Friday, April 29, 2016

Rais Magufuli amtumbua Mkurugenzi Mkuu TIC

RAIS John Magufuli ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Juliet Kairuki kwa sababu mbalimbali, ikiwemo kutochukua mshahara wake tangu alipoteuliwa mwaka 2013.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Profesa Adolf Mkenda, Dk Magufuli ametengua uteuzi huo rasmi kuanzia Aprili 24, mwaka huu. Profesa Mkenda alisema pamoja na mambo mengine, hatua hiyo imechukuliwa na Dk Magufuli baada ya kupata taarifa kuwa mkurugenzi huyo alikuwa hachukui mshahara wa serikali tangu alipoajiriwa, jambo lililozua maswali.
Aidha, kwa mujibu wa Profesa Mkenda, endapo Kairuki atakuwa tayari kuendelea kufanya kazi na Serikali ya Awamu ya Tano, atapangiwa kazi nyingine. Alisema kutokana na hatua hiyo, tayari mchakato wa kumpata Mkurugenzi mpya umeanza mara moja.
“Wakati mchakato huo ukiendelea kwa sasa Clifford Tandali atakaimu nafasi ya Mkurugenzi Mtendaji wa kituo hicho,” alisisitiza Katibu Mkuu huyo. Kairuki anakuwa Mkurugenzi wa pili wa mashirika ya umma kutenguliwa uteuzi wake baada ya Rais Magufuli juzi kutengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Dk Ally Simba.
Kairuki ni mtaalamu wa Sheria na masuala ya ubia kati ya Serikali na wawekezaji, na aliteuliwa kushika wadhifa huo Aprili 12, 2013 na Rais wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete kutoka katika Chama cha Mabenki Afrika Kusini akiwa ni Meneja Mkuu wa Idara ya Benki na Huduma za Fedha.

Thursday, April 21, 2016

Meya Chadema aomba Rais Magufuli aungwe mkono

MEYA wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita (Chadema) amesema ni wakati wa kuweka itikadi za siasa pembeni na kumuunga mkono Rais John Magufuli katika jitihadi zake za kuijenga nchi.
Pamoja na hayo, mameya wa manispaa mbalimbali za jiji hilo, wamebainisha kuwa wamepanga kufanya kazi kwa ushirikiano kwa lengo moja la kulijenga jiji hilo na kuwaletea wananchi wake maendeleo bila kujali itikadi zao za kisiasa.
Akizungumza katika uzinduzi wa daraja la kisasa la Nyerere jijini Dar es Salaam juzi, Mwita alisema kwa sasa Tanzania inahitaji umoja na mshikamano. “Baada ya harakati za uchaguzi zilizomalizika mwaka jana, sasa uchaguzi umeisha ni kipindi cha kujenga taifa letu.
Tukienda kwa mtindo wa kugawana mbao hatutojenga taifa hili,” alisisitiza diwani huyo wa Vijibweni katika wilaya mpya ya Kigamboni. Alisema ni wakati wa kumsaidia Dk Magufuli kwa kuhamasisha watu wote wanaostahili kulipa kodi walipe kodi hiyo, ikiwa ni pamoja na kubuni vyanzo vipya vya mapato.
Alisema ili Dar es Salaam ipate maendeleo lazima wananchi hasa wafanyabiashara walipe kodi. “Tunahitaji kujenga madaraja, shule na hospitali. Msidhani Rais ana uwezo wa kutoa fedha mbinguni kwa ajili ya kujenga taifa hili. Lipeni kodi tupate maendeleo,” alisisitiza.
Kwa upande wake, Meya wa Temeke, Abdallah Chaurembo (CCM) alisema kwa sasa Jiji la Dar es Salaam lina mameya wanne na wote wamejipanga kufanya kazi kwa maslahi ya wana Dar es Salaam na kuheshimu viongozi wote.
“Usiwe na mashaka na kuhusu utekelezwaji wa Ilani ya CCM katika jiji hili, kwani hata bajeti ya halmashauri zetu zimetumia vigezo vilivyopo kwenye Ilani hiyo,” alisema Chaurembo akimueleza Rais Magufuli.
Akizindua daraja hilo, Magufuli ambaye amekuwa akisisitiza utaifa mbele badala ya mambo ya vyama, alisema, “Nafikiri kama Wizara ya Ujenzi itakubali kutokana na historia ya daraja hili, wapo viongozi wetu waliofanya makubwa, waliunganisha watu zaidi ya makabila 200, tukapendana bila kubaguana kwa vyama, rangi, lugha wala dini...Na daraja hili halitabagua mtu wa kupita, halitabagua CCM wala Chadema, wote hawa watapita.”

