mh.Dr JPM, Tuungane na mkuu wetu wa mkoa Dar  Mh.Makonda na viongozi wote wa kitaifa kusema
HAPANA KWA BIASHARA NA MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA* hatimae tutaweza kuinusuru nchi yetu na janga hili la madawa ya Kulevya


Imeandaliwa na
*Tony Mafie*
*Udsm Student*

Wednesday, February 01, 2017

Angalia matokeo ya form four 2016/2017


kuangalia matokeo ya formform four 2016/2017

Angalia Matokeo hapa 

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2016 - FORM FOUR (CSEE) EXAM RESULTS 2016  - NECTA - Link 1

 

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2016 - FORM FOUR (CSEE) EXAM RESULTS 2016  - NECTA - Link 2

 

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE - FORM FOUR (CSEE) EXAM RESULTS  - NECTA - MWAKA - 2015

                                                         OR

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2015 - FORM FOUR (CSEE) EXAM RESULTS 2015  - NECTA 


MATOKEO YA KIDATO CHA NNE - FORM FOUR (CSEE) EXAM RESULTS  - NECTA - MWAKA - 2014

                                                           OR

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2014 - FORM FOUR (CSEE) EXAM RESULTS 2014 - NECTA


MATOKEO YA KIDATO CHA NNE - FORM FOUR (CSEE) EXAM RESULTS  - NECTA -MWAKA - 2013

                                                          OR                                    

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2013 - FORM FOUR (CSEE) EXAM RESULTS 2013  - NECTA


MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2012 - FORM FOUR (CSEE) EXAM RESULTS 2012  - NECTA

                                                          OR

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE - FORM FOUR (CSEE) EXAM RESULTS  - NECTA - MWAKA - 2012


Bofia Hapa: MATOKEO YA KIDATO CHA NNE - FORM FOUR (CSEE) EXAM RESULTS  - NECTA - MWAKA - 2011

                                                           OR

Bofia Hapa: MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2011 - FORM FOUR (CSEE) EXAM RESULTS 2011  - NECTA


Bofia Hapa: MATOKEO YA KIDATO CHA NNE - FORM FOUR (CSEE) EXAM RESULTS  - NECTA - MWAKA - 2010

                                                           OR

Bofia Hapa: MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2010 - FORM FOUR (CSEE) EXAM RESULTS 2010  - NECTA


Bofia Hapa: MATOKEO YA KIDATO CHA NNE - FORM FOUR (CSEE) EXAM RESULTS  - NECTA - MWAKA - 2009

                                                           OR

Bofia Hapa: MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2009 - FORM FOUR (CSEE) EXAM RESULTS 2009  - NECTA

 

Bofia Hapa: MATOKEO YA KIDATO CHA NNE/ FORM FOUR (CSEE) EXAM RESULTS  - NECTA - MWAKA - 2008


Bofia Hapa: MATOKEO YA KIDATO CHA NNE/ FORM FOUR (CSEE) EXAM RESULTS - NECTA - MWAKA - 2007


Bofia Hapa: MATOKEO YA KIDATO CHA NNE/ FORM FOUR (CSEE) EXAM RESULTS  - NECTA - MWAKA - 2006

 

Bofia Hapa: MATOKEO YA KIDATO CHA NNE/ FORM FOUR (CSEE) EXAM RESULTS  - NECTA - MWAKA - 2005

 

Bofia Hapa: MATOKEO YA KIDATO CHA NNE/ FORM FOUR (CSEE) EXAM RESULTS  - NECTA - MWAKA - 2004



Bofia Hapa: MATOKEO YA KIDATO CHA NNE/ FORM FOUR (CSEE) EXAM RESULTS  - NECTA - MWAKA - 2003