Tuesday, March 29, 2016

Agizo la Magufuli kwa MaRC mwisho leo

SIKU 15 alizotoa Rais John Magufuli kwa wakuu wa mikoa, wawe wamejumlisha wafanyakazi wote na kuhakikisha wanaondoa wafanyakazi hewa, zimetimia leo. Baadhi ya mikoa imeanika idadi ya watumishi hewa, waliobainika kupitia uhakiki huo, lakini mingi haijafanya hivyo.
Agizo hilo la Rais Magufuli ni sehemu ya maagizo kadhaa aliyotoa Machi 15 mwaka huu wakati akiwaapisha wakuu hao wa mikoa jijini Dar es Salaam; ambao aliwasisitiza kuwa ili mradi wamekubali kushika wadhifa huo, wameingia kwenye mtego.
Pamoja na majukumu mengine waliyopewa kuhakikisha wanayatekeleza katika uongozi wao, suala la watumishi hewa ni mtego unaowakabili wakuu hao wa mikoa wakipaswa kujinasua nao ndani ya wiki hii ambao siku zilizotolewa zimefika ukomo; Vinginevyo, wataweka rehani nyadhifa zao.
Majukumu mengine ambayo wakuu hao wa mikoa walipewa na Rais wahakikishe wanayatekeleza, ni pamoja na kukabili ujambazi hususan wakuu wa mikoa ya pembezoni inayokabiliwa na tatizo la utekaji magari kiasi cha serikali kuamua kuweka utaratibu wa polisi kuyasindikiza.
Mengine ni kukabili watu wazembe, watendaji wanaowanyanyasa wananchi, njaa, kodi za mazao, migogoro ya ardhi na kuhakikisha wanasimamia mpango wa elimu bure unafanikiwa.
Tangu Rais atoe maelekezo hayo ya kukabili wafanyakazi hewa, mikoa mbalimbali inaendelea na mchakato wa kuhakiki wafanyakazi kwenye idara na taasisi mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kuwataka watumishi kuwasilisha nyaraka mbalimbali ikiwemo barua za ajira.
Katika mchakato huo ambao umezaa matunda kwa kubaini watumishi hewa waliokuwa wakilipwa mishahara, baadhi ya halmashauri zililazimika kufuta huku baadhi ya halmashauri zimeamuru watumishi wake walio masomoni na kwenye likizo, warudi mara moja katika vituo vyao vya kazi kuhakikiwa.
Madudu yaibuliwa Miongoni mwa mikoa ambayo imetoa taarifa za uhakiki ni pamoja na mkoa wa Dodoma, ambao umetajwa kuwa na watumishi hewa 144. Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Jordan Rugimbana, ameagiza kupelekewa orodha ya watumishi hao na wakati huo huo kupatiwa maelezo kwa nini kuna watumishi hewa na kutaka kupatiwa orodha za watumishi hao.
Akizungumza hivi karibuni wakati wa makabidhiano ya ofisi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Chiku Gallawa aliyehamia Mkoa wa Songwe, Rugimbana alisema uhakiki wa watumishi wa serikali umebaini uwepo wa idadi hiyo ya watumishi hewa .
Mkoa wa Kigoma pia ni miongoni mwa mikoa ambayo taarifa zake za uhakiki zimeshatolewa ambako imebainika kuwapo watumishi hewa 169 kwa kipindi cha mwaka uliopita.
Hata hivyo Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Emanuel Maganga amewataka wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wote waliopo katika halmashauri zote kutaja kiasi cha fedha kilichotumika kulipa mishahara watumishi hewa hao 169 ndani ya kipindi hicho cha mwaka mmoja uliopita.
Kwa mujibu wa Mkuu wa Mkoa huo wa Kigoma, watumishi hewa waliowabaini, wamo waliokwishafukuzwa, waliofariki na wengine wasiokuwa na sifa za kuwa watumishi wa umma.
Maganga ametaka fedha walizokuwa wakilipwa watumishi hao hewa kwa ajili ya mishahara, zirudi na wakati huo huo wakurugenzi wawafute kwenye orodha ya malipo.