HIACE YATUMBUKIA BAHARINI, YAUA WAWILI

DAR ES SALAAM WATU wawili wamefariki dunia baada ya kutumbukia baharini wakiwa ndani ya gari aina ya Toyota Hiace iliyokuwa imebebwa ndani ya Kivuko cha MV Kigamboni, Dar es Salaam. Tukio hilo la kusikitisha lilitokea jana, wakati kivuko hicho kikipakia abiria katika kituo cha Magogoni. Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo, Brown Mwakalago aliiambia MTANZANIA kuwa lilitokea saa 10 alfajiri ambapo mmoja wa waliofariki dunia ni dada yake, Nice Mwakalago (52) mkazi wa Tukuyu mkoani Mbeya. Akisimulia tukio hilo, Mwakalago alisema walitoka Mbeya kuja Dar es Salaam

Saturday, April 16, 2016

Nusu Fainali ya Uefa Europa League

3330EE6C00000578-0-image-a-15_1460716219507
Droo ya Nusu Fainali ya Uefa Europa League imefanyika na tayari timu nne zilizoingia katika hatua hiyo zimepangwa jinsi zitakavyokutana.
Villarreal imepangwa kuanza mechi ya kwanza ya hatua hiyo kwa kuikaribisha Liverpool wakati ambapo Shakhtar Donetsk itacheza dhidi ya Sevilla.
Nusu fainali ya kwanza inatarajiwa kuchezwa Aprili 28 wakati ambapo mechi za marudio za hatua hiyo zitachezwa Mei 5, 2016.
Fainali ya michuano hiyo inatarajiwa kuchezwa Mei 18, 2016 kwenye Uwanja wa St. Jakob-Park...


RATIBA YA NUSU FAINALI YA EUFA CHAMPIONS LEAGUE HII HAPA

RATIBA YA NUSU FAINALI YA EUFA CHAMPIONS LEAGUE HII HAPA

Tayari ratiba ya nusu fainali ya michuano ya UEFA Champions League imeshatoka baada ya kuchezeshwa draw ya kutafuta nani ataumana na nani kati ya vilabu vinne vilivyosalia kwenye michuano hiyo baada ya Jumanne na Jumatano kushuhudia vilabu vingine vinne vikiyaaga mashindano hayo ikiwa ni pamoja na bingwa mtetezi Barcelona.
Manuel Pellegrini atarejea kwenye klabu yake ya zamani baada ya Manchester City kujikuta ikitakiwa kupambana na miamba ya Hispania Real Madrid wakati Atletico Madrid watakwaana na kikosi cha Pep Guardiola Bayern Munich mechi ambazo zitapigwa April 26/27 na May 3/4.
Atletico Madrid v Bayern unatarajiwa kuwa mchezo wa ina yake uliojaa mbinu na ufundi mwingi kutokana na makocha wa timu hizo kufahamiana vizuri kwasababu walishawahi kuchuana kwenye ligi ya Hispania La Liga wakati Pep akiwa kocha wa klabu ya Barcelona. Kunauwezekano wa kuwepo fainali ya Madrid derby endapo vilabu vyote vya Hispania vitafuzu hatua ya fainali kitu ambacho kilitokea mwaka 2014.
Kitu kingine kizuri ni kwamba, endapo The Bavarians na Manchester City zitafuzu hatua ya fainali, Pep Guardiola atakutana na timu yake atakayoifundisha msimu ujao.

Sunday, April 10, 2016

Njia za Mawasiliano za Jeshi La Polisi Tanzania



NAMBA ZA MAKAMANDA WA POLISI  
MKOA JINA LA KAMANDA NAMBA ZA SIMU  
ARUSHA DCP  LIBERATUS  SABAS 0715 009 912  
MWANZA SACP JASTUS KAMUGISHA 0715 009 949  
KIGOMA SACP FERDINAND E. MTUI 0715 009 915  
RUKWA SACP JACOB MWARUANDA 0715 009 954  
KAGERA SACP AUGUSTINO OLLOMI 0715 009 916  
ILALA SACP LUCAS MKONDYA 0715 009 980  
KATAVI SACP DHAHIRI KIDAVASHARI 0715 009 957  
MOROGORO SACP ULRICH MATEI 0715 009 946  
DODOMA ACP LAZARO MAMBOSASA 0715 009 914  
MBEYA SACP AHMED MSANGI 0715 009 931  
KILIMANJARO ACP WILBROAD MTAFUNGWA 0715 009 923  
PWANI ACP BONAVENTURA MSHONGI 0715 009 953  
MTWARA ACP  HENRY MWAIBAMBE 0715 00 99 48  
SHINYANGA ACP MIKA NYANGE 0767 508 090  
MANYARA ACP FRANCIS MASSAWE 0715 009 929  
NJOMBE ACP PRUDENSIANA PROTAS 0658 376 495   
MARA ACP  RAMADHANI NG'AZI 0715 009 930  
SIMIYU ACP ONESMO   LYANGA 0658 37 64 81  
TANGA SACP LEONARD PAUL 0715 009 963  
LINDI ACP RENATA M. MZINGA (BI) 0715 009 927  
SINGIDA ACP THOBIAS G. SEDOYEKA 0715 009 959  
RUVUMA ACP ZUBERI MWOMBEJI 0715 00 99 56                            
TARIME RORYA ACP  GILLES MROTO 0715 009 964  
GEITA ACP MPONJOLI LOTSON 0658 376 488  
TEMEKE ACP ANDREW SATTA 0715 009 979  
KINONDONI ACP CHRISTOPHER FUIME O715 009 976  
TABORA ACP HAMISI SELEMAN  0715 009 961  
IRINGA ACP PETER KAKAMBA 0715 009 921  
       
       
MAKAMANDA WA VIKOSI NA VYUO VYA POLISI  
JINA LA KIKOSI JINA KAMILI SIMU
Kamanda wa kikosi cha Usalama Barabarani DCP  Mohamed Mpinga 0754 360 046
kamanda Bohari Kuu la Polisi DCP  Andrian  Magayane 0713 635 425
Mkuu wa Chuo cha Polisi Dar es salaam SACP Fulgence Ngonyani 0715 009 985
Kamanda kikosi cha Anga SACP Modestus Lyimo 0658 37 64 67
Kamanda kikosi cha Wanamaji SACP Mboje  Kanga 0658 481 002
Kamanda kikosi cha Ufundi  SACP Shabani M. Hiki 0713 629 824
Kamanda wa Polisi Tazara   Tazara  SACP Patrick   Byatao 0715 00 30 10
Kamanda wa  kikosi cha Ujenzi Ujenzi  SACP Richard Malika 0658 376 503
Kamanda wa Polisi Reli SACP Simon  Chillery 0658 69 99 96
Mkuu wa Shule ya Polisi Moshi  SACP Matanga Mbushi 0715 009 972
Mkuu wa kitengo cha kuzuia dawa za kulevya  ACP Mihayo Msikhela  
Mkuu wa Chuo cha Polisi Zanzibar SACP Deusdedit Nsimeki 0715 009 973
Kamanda wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU)  SACP Frasser Kashai 0719 222 101
Kamanda wa kikosi  cha Polisi Bendi ACP Adelgot Haule 0717 260791
Kamanda wa Polisi viwanja vya Ndege ACP  Martin Otieno 0658 444 488 
Kamanda kikosi cha Polisi Afya  ACP Paulo Kasabago 0713 63 26 91
Kamanda wa  Kikosi cha Kuzuia wizi wa Mifugo              ACP Simon C. Ngowi 0658 37 60 62
Mkuu wa Kikosi cha Mbwa na Farasi SSP DK Eugen Emmanuel 0782 078 503
       
       
       
  MAKAO MAKUU YA JESHI LA POLISI  
Inspekta Jenerali wa Polisi Tanzania IGP Ernest  Mangu 0789 94 94 95
Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi DIGP Abdulrahmani Kaniki 0658 90 01 26
Kamishina wa Fedha na Logistics CP Albert Nyamhanga 0786 02 98 96
Kamishina wa Operesheni na Mafunzo CP  Nsato Marijani  0658 48 10 03
Kamishina wa Polisi  jamii CP  Mussa Alli Mussa 0782 41 72 47
Kamishina wa Utawala na Utumishi CP Thobias  Andengenye 0688 88 33 73
Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai CP Diwani Athumani 0 715 32 34 44
Kamishna wa Uchunguzi wa Sayansi ya Makosa ya Jinai  CP Elice Mapunda 0719 11 40 00
Kamishna wa Intelijensia ya Jinai CP Robert Boaz  0677 88 51 00
Mkuu wa ufuatiliaji na Tathmini  DCP Mpinga Gyumi 0658 27 10 02
Mkuu wa Kitengo cha Miradi ya Maendeleo na Ununuzi DCP Sospeter Kondela 0713  63 58 40
Mkuu wa  Mafunzo   DCP Ally Lugendo 0754 59 44 50
Afisa Mnadhimu Makao  Makuu ya Upelelezi DCP Faustine Shilogile 0786 28 32 55
Mkuu wa operesheni za Polisi DCP Jackson Daniel Nyambabe 0658 47 05 02
Mkuu wa Mipango na Bajeti SACP Francis Massawe  
Mkuu wa Mahusiano ya Kimataifa SACP  Germanus  Muhume 0713 63 36 17
Mkuu wa Interpol    SACP Gustavus Babile 0754  28 89 72
Mkuu wa  Fedha   SACP Ndallo Shihango 0754 50 79 18
Mkuu wa kitengo cha Teknohama ACP Mkungu 0677 00 43 32
Mkuu wa Dawati la jinsia na watoto ACP Tatu Mfaume  
Afisa Mnadhimu Makao Makuu ya Polisi ACP Akili Mpwapwa 0754 47 08 92
Mhasibu Mkuu  wa Jeshi la Polisi Bw. Frank Msaki 0754 49 42 86
Msemaji wa Jeshi la Polisi SSP Advera Bulimba 0758 00 98 61
Meneja Mkuu Bwalo la Maafisa Oystarbay INSP Antonin Mkundi 0655 83 15 25
Kitengo cha maadili na malalamiko   0732 92 20 68/ 0677 99 99 99
       
       
  KANDA MAALUM YA POLISI DAR ES SALAAM  
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum DSM   CP Simon Sirro 0686 28 09 94
Mkuu wa Utawala na Fedha Kanda Maalun   DCP Hezron Gimbi 0677 88 51 03
Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalumu ACP Camilius Wambura 0658 11 11 00
Mkuu wa Kikosi cha Polisi 999 DSM SP  George  Daniel 0713 32 39 99
Simu ya Dharura     111 /112
Chumba cha 999     0787 66 83 06
       
       
  KAMISHENI YA POLISI  ZANZIBAR  
Kamishina wa Polisi Zanzibar CP  Hamdani Makame 0754 41 26 90
Naibu Mkurugenzi  wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Zanzibar DCP Salum Msangi 0713 37 07 30
       
       
       
  MAKAMANDA WA POLISI MIKOA YA ZANZIBAR
Kaskazini Pemba SACP Hassan Nassiri Ali 0715 00 99 17  
Kusini Unguja ACP Juma Saadi Khamis 0715 00 99 25  
Mjini Magharibi ACP Mkadam Khamis Mkadam 0715 00 99 39  
Kusini Pemba ACP Mohamed S. Mohamed 0715 00 99 24  
Kaskazini Unguja ACP Hassan M. Msangi 0715 00 99 18  
       
     

Rais wa Zanzibar achagua mawaziri 13

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein ametangaza Baraza la Mawaziri lenye wizara 13.
Baraza hilo lina sura mpya nane, likiwajumuisha wajumbe kutoka katika vyama vya siasa vya upinzani, wanasiasa mashuhuri visiwani humo, huku naibu mawaziri saba wote wakiwa wageni katika nafasi hiyo.
Akitangaza majina hayo jana, Dk Shein anayeianza awamu ya pili ya utawala wake Zanzibar, alimtangaza Dk Halid Salum Mohammed, ambaye ni Mwakilishi wa Jimbo la Donge, kuwa Waziri wa Fedha na Mipango.
Katika awamu iliyopita, Dk Halid alikuwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais.
Riziki Pembe Juma, Mwakilishi wa Viti Maalumu, ameteuliwa kuwa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali, wakati Moudin Castico, Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi aliyeteuliwa na Rais, anakuwa Waziri wa Kazi, Uwezeshaji Wazee, Wanawake na Watoto.
Wengine ni Rashid Ali Juma, Mwakilishi wa Jimbo la Amani ambaye ameteuliwa kuwa Waziri wa Habari, Utangazaji, Utalii na Michezo.
Balozi Ali Karume, mmoja wa wanasiasa mashuhuri Zanzibar, ambaye kwa sasa ni Mwakilishi wa Kuteuliwa na Rais, yeye ameteuliwa kuwa Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, huku Salama Aboud Talib, ambaye ni Mwakilishi wa Viti Maalumu na Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wanawake nchini (UWT), akiteuliwa kuwa Waziri wa Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira.
Balozi Amina Salum Ali aliyeshika nafasi ya pili, baada ya Rais John Magufuli, katika mchakato wa kumpata mgombea urais kwa tiketi ya CCM mwaka jana, yeye ameteuliwa kuwa Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko.
Wapinzani ndani
Dk Shein pia amemteua Hamad Rashid Mohammed, ambaye ni Mwenyekiti wa chama cha ADC, ambaye pia amewahi kuwa kiongozi wa ngazi za juu wa CUF, kuwa Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi.
Hamad pia ndiye aliyeibuka katika nafasi ya pili katika Uchaguzi Mkuu wa marudio wa Zanzibar kwa kupata kura 6,734 baada ya Rais Shein aliyeibuka na ushindi mnono wa kura 299,982 sawa na asilimia 91.4.
Waziri huyo wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi alifuatiwa kwa karibu na mgombea urais wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad aliyepata kura 6,076. Viongozi wengine kutoka vyama vya upinzani walioteuliwa katika Baraza la Mawaziri ni Said Soud Said kutoka AFP na Juma Ali Khatib kutoka TADEA, ambao wanakuwa mawaziri wasiokuwa na wizara maalumu.
Mawaziri wa zamani
Mawaziri wanaoendelea na nyadhifa zao ni Haji Omar Kheir aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalumu za Serikali, huku Issa Haji Ussi Gavu ambaye katika kipindi kilichopita alikuwa Naibu Waziri wa Mawasiliano na Miundombinu, amepanda na kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Baraza la Mapinduzi.
Mwakilishi wa Jimbo la Makunduchi, Haroun Ali Suleiman, ameteuliwa kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Katiba, Sheria na Utawala Bora).
Mohammed Aboud Mohamed ambaye katika kipindi kilichopita alikuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, anaendelea na wadhifa wake huo bila ya mabadiliko, huku Mahmoud Thabit Kombo Jecha, ambaye ni Mwakilishi wa Kiembesamaki akipandishwa kutoka Naibu Waziri wa Afya kuwa waziri kamili wa wizara hiyo.
Naibu Mawaziri Dk Shein ameteua naibu mawaziri saba wote wakiwa ni wapya akiwemo Lulu Msham Khamis kuwa Naibu Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi na Harusi Said Suleiman kuwa Naibu Waziri wa Afya.
Chum Kombo Khamis, ameteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Habari, Utangazaji, Utalii na Michezo na Mmanga Mjengo Mjawiri ameteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali.
Wengine ni Juma Makungu Juma ambaye amechaguliwa kuwa Naibu Waziri wa Ardhi, Maji, Ujenzi, Nishati na Mazingira, huku Khamis Juma Maalim, akiwa Naibu Waziri wa Katiba na Sheria na Mohammed Ahmed Salum akiteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Ujenzi.
Waliotemwa
Mawaziri waliotemwa ni pamoja na Dk Mwinyihaji Makame, Mwakilishi wa Dimani ambaye katika baraza lililopita alikuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu na aliyekuwa Waziri wa Fedha, Omar Yussuf Mzee.
Mwingine ni Dk Sirra Umbwa Mamboya ambaye katika baraza lililopita alikuwa Waziri wa Kilimo na Maliasili na katika Baraza la Wawakilishi alikuwa Mjumbe wa Kuteuliwa na Rais, ambaye mwaka huu hakupata uteuzi wowote.
Kwa mujibu wa taarifa ya Ikulu iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Dk Abdulhamid Yahya Mzee, Rais ataapisha mawaziri wapya na naibu mawaziri leo Jumapili Ikulu kwa ajili ya kuanza kutekeleza majukumu yao mapya kwa mujibu wa Katiba.
Lawama za SUK
Baada ya kutangaza mawaziri hao, Dk Shein alisema Serikali ya Umoja wa Kitaifa, imekwama kutokana na matakwa ya wananchi na si kikatiba.
Amefafanua kuwa tatizo ni vyama vya siasa ikiwemo CUF, kukacha kushiriki kikamilifu katika Uchaguzi Mkuu wa Marudio Machi 20, mwaka huu na kusisitiza hatishwi na uamuzi wa chama hicho na vingine vya upinzani kutoitambua Serikali yake.
“Kukwama kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa si kikatiba ni matakwa ya wananchi ambao waliamua kupigia Chama Cha Mapinduzi kura nyingi na kushinda katika majimbo yote ya uchaguzi Unguja na Pemba. “Tatizo hapa lipo kwa vyama vya siasa vilivyoamua kususia uchaguzi wa marudio ambao uliitishwa kwa mujibu wa Katiba na sheria za Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar ZEC,” alisema.
Dk Shein alisema Serikali ya Umoja wa Kitaifa ambayo ameiongoza kwa miaka mitano, imetekeleza majukumu yake vizuri licha ya kuwepo kwa hitilafu ndogo ndogo alizoziita ni za kawaida.
Pamoja na kuwepo kwa changamoto hiyo ya kukwama kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa, iliyotokana na hatua ya makusudi ya CUF ya kutoshiriki katika uchaguzi wa marudio, Dk Shein amesema hatabadilisha vifungu vya Katiba kwa ajili ya kuruhusu na kutoa nafasi ya muundo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa kama ilivyokuwa awali.
Kutambuliwa na Mungu
Alisema hababaishwi na kauli za CUF zilizotolewa na Maalim Seif za kutoitambua serikali yake na kusisitiza Serikali yake inatambuliwa na Mungu ambaye ameipa baraka zote pamoja na wananchi wa Unguja na Pemba ambao ndiyo walioipigia kura kwa wingi na kuipa nafasi ya kushika hatamu ya madaraka.
“Serikali yangu inatambuliwa na Mwenyezi Mungu kutokana na kudra zake na anayesema haitambui basi hiari yake, lakini mimi nawapongeza wananchi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi, ambao wamenipigia kura za ndiyo kwa ajili ya kunipa ridhaa ya kushika hatamu ya kuongoza dola,” alisema.