Monday, September 26, 2016
HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA CHUO KIKUU MWALIMU NYERERE 2016/2017
HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA CHUO KIKUU MWALIMU NYERERE 2016/2017
HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA CHUO KIKUU TUMAINI MAKUMIRA UNIVERSITY 2016/2017
MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA CHUO KIKUU TUMAINI MAKUMIRA UNIVERSITY 2016/2017
makumira-tcu-selection-2016-2017
makumira-tcu-selection-2016-2017
Undergraduate Admission degree Programme 2016/2017
Undergraduate Admission degree Programme 2016/2017
The following applicants have been selected to join various undergraduate degree programmes for the 2016/2017 academic year. The selected applicants should report at the Mwl. J.K. Nyerere Mlimani Campus on Saturday 8th October 2016 for the orientation week which will start on Monday 10th October 2016. Applicants selected for admission into Dar es Salaam University College of Education (DUCE) and Mkwawa University College of Education (MUCE) should report directly to the college's campuses in Chang'ombe and Iringa respectively on the same dates. Joining instructions and admission letters should be collected at the University campuses where one is admitted. Joining instructions and other important information can also be downloaded from the University website
Udsm
Udsm admission 2015/2016
Thursday, September 22, 2016
Sunday, September 18, 2016
Serikali kutoa ubani kwa wafiwa wa tetemeko Bukoba
SERIKALI imesema itatoa fidia ya Sh milioni 1.17 kwa kila familia
iliyofiwa na ndugu wakati wa tetemeko la ardhi lililotokea Septemba 10,
mwaka huu mkoani Kagera.
Taarifa hiyo ilitolewa bungeni jana na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, alipokuwa akisoma hotuba ya kuahirisha mkutano wa nne wa Bunge la 11.
“Kama Bunge lako tukufu lilivyojulishwa, Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, imechukua hatua kadhaa kushughulikia athari za tetemeko la ardhi lililotokea Septemba 10, mwaka huu.
“Pamoja na viongozi kutembelea maeneo yenye madhara, Serikali pia imewapatia chakula waathirika, imeimarisha Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera kwa kupeleka dawa na vifaa tiba kupitia Bohari Kuu ya Dawa na pia imepeleka timu ya wataalamu na madaktari 12 kutoka Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Bugando.
“Wananchi waliokosa kabisa hifadhi ya makazi, wamepewa maturubai na mahema kwa ajili ya makazi ya muda na waathirika ambao nyumba zao zimebomoka kabisa kwa kuanzia kila mmoja ametengewa mabati 20, saruji mifuko mitano pamoja na mablanketi na mikeka na kwa wapangaji waliokuwa katika nyumba hizo kila mmoja ametengewa kodi ya pango ya miezi sita ili apate mahali pa kujihifadhi.
“Tathmini ya uharibifu wa barabara imefanyika na barabara zilizoharibika zitarejeshwa katika hali yake ya kawaida ili wananchi waendelee kupata huduma za msingi huku Serikali ikiendelea kuchukua hatua za kukarabati miundombinu ya maji safi na maji taka.
“Pamoja na hayo, Serikali imewafariji wafiwa na kushiriki mazishi kwa kusaidia kutoa majeneza, sanda, usafiri na kutenga shilingi milioni 20 za rambirambi kwa wafiwa ambazo zitatolewa kwao muda wowote,” alisema Majaliwa.
Pia alizungumzia mwenendo wa ukusanyaji wa mapato serikalini na kusema Serikali imedhamiria kuongeza na kuimarisha ukusanyaji huo kwa kuchukua hatua mbalimbali.
Katika hatua nyingine, alisema katika mwaka wa fedha wa 2016/2017, mapato ya Serikali yanatarajia kuongezeka na kupunguza utegemezi wa kibajeti kutoka kwa washirika wa maendeleo huku ikiendelea kudhibiti utoaji wa misamaha ya kodi ili kuleta tija kwa Taifa.
“Katika mwaka wa fedha wa 2016/2017, Serikali imelenga kukusanya mapato ya ndani ikijumuisha mapato ya halmashauri ya jumla ya shilingi trilioni 18.46. Takwimu za mwenendo wa ukusanyaji wa mapato zinaonyesha kuwa katika kipindi cha kuanzia Julai hadi Agosti, mwaka huu, mapato yaliyokusanywa na TRA yalikuwa shilingi trilioni 2.168 ikilinganishwa na makadirio ya kukusanya shilingi trilioni 2.113,” alisema.
Taarifa hiyo ilitolewa bungeni jana na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, alipokuwa akisoma hotuba ya kuahirisha mkutano wa nne wa Bunge la 11.
“Kama Bunge lako tukufu lilivyojulishwa, Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, imechukua hatua kadhaa kushughulikia athari za tetemeko la ardhi lililotokea Septemba 10, mwaka huu.
“Pamoja na viongozi kutembelea maeneo yenye madhara, Serikali pia imewapatia chakula waathirika, imeimarisha Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera kwa kupeleka dawa na vifaa tiba kupitia Bohari Kuu ya Dawa na pia imepeleka timu ya wataalamu na madaktari 12 kutoka Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Bugando.
“Wananchi waliokosa kabisa hifadhi ya makazi, wamepewa maturubai na mahema kwa ajili ya makazi ya muda na waathirika ambao nyumba zao zimebomoka kabisa kwa kuanzia kila mmoja ametengewa mabati 20, saruji mifuko mitano pamoja na mablanketi na mikeka na kwa wapangaji waliokuwa katika nyumba hizo kila mmoja ametengewa kodi ya pango ya miezi sita ili apate mahali pa kujihifadhi.
“Tathmini ya uharibifu wa barabara imefanyika na barabara zilizoharibika zitarejeshwa katika hali yake ya kawaida ili wananchi waendelee kupata huduma za msingi huku Serikali ikiendelea kuchukua hatua za kukarabati miundombinu ya maji safi na maji taka.
“Pamoja na hayo, Serikali imewafariji wafiwa na kushiriki mazishi kwa kusaidia kutoa majeneza, sanda, usafiri na kutenga shilingi milioni 20 za rambirambi kwa wafiwa ambazo zitatolewa kwao muda wowote,” alisema Majaliwa.
Pia alizungumzia mwenendo wa ukusanyaji wa mapato serikalini na kusema Serikali imedhamiria kuongeza na kuimarisha ukusanyaji huo kwa kuchukua hatua mbalimbali.
Katika hatua nyingine, alisema katika mwaka wa fedha wa 2016/2017, mapato ya Serikali yanatarajia kuongezeka na kupunguza utegemezi wa kibajeti kutoka kwa washirika wa maendeleo huku ikiendelea kudhibiti utoaji wa misamaha ya kodi ili kuleta tija kwa Taifa.
“Katika mwaka wa fedha wa 2016/2017, Serikali imelenga kukusanya mapato ya ndani ikijumuisha mapato ya halmashauri ya jumla ya shilingi trilioni 18.46. Takwimu za mwenendo wa ukusanyaji wa mapato zinaonyesha kuwa katika kipindi cha kuanzia Julai hadi Agosti, mwaka huu, mapato yaliyokusanywa na TRA yalikuwa shilingi trilioni 2.168 ikilinganishwa na makadirio ya kukusanya shilingi trilioni 2.113,” alisema.
TCU yashusha viwango kujiunga vyuo vikuu
TUME ya Vyuo Vikuu nchini (TCU), imetangaza kushusha viwango vya
kujiunga na elimu ya juu (GPA) kwa wahitimu wa ngazi ya stashahada
kutoka 3.5 hadi 3.0.
Bila kueleza sababu ya kufikia uamuzi huo, TCU imesema kushushwa kwa viwango hivyo kumelenga kuruhusu idadi kubwa ya wanafunzi kudahiliwa katika vyuo vikuu mbalimbali nchini, huku vigezo vingine vikisalia kama vilivyokuwa awali.
Pamoja na hilo, TCU pia imeongeza muda wa udahili kuanzia Septemba 12 hadi 23 mwaka huu ili kutoa fursa kwa waombaji wenye sifa kuchagua tena kozi zenye nafasi baada ya zile walizoomba awali kujaa.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume hiyo, Eleuther Mwageni, alisema jumla ya walioomba nafasi katika awamu ya kwanza ni 55,347.
Alisema katika awamu hiyo iliyohusisha wanafunzi kutoka kidato cha sita na wenye vyeti kutoka nje ya nchi jumla ya waliodahiliwa ni 30,731 ambapo kidato cha sita ni 30,529 huku wenye vyeti kutoka nje ya nchi wakiwa ni 202.
Waliokosa nafasi katika awamu ya kwanza ni 24,616 ambapo 24,341 ni wale waliohitimu kidato cha sita na 275 ni wenye vyeti kutoka nje ya nchi.
Alisema katika jumla ya waombaji 55,347 walioomba wenye sifa za kudahiliwa ni 47,203 sawa na asilimia 85.3% waliopata ni 30,731 sawa na asilimia 65% waliokosa ni 16,472 sawa na asilimia 35% na wasiokuwa na sifa ni 8,144.
Mwageni alisema wengi waliokosa ni kutokana na kujaa kwa nafasi katika vyuo walivyoomba ambapo idadi kubwa ya waombaji kupendelea zaidi vyuo hivyo.
“Kwa mfano kozi zote zinazotolewa na Muhimbili na nyingi za Chuo cha Ardhi zimejaa, baadhi ya kozi zimekimbiliwa na waombaji wengi kuliko nafasi zilizopo katika vyuo hivyo,” alisema Mwageni.
Alizitaja kozi nyingine zilizojaa katika vyuo vilivyoombwa na idadi kubwa ya waombaji kuwa ni ualimu, udaktari wa binadamu, ufamasia, sayansi ya uthamini wa ardhi na sheria.
“Kozi ya ualimu katika Chuo Kikuu Kishiriki cha Dar es Salaam ilikuwa na waombaji 15,803 wakati nafasi ni 1,000 tu. Halikadhalika kozi ya sayansi ya uthamini wa ardhi ya Chuo Kikuu Ardhi ilikuwa na waombaji 4,599 wakati nafasi ni 100,” alieleza Mwageni.
Aliongeza kuwa waliokosa nafasi ni kutokana na ushindani uliopo kutokana na uhaba wa nafasi katika kozi hizo huku baadhi ya waombaji wakishindwa kuzingatia sifa linganishi.
“Kwa hali hiyo Tume imeongeza muda wa udahili kuanzia Septemba 12 hadi 23 mwaka huu kwa waombaji wenye sifa ili wapate fursa ya kuchagua tena kozi zenye nafasi,” aliongeza Mwageni.
Mapema Julai mwaka huu, Tume hiyo ilitangaza kuongeza viwango vya kujiunga na elimu ya juu kwa wanafunzi waliohitimu ngazi ya stashahada kutoka GPA 2.7 iliyokuwapo awali hadi 3.5.
Bila kueleza sababu ya kufikia uamuzi huo, TCU imesema kushushwa kwa viwango hivyo kumelenga kuruhusu idadi kubwa ya wanafunzi kudahiliwa katika vyuo vikuu mbalimbali nchini, huku vigezo vingine vikisalia kama vilivyokuwa awali.
Pamoja na hilo, TCU pia imeongeza muda wa udahili kuanzia Septemba 12 hadi 23 mwaka huu ili kutoa fursa kwa waombaji wenye sifa kuchagua tena kozi zenye nafasi baada ya zile walizoomba awali kujaa.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume hiyo, Eleuther Mwageni, alisema jumla ya walioomba nafasi katika awamu ya kwanza ni 55,347.
Alisema katika awamu hiyo iliyohusisha wanafunzi kutoka kidato cha sita na wenye vyeti kutoka nje ya nchi jumla ya waliodahiliwa ni 30,731 ambapo kidato cha sita ni 30,529 huku wenye vyeti kutoka nje ya nchi wakiwa ni 202.
Waliokosa nafasi katika awamu ya kwanza ni 24,616 ambapo 24,341 ni wale waliohitimu kidato cha sita na 275 ni wenye vyeti kutoka nje ya nchi.
Alisema katika jumla ya waombaji 55,347 walioomba wenye sifa za kudahiliwa ni 47,203 sawa na asilimia 85.3% waliopata ni 30,731 sawa na asilimia 65% waliokosa ni 16,472 sawa na asilimia 35% na wasiokuwa na sifa ni 8,144.
Mwageni alisema wengi waliokosa ni kutokana na kujaa kwa nafasi katika vyuo walivyoomba ambapo idadi kubwa ya waombaji kupendelea zaidi vyuo hivyo.
“Kwa mfano kozi zote zinazotolewa na Muhimbili na nyingi za Chuo cha Ardhi zimejaa, baadhi ya kozi zimekimbiliwa na waombaji wengi kuliko nafasi zilizopo katika vyuo hivyo,” alisema Mwageni.
Alizitaja kozi nyingine zilizojaa katika vyuo vilivyoombwa na idadi kubwa ya waombaji kuwa ni ualimu, udaktari wa binadamu, ufamasia, sayansi ya uthamini wa ardhi na sheria.
“Kozi ya ualimu katika Chuo Kikuu Kishiriki cha Dar es Salaam ilikuwa na waombaji 15,803 wakati nafasi ni 1,000 tu. Halikadhalika kozi ya sayansi ya uthamini wa ardhi ya Chuo Kikuu Ardhi ilikuwa na waombaji 4,599 wakati nafasi ni 100,” alieleza Mwageni.
Aliongeza kuwa waliokosa nafasi ni kutokana na ushindani uliopo kutokana na uhaba wa nafasi katika kozi hizo huku baadhi ya waombaji wakishindwa kuzingatia sifa linganishi.
“Kwa hali hiyo Tume imeongeza muda wa udahili kuanzia Septemba 12 hadi 23 mwaka huu kwa waombaji wenye sifa ili wapate fursa ya kuchagua tena kozi zenye nafasi,” aliongeza Mwageni.
Mapema Julai mwaka huu, Tume hiyo ilitangaza kuongeza viwango vya kujiunga na elimu ya juu kwa wanafunzi waliohitimu ngazi ya stashahada kutoka GPA 2.7 iliyokuwapo awali hadi 3.5.
Subscribe to:
Comments (Atom)