Halmashauri za mkoa wa Kigoma zenye watumishi hewa na idadi yake kwenye mabano ni Kasulu (78), Kigoma (23), Manispaa ya Kigoma Ujiji (29), Buhigwe (11), Uvinza (19), Kibondo (5) na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa yenye watumishi hewa wanne.
Halmashauri ya Kakonko ndiyo pekee isiyo na mtumishi hewa. Akizungumza na mwandishi wa gazeti hili jana, Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Evarist Ndikilo, alisema leo ambayo ndiyo ukomo wa muda aliotoa Rais, atatoa taarifa kamili ya kazi hiyo ya kuhakiki wafanyakazi na kuondoa wafanyakazi hewa watakaokuwa wamebainika.
Ndikilo alisema, ipo timu inayo endelea kufanya uhakiki kwenye wilaya mbalimbali kwa kushirikiana na wakurugenzi wa halmashauri. Likizo zaahirishwa Kwa upande wa mkoa wa Dar es Salaam, Halmashauri ya wilaya ya Temeke ililazimika kuwaita watumishi wake walioko masomoni na likizo kurudi mara moja katika vituo vyao vya kazi wahakikiwe.
Msemaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Temeke, Joyce Nsumba alisema hivi karibuni uhakiki uliendelea kwa makundi mbalimbali wakiwemo watumishi kutoka Idara ya Afya, Elimu, Fedha na Biashara, Kilimo, Mifugo, Ujenzi na Maendeleo ya Jamii.
Wakati anazungumza na mwandishi wa habari hizi hivi karibuni, Nsumba alisema walishahakiki watumishi 8,000. Sababu za uhakiki Uamuzi wa Rais Magufuli kuamuru ufanyike uhakiki, ulitokana na uchunguzi uliofanywa katika mikoa ya Singida na Dodoma katika halmashauri 14 na kugundulika kwa watumishi hewa 202 wanaolipwa mishahara.
Aliagiza uhakiki kwa watumishi wote katika wizara, mikoa, wilaya, idara,taasisi na Wakala za Serikali ndani ya siku 15. “Sasa niwaombe ndugu zangu wakuu wa mikoa, najua mtakwenda kuwapa maagizo wakurugenzi na wakuu wa wilaya.
Lakini niwape muda, ndani ya siku 15, wawe wamejumlisha wafanyakazi wote, wamewatoa wafanyakazi hewa,” ali waagiza. Rais Magufuli alisema mshahara ujao, ikigundulika kuwapo wafanyakazi hewa kwenye orodha ya malipo, mkurugenzi husika ajihesabu hana kazi na atafikishwa mahakamani.
Vile vile amewaambia mawaziri, hususan Waziri wa Fedha na Mipango aliyekuwapo kwenye hafla hiyo, wakawaeleze watendaji kwenye wizara zao na taasisi mbalimbali wahakikishe wanawaondoa wafanyakazi hewa ndani ya siku 15 na wasipotimiza agizo hilo hatua zitakuwa ni zilezile kwani sheria ni msumeno.
Alisema inasikitisha kuona fedha zinazokusanywa haziendi kwenye miradi inayopangwa, badala yake sehemu kubwa inatumika kulipa mishahara ikiwemo hewa. Alisema kwa ujumla Serikali inalipa mishahara kila mwezi kwa watumishi wake wa umma jumla ya Sh bilioni 549 mpaka bilioni 550.
Alisema kwa hali ilivyo, fedha nyingi zinaishia kwenye mishahara feki. Nawapa Ma-RC siku 15 mhakikishe Wakurugenzi wa halmashauri zote wamejumlisha idadi ya wafanyakazi wote waliopo na kuondoa wafanyakazi hewa katika halmashauri zao,” alisisitiza Rais Magufuli.
Mikoa ya Tanzania Bara ni: Arusha, Dar es Salaam, Dodoma, Tanga, Lindi, Mtwara, Ruvuma, Iringa, Njombe, Mbeya, Songwe, Rukwa, Katavi, Kigoma, Kagera, Geita, Mwanza, Simiyu, Shinyanga, Singida, Tabora, Pwani, Manyara, Mara, Morogoro na Kilimanjaro

Friday, March 25, 2016

Kuapisha kwa rais wa zanzibar

RAIS Ali Mohammed Shein ameapa kuiongoza tena Zanzibar huku akiahidi kuunda serikali itakayowaunganisha Wazanzibari wote.
Uundwaji wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) ni jambo linalosubiriwa kwa hamu na wananchi, kuona kama Dk Shein baada ya kushinda kwa zaidi ya asilimia 90, ataunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa.
Hiyo ni kutokana na Chama cha Wananchi (CUF) ambacho ni chama kikuu cha upinzani, kususia uchaguzi wa marudio uliompa ushindi wa kishindo Dk Shein kwa kile wanachodai kuwa hawawezi kushiriki uchaguzi haramu ambao matokeo yake ni kubakwa kwa demokrasia.
Lakini Dk Shein wakati amemaliza kuapa na kusomewa dua na viongozi mbalimbali wa dini kutoka madhehebu ya Kiislamu, Wakatoliki na Anglikana kwenye Uwanja wa Amaan mjini Unguja jana, aliwahakikishia Wazanzibari kuwa ataendelea kuulinda umoja wao kwa kushirikiana na vyama vya upinzani ili kuiletea Zanzibar maendeleo.
“Vyama vya upinzani vimenipa imani kubwa hasa kutokana na maelezo yao waliyoyatoa siku ya kutangazwa matokeo, ujumbe wao ni wa kuijenga Zanzibar na mimi naahidi kuwa nitashirikiana nao bila ubaguzi wowote,” alisema Dk Shein anayeongoza muhula wake wa pili na wa mwisho kikatiba.
Alisema serikali atakayoiunda itaheshimu misingi ya utawala bora, haki za binadamu na hivyo aliwaomba wananchi wamuunge mkono kwa kufanya kazi ili wajiletee maendeleo kwa kuwa uchaguzi tayari umeshaisha.
“Uchaguzi umeisha, sasa tushirikiane wote kuijenga Zanzibar yetu, kila mtu akafanye kazi maana kila mtu mchango wake ni muhimu kwa ustawi wa nchi yetu,” alisema Dk Shein.
Pia alitoa mwito kwa wananchi kuendelea kuitunza amani iliyopo huku akionya kuwa serikali yake ile ya Muungano haitakuwa na uvumilivu kwa mtu au kikundi kitakachojaribu kuvuruga amani iliyopo.
Hata hivyo, aliahidi kutoa mwelekeo wa Serikali yake atakapokuwa anazindua Baraza la Mapinduzi Zanzibar hivi karibuni. Hali ilivyokuwa Amaan Jina la Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha ndilo lililoshangiliwa kwa nguvu na wafuasi wa CCM waliofurika kwenye Uwanja wa Amaan wakati wa shughuli ya kumwapisha Dk Shein.
Jecha aliyejitokeza akiwa kwenye jopo la watu mashuhuri ambao waliitwa kwenda kwenye jukwaa maalumu, lililoandaliwa kwa ajili ya Rais Mteule kuapa, alishangiliwa kwa nguvu wakati anashuka kwenda jukwaa hilo.
Jopo hilo lilihusisha Spika wa Baraza la Wawakilishi, Katibu wa Baraza la Wawakilishi, Katibu Kiongozi, viongozi wa dini pamoja na viongozi wengine liliongozwa na Jaji Mkuu wa Zanzibar, Omar Othman Makungu.
“Jecha, Jecha, Jecha,” wananchi waliimba jina hilo mara kwa mara wakati anaenda kwenye jukwaa hilo na wakati wanarudi baada ya kumaliza shughuli za kumwapisha Rais Shein. Jina la Jecha limekuwa maarufu baada ya kutangaza kufuta uchaguzi wa Oktoba 25, 2015.
Tangu atoe tangazo hilo, hawakuwahi kuonekana hadharani hadi juzi alipojitokeza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi wa marudio. Kufutwa kwa uchaguzi huo, kumefanya kuwepo na mpasuko mkubwa wa kisiasa visiwani hapa baada ya CUF ambacho ni chama kikuu cha upinzani kutangaza kususia kushiriki marudio ya uchaguzi uliofanyika Machi 20, 2016.
Maelfu ya watu walifurika katika uwanja wa Aman kushuhudia tukio hilo la kihistoria, lakini kwa bahati mbaya zaidi wengi wa watu hawakupata nafasi ya kuingia ndani na hivyo kulazimika kubaki nje na kusikiliza sherehe hizo kupitia vipaza sauti vilivyofungwa uwanjani hapo.
Kikundi cha Culture kilikuwepo kutumbuiza sherehe hizo. Nyimbo zake za ‘aliyepewa kapewa, hapokonyeki, hata ukifanya chuki unajisumbua’ na ule wa ‘unaomba radhi ya nini wakati uliyokusudia hayakuwa’, zilipamba sherehe hizo na kushangiliwa kwa nguvu na wananchi.
Sherehe hizo pia zilipambwa na gwaride la vikosi vya Jeshi la Ulinzi wa Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Polisi, Kikosi Maalumu cha Kuzuia Magendo (KMKM), Mafunzo na Jeshi la Kujenga Uchumi (JKU).
Vikosi hivyo vilichora herufi ya A ambacho ni kifupi cha neno la Kigiriki la Alfa, ambalo maana yake ni mwanzo. Kuapishwa kwa Dk Shein jana ni mwanzo wa kuiongoza Zanzibar kwa muhula wa pili akiwa Rais wa Awamu ya Saba ya Zanzibar.
Marais wengine waliowahi kuiongoza Zanzibar tangu Mapinduzi ya mwaka 1964 ni Abeid Amani Karume, Aboud Jumbe, Ali Hassan Mwinyi, Abdul Wakil, Salmin Amour na Amani Abeid Karume.

Ndege yakamatwa ilikuwa ikisafilisha tumbili

WAKATI Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe akiwasimamisha kazi mara moja wakurugenzi wanne na mameneja saba wa Kanda wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) na Idara ya Wanyamapori kutokana na usimamizi mbovu wa rasilimali za nchi, ndege iliyokuwa ikisafirisha tumbili 61 nje ya nchi imekamatwa.
Mbali ya ndege hiyo ya mizigo ya Afrika Kusini, serikali inawashikilia watu kadhaa kwa kosa la kutaka kusafirisha nyani hao, rubani wake na watu waliohusika kutoa vibali vya kusafirisha nyani hao kinyume cha sheria.
Aidha, Profesa Maghembe amesema magogo yenye thamani ya Sh milioni 500 yaliyokuwa yamekatwa katika msitu wa Kalambo wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa hivi karibuni, yametekezwa kwa moto na kuisababishia hasara serikali.
Waliosimamishwa kutoka TFS ni Mtendaji Mkuu wa Wakala huo, Juma Mgoo, Mkurugenzi Rasilimali Misitu, Zawadi Mbwambo na Mkurugenzi wa Matumizi Rasilimali Misitu, Nurdin Chamuya huku aliyesimamishwa kutoka Idara ya Wanyamapori ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Wanyamapori Matumizi Endelevu, Dk Charles Mulokozi.
Baada ya kuwasimamisha hao amewateua watu wengine kushika nafasi zao wakati mchakato wa kuwapata watendaji wapya ukifanyika na walioteuliwa kukaimu nafasi hizo ni Kaimu Mtendaji Mkuu TFS, Gerald Kamwendo, Kaimu Mkurugenzi Rasilimali Misitu, Mwanaidi Kijazi, na Kaimu Mkurugenzi wa Matumizi Rasilimali Misitu, Haji Mpya na Kaimu Mkurugenzi upande wa Utawala, Emmanuel Winfred.
Profesa Maghembe alisema amewasimamisha kazi vigogo hao kwa kushindwa kusimamia na kudhibiti uvunaji haramu wa magogo, kusimamia ukusanyaji wa mapato na kushindwa kudhibiti usafirishaji wa wanyamapori.
Mbali na wakurugenzi hao, pia amewasimamisha kazi mameneja saba wa kanda wa TFS kwa kushindwa kusimamia ukusanyaji mapato yatokanayo na misitu katika maeneo yao.
Waliosimamishwa kazi na kanda zao katika mabano ni Hubert Haule (Kusini), Bakari Rashid (Mashariki), Cuthbert Mafipa (Kaskazini), Emmanuel Minja (Magharibi), Haji Khatibu (Ziwa) na Bruno Mallya (Nyanda za Juu Kusini).
Profesa Maghembe alisema amewasimamisha kazi maofisa hao kwa kushindwa kusimamia na kudhibiti uvunaji haramu wa magogo aina ya mkurungu na kusababisha uharibifu mkubwa katika Msitu wa Kalambo.
Jambo lingine ni ukusanyaji mapato ya serikali yatokanayo na misitu, lakini wakashindwa kuyapeleka benki na waliopeleka walipeleka kiwango kidogo kuliko walichokusanya na wengine hawakupeleka kabisa mapato hayo.
Kuhusu Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Wanyamapori Matumizi Endelevu, Dk Mulokozi, alisema amemsimamisha kazi kupisha uchunguzi kutokana na kutoa kibali cha kusafirisha nyani 61 kati ya 450 waliokamatwa katika maeneo mbalimbali ya Kilimanjaro na Arusha wakati alimpa maelekezo ya kutokutoa vibali hivyo kwa siku nane.
Mapato
Kuhusu mapato, alisema Januari mwaka huu aliagiza kufanyika ukaguzi wa makusanyo ya fedha, zilizotokana na mapato ya maliasili na namna mameneja wa TFS walivyoshiriki kukusanya fedha na kuziwasilisha serikalini.
Alisema Kamati iliundwa kuchunguza ukusanyaji wa mapato katika kanda mbalimbali. Alisema kamati hiyo ilibaini mapungufu makubwa na ilitoa mapendekezo ya kufanyiwa kazi.
“Kamati imepitia na wametoa maelekezo zichukuliwe hatua za kinidhamu mapema iwezekanavyo.Wale ambao wa kufukuzwa kazi wafukuzwe, wale wa kusimamishwa kazi na wasimamishwe na kushtakiwa na wale wa kupata makaripio makali wapate,” alisema Profesa Maghembe.
Aliongeza kuwa licha ya mapendekezo hayo, TFS haikuchukua hatua zozote juu ya watumishi hao. Waziri huyo alisema anaona biashara zinaendelea kama kawaida bila hatua zozote.
Magogo.
Alisema hivi karibuni walipokea taarifa ya uvunaji wa magogo katika msitu wa Kalambo kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Kalambo, William Ndile na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Magalula Magalula wakiomba msaada wa wizara juu ya udhibiti ilhali TFS ikiwa kimya.
Alisema baada ya taarifa hiyo, ilitumwa timu maalumu ya kuchunguza makosa makubwa kwenda kufanya uchunguzi.
Alisema timu hiyo iliona ni kweli magogo jamii ya mninga, yanakatwa na kutayarishwa huko huko na kisha kupakiwa katika makontena na kufungwa na rakili ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na nyaraka zinatengenezwa Zambia kwa kuwa Tanzania hairuhusu kusafirisha magogo nje ya nchi.
“Kwa kuwa inajulikana sisi kwa sheria zetu hairuhusiwi kusafirisha magogo nje ya nchini, rakili inafungwa huko huko porini na nyaraka zinatoka Zambia na wakati mwingine makontena hayo hupitishiwa Zambia na kuingizwa nchini na kupitishwa hadi bandarini,” alibainisha Waziri.
Alisema yote hayo yalikuwa yakifanyika huku TFS wakifahamu juu ya uvunaji huo wa magogo, ambao Meneja wa Wilaya na Mkoa walikuwa na taarifa na hata yeye alipofika huko, alishuhudia uharibifu huo wa misitu.
Alisema kuwa aliagiza magogo hayo, yaliyopo msituni yatolewe msituni, yapelekwe Matai yaliko makao makuu ya wilaya kwa ajili ya kuyapiga mnada ili fedha zake zikasaidie shughuli nyingine za serikali kama kununua vifaa tiba.
Lakini baada ya wao kuondoka huko Machi 9, mwaka huu na kudhani kuwa magogo yote sasa yatakuwa yametolewa hadi Matai ili uandaliwe utaratibu wa kuyapiga mnada, ameambiwa kuwa magogo yale yamemwagiwa petroli na kuchomwa moto yakiwa na thamani ya Sh milioni 500.
“Kwa wiki mbili tangu tuagize magogo haya yawe yametolewa msituni, kama TFS wangechukua hatua haraka za kutoa magogo hayo, fedha za serikali zisingeweza kuchomwa moto na kukaa kuhangaika kupata fedha za kununulia dawa wananchi,” alieleza Profesa Maghembe.
Alisema kuna matatizo mengi katika TFS katika uvunaji wa misitu na wamekuwa wakifanya uchunguzi. Alisema kuna wavunaji misitu husafirisha mazao hayo kwa kutumia vivuli vya vibali, badala ya vibali halisi.
Maeneo mengine aliyoyasema yana matatizo ni katika vivuko vya ukaguzi, ambako alisema wapo watu ambao hawalipishwi ushuru kutokana na urafiki wao.
Hivyo alisema wamekubaliana na serikali, kubadilisha uongozi wa TFS ili kupata watu wengine, watakaoweza kusimamia vyema mapato ya serikali na rasilimali za misitu.
Nyani (tumbili)
Katika tukio lingine, Profesa Maghembe alisema juzi usiku kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), wamekamata watu wakitaka kusafirisha nyani ‘Velvety Monkey’ 61 kwenda nje ya nchi kwa kutumia ndege ya mizigo ya kukodi kutoka Afrika Kusini.
Alisema watu hao kutoka Ulaya Mashariki na washirika wao wa hapa nchini, walikodisha ndege ili kuwaondoa tumbili hao kwenda Ulaya Mashariki. Alisema harakati za kukamata tumbili hao porini zilianza wiki iliyopita na jumla ya idadi yao ni 450 ilhali kuna taasisi zinazolinda hayo mapori bila walinzi wa mapori hayo kujua.
Maghembe alisema tumbili hao walikamatwa kutoka Upare, Hanang, Manyara na Mlima Kilimanjaro na aliwaita wasimamizi na kuwapa taarifa juu ya watu hao, wanaokamata tumbili porini.
“Nikiwa Moshi katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa nilimuita Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Wanyamapori Matumizi Endelevu, Dk Charles Mulokozi na kumuarifu juu ya kamata kamata hiyo na kumuagiza kutotoa kibali cha kusafirisha wanyama ili tuwakamate watu hao, lakini baadaye tukagundua yeye ndio amesaini kibali hicho kutoka Dar es Salaam,” alisema Maghembe.
Alisema watu hao hawakufuata taratibu, kwani hawakuwa na kibali cha kukamata wanyama hao na ofisi yake ina taarifa za kutokuwepo mtu aliyeomba kukamata.
Alimtaka Katibu Mkuu, Meja Jenerali Gaudence Milanzi kufanya uchunguzi wa kina tangu kukamatwa kwa twiga waliokuwa wakisafirishwa nje na waangalie wanaotoa vibali hivyo na wanaohusika na biashara ya wanyamapori.
Polisi yazungumza
Kwa upande wake, Polisi mkoani Kilimanjaro imesema imewakamata watu wawili raia wa Uholanzi kwa tuhuma za kusafirisha wanyamapori aina ya tumbili kupitia KIA; anaandika Arnold Swai kutoka Moshi.
Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro, Wilbroad Mutafungwa alisema watu hao walikamatwa Machi 23, saa moja jioni, wakiwa katika uwanja wa Kia tayari kuwasafirisha wanyama hao.
Kamanda Mutafungwa alisema wanyama hao walikuwa 61 ambao walikuwa kwenye masanduku sita ya mbao na walikuwa wakisafirishwa kwenda Armenia kwa kutumia Kampuni ya Arusha Fright Limited. Alisema wanyama hao walikamatwa eneo la mizigo la CAGO na walikuwa wasafirishwe kwa ndege binafsi yenye namba EW/36 4G.
Aliwataja watuhumiwa waliokamatwa ni Artem Vardanian (52) mwenye hati ya kusafiria namba NWF8CKJR8 na Edward Vardanian (46) mwenye hati ya kusafiria namba NY969P96, wote wakiwa ni raia wa Uholanzi.
Alisema watuhumiwa wanashikiliwa katika Kituo cha Polisi KIA na wanyama wamehifadhiwa na uchunguzi unaendelea kufanyika kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii.

Thursday, March 17, 2016

Magufuli apiga ‘marufuku’ mitambo ya kukodi

RAIS John Magufuli ametaka Shirika la Umeme Tanzania ( Tanesco) kuachana na miradi ya mitambo ya kukodi na kutosikia kuna mapendekezo ya kutaka kuongeza mkataba.
Amewataka watendaji wa shirika hilo kuondokana moja kwa moja na wazo la kufa kwa kuwasisitiza kwamba life mawazoni mwao huku akimhadharisha Waziri mwenye dhamana kwamba mtendaji atakayemshauri juu ya hilo, hafai, ikiwezekana amuondoe wizarani. Magufuli alisema hayo jana wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa kituo cha kufua umeme cha Kinyerezi II , jijini Dar es Salaam.
Alisema ipo mikataba mingi aliyoiita ya hovyo na kusisitiza kwamba Watanzania wamechoka na miradi ya hovyo ambayo kila siku imekuwa ikizaa matatizo. “Niwaombe Tanesco katika siku za usoni muachane na miradi ya kukodisha mitambo ya umeme na matumaini yangu sitasikia tena mnaleta mapendekezo kwamba mnataka kuongeza mkataba au tunataka kukodi,” alisema.
Akimsisitiza Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo kusimamia hilo, alisisitiza, “suala la kukodi likafe kabisa; na hayo mawazo nayo yakafe; kuwe na mawazo ya kujenga mitambo yetu.” Alisema lazima kuachana na umeme wa kukodisha usio na uhakika au wa kutumia watu. Alisema ndiyo maana kumekuwa na matatizo mengi kama ya IPTL .
Awafagilia Muhongo, Makonda Rais Magufuli ambaye ameeleza kufurahishwa na Wizara ya Nishati na Madini, aliitaka iende na kasi kubwa zaidi kwa kuachana na mitambo ya kukodi. Alisema nchi imechoka kufanyishwa biashara na wawekezaji aliowaita wa ajabu, kwa kulipia ‘capacity charge’ na bei za ajabu huku wakiumiza wananchi kwa bei juu. “Wizara endeleeni kujipanga vizuri kwa spidi ya hapa kazi tu na ndiyo maana niliamua kumrudisha Profesa Muhongo.
Na wakati mwingine vitu vizuri vinapigwa vita, hata Makonda (Paul-Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam) alikuwa anapigwa vita, nikaona mbaya wao nimrudishe hapa kwani kila nikisali naona Makonda anabaki hapa hapa,” alisema. Alisema hachagui mwanasiasa bali mchapakazi kwani maendeleo hayahitaji siasa. Alisema kila mmoja anahitaji maendeleo na ndiyo maana alichagua wachapa kazi.
Bwawa la Mtera Aidha aliwaambia Tanesco kwamba kutokana na mvua za mafuriko zilizotokea mkoani Iringa hivi karibuni, hatarajii kupewa taarifa za kupungua kwa maji kwenye bwawa la Mtera. “Kama mna mtindo la kufungulia maji na kusema maji ya Mtera hayatoshi kuzalisha umeme wakati tumeshuhudia watu wanapelekwa na maji, sitawaelewa,” alisema.
“Mkurugenzi (Felchesmi Mramba) sitakuelewa, Waziri (Muhongo) sitakuelewa na hata Katibu Mkuu (Profesa Justin Ntalikwa) sitakuelewa,”alisema Rais Magufuli. Alisema watakapoachia maji yakaondoka, wahakikishe umeme haupungui hata siku moja. Alisema ni lazima kuwaambia ukweli na kueleza kwamba anajua wamemwelewa. Alisema haiwezekani kuendelea kuwa masikini wakati wasomi wapo na wizara nzima ikiwa ina viongozi maprofesa.
Anayenikwamisha, atakwama Alisema serikali yake itafanya kazi kwani wananchi walimchagua bure bila kuwahonga kwa lengo la kuondoa kero. Alihakikishia umma wa watanzania kuwa amejipanga kufanya kazi na anayetaka kumkwamisha, atakwama yeye na kuondoka siku hiyohiyo. Aliwataka wananchi kusaidia serikali kwenda mbele kwa kufanya kazi na kuwapuuza wanaotaka kuchelewesha maendeleo.
Alisema upatikanaji wa umeme ni kipimo cha maendeleo ya nchi, hivyo bila kuwepo umeme wa uhakika ndoto ya kujenga uchumi wa viwanda haitakamilika. “Umeme ukiwepo, ndoto itakamilika na kujenga ajira kwa Watanzania,” alisema. Uzalishaji umeme Alisema uwezo wa nchi kuzalisha umeme ni megawati 1,200 hadi 1,500 kwa mwaka.
Alisema sasa uzalishaji umefikia megawati 1026 na kila Mtanzania anatumia wastani wa watt 30 kwa mwaka kiasi ambacho kiko chini licha ya kuwa na vyanzo vingi vya kuzalisha umeme. Alisema ikilinganishwa na nchi nyingine hususani Kenya, kila Mkenya anatumia watt 40, China watt 490 kwa mwaka, Afrika Kusini 500, Marekani watt 1,683.
Magufuli alisema kuweka jiwe hilo la msingi ni hatua nzuri kwani mradi utapunguza kwa kiwango kikubwa tatizo la umeme. Alisema ndiyo maana baada ya kuingia serikalini na kukusanya mapato alihakikisha analipa dola milioni 120 ambazo ni asilimia 15 ya gharama za mradi zilizotakiwa kulipwa na serikali. Alisema katika gharama zote za dola za Marekani milioni 344, serikali ya Japan inatoa asilimia 85 ya gharama hiyo lakini Tanzania ilikaa miaka miwili kupata fedha hizo.
Alisema pia mtambo wa Kinyerezi I wenye uwezo wa kuzalisha megawati 150 unaweza kuongeza na kufikia megawati 335 na mkandarasi anahitaji dola milioni 20 kuendeleza ujenzi na kuahidi kuzitafuta mwezi huu na kuanza ujenzi. Alitaka kampuni inayojenga mradi wa Kinyerezi II kumaliza mapema kama ilivyopangwa kwa ubora unaotakiwa kwa heshima ya fedha.
Akizungumzia ulipwaji fidia kwa wakazi wa Kinyerezi wanaodai Sh bilioni mbili, alisema atawapelekea fedha na kulipwa kwa mujibu wa sheria. Alitaka waliolipwa wasifanye ujanja kwa kuwa hakuna fedha za bure. Alisema mradi huo upo maeneo ya Kinyerezi ambako vijana na akinamama wanapaswa kupewa nafasi ya kupewa ajira.
Aliwataka wakipata ajira hizo wasiibe vifaa vya kazi kwani mradi ni wa Watanzania wote kwa kuwa wakiiba, itakuwa chanzo cha kuchelewesha mradi. “Ni vema kufanya kazi kwa ua minifu ili kuwanufaisha Watanzania wote kwani inatakiwa Tanzania mpya yenye maendeleo,” alisema. Aliwaeleza wakazi wa Kinyerezi kuwa katika mradi huo pia watajenga kituo cha polisi kwa ajili ya usalama wa raia.
Aliwashukuru wadau wa maendeleo kwa misaada yao na kuwathibitishia kuwa wataendelea kutoa ushirikiano na kuwahakikishia wadau wa maendeleo kuwa fedha walizotoa zitatumika kwa uangalifu bila kufuja na kupeleka panapotakiwa na kujenga nidhamu ya matumizi bora ya fedha. Umiliki Kinyerezi II Waziri Muhongo alisema mradi wa Kinyerezi II unamilikiwa na serikali kwa asilimia 100.
Serikali ya Japan imetoa Dola za Marekani milioni 292 ambao ni mkopo wa masharti nafuu na serikali imetoa dola za Marekani milioni 52 hivyo kutumia Dola milioni 344 sawa na Sh bilioni 740. Alisema tangu Rais Magufuli aingie madarakani, hali ya umeme imezidi kuimarika na kufikia megawati 1,000 ambazo hazijafikiwa ndani ya miaka mitano na kwa jana ilikuwa megawati 1,025 za mahitaji.
Alisema baada ya ujenzi wa mradi huo, utafuata wa Kinyerezi III wa megawati 600 na Kinyerezi IV megawati 330 na baadaye kuhamia mikoa mingine. Umeme wa mvuke Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Mramba alisema mtambo huo wa Kinyerzi II ni wa kwanza kutumia teknolojia ya ‘combined cycle’ ambao umeme utazalishwa kwa gesi na pia kutumia mvuke.
Mradi huo utakuwa na mitambo sita ya Hitachi-25 itakayozalisha megawati 160 kutokana na gesi na mitambo miwili ya mvuke itakayozalisha megawati 80 na kufanya uzalishaji wa megawati 240. Alisema mitambo hiyo inatengenezwa na kampuni ya Hitachi ya Japan na itafungwa na mkandarasi wa Kampuni ya Sumitono ya nchini humo ikiwa ya kisasa yenye uwezo wa kuzalisha umeme kwa zaidi ya miaka 20 ijayo

Wednesday, March 09, 2016

RAIS WA VIETNAM, MHE. TRUONG TAN SANG AKARIBISHWA IKULU, JIJINI DAR LEO


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Joseph Magufuli wa pili 
kushoto) akimkaribisha mgeni wake Rais wa Vietnam, Mhe. Truong Tan Sang Ikulu Jijini
Dar es Salaam 9 Machi,pia walikuwemo viongozi wa serikali wengine kama Waziri mkuu 
 Mhe.Kassim Majaliwa Majaliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
 
 
 
 

Raisi Magufuli Amtembelea Maalim Seif

Raisi Magufuli Amtembelea Maalim Seif katika Hoteli ya Serena kwa ajili ya kumjuilia hali yake.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF ambaye pia ni Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Shariff Hamad jijini Dar es Salaam. Maalim Seif aliruhusiwa kutoka hospitalini jana na hali yake inaendelea vizuri






Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF ambaye pia ni Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Shariff Hamad jijini Dar es Salaam. Maalim Seif amemshukuru Rais Dkt. Magufuli kwa kumjulia hali  na kusema kuwa hali yake ya kiafya inaimarika siku baada ya siku.

 










































Monday, March 07, 2016

DKT. JOHN MAGUFULI AMUAPISHA MHE. BALOZI ENG. JOHN WILLIAM KIJAZI KUWA KATIBU MKUU KIONGOZI

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Balozi Eng. John William Herbert Kijazi kuwa Katibu Mkuu Kiongozi Ikulu jijini Dar es Salaam. Balozi Kijazi anachukua nafasi ya Balozi Ombeni Sefue ambaye atapangiwa kazi nyingine.

 
 
 
 
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemuapisha Balozi Mhandisi John William Kijazi kuwa Katibu Mkuu Kiongozi.
Hafla ya kuapishwa Balozi Kijazi imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa, Wakuu wa vyombo vya Ulinzi na Usalama, Makatibu wakuu na Naibu Katibu Wakuu.

Balozi Kijazi ambaye kabla ya kuteuliwa kuwa Katibu Mkuu Kiongozi alikuwa Balozi wa Tanzania nchini India, anachukua nafasi ya Balozi Ombeni Sefue ambaye atapangiwa kazi nyingine.

Wakati huo huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John  Pombe Magufuli ameagana na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi (UNHCR) anayemaliza muda wake Bi. Joyce Mends-Cole Ikulu Jijini Dar es Salaam, ambapo pamoja na mambo mengine amemshukuru kwa kazi kubwa ya kuhudumia wakimbizi kwa kipindi chote alichokuwepo hapa nchini.

Kwa upande wake Bi. Joyce Mends-Cole amempongeza Rais Magufuli kwa kazi nzuri inayofanywa na Tanzania kuzisaidia nchi zenye matatizo, hususani migogoro ya kisiasa ambayo husababisha watu wake kuwa wakimbizi.

Pia amepongeza kuteuliwa kwa Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Mheshimiwa Benjamin William Mkapa, kusaidia usuluhishi wa mgogoro wa Burundi ambao umesababisha idadi kubwa ya wakimbizi kukimbilia Tanzania.

Hata hivyo amesema idadi ya wakimbizi wanaokimbilia Tanzania imepungua kutoka wakimbizi 3,000 waliokuwa wakiingia hapa nchini kwa wiki, wakati Mgogoro wa Burundi ulipoanza hadi kufikia wakimbizi takribani 1,000 wanaingia hapa nchini kwa wiki hivi sasa.

Aidha, Bi. Joyce Mends-Cole amewashukuru Watanzania kwa ushirikiano alioupata kwa kipindi cha miaka mitatu aliyofanya kazi hapa nchini, na ameahidi kuwa Balozi wa kuitangaza vyema Tanzania.
 
Gerson Msigwa.
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
07 Machi, 2016
 

Thursday, March 03, 2016

Google Car Stubs Toe

One of Google's self-driving cars kissed a bus on Valentine's day, marking the first accident in which the one of the company's autonomous vehicles was at least partly at fault.
Possibly too smart for its own good, the self-driving car was attempting to reenter its previous lane when it contacted a municipal bus.
The car had pulled over in preparation for a right turn, but came to a stop when it detected sandbags near a storm drain at the intersection, according to Google.
The reason the car pulled to the side before making the right hand turn is that it's what a human driver would do.
Google was testing a software update that would empower its autonomous vehicles to make such a maneuver, in order to give vehicles behind it the space and opportunity to pass an automobile that was preparing to make a turn.
The car navigated back into the roadway under the assumption that the bus, traveling in the same direction, had enough time to yield to it and would do so. However, that wasn't the case.
Traveling at under 2 mph, the Google car hit the passing bus, which was traveling at 15 mph. The California DMV estimated that the bus driver had about 3 seconds to respond to the car's reentry attempt.



The Case for Turning Over the Wheel

In the other collisions involving Google's driverless cars, only humans were at fault. This time, the car was operating in autonomous mode.
The impact of the collision may be much more severe than the damage the driverless car suffered to its front-left fender, front-left wheel and one of its sensors. The accident is a hit to the reputation of driverless vehicles.
The average consumer typically hears about driverless cars only when the vehicles have been involved in collisions, which hasn't done much for the technology's reputation, said Jack Nerad, executive market analyst for Kelley Blue Book.
"There is also the issue of control," he told TechNewsWorld.
Many people believe their driving skills are better than others' are, Nerad said. "Thus, many folks would prefer to do it themselves versus letting an unknown machine take over. We've all experienced computer crashes, but a computer crash in an autonomous car could lead to a genuine life-threatening crash."
In a driverless near future, things would have played out a little differently than the test car crash. Had both the bus and car been manned by machines, it would have made fault-finding a lot easier, suggested Charles King, principal analyst for Pund-IT.
"It also brings up issues of liability and possible punishment fit for a TV sitcom," King told TechNewsWorld. "Who made the arrest? Robocop on traffic detail? What would a jury of peers consist of? Laptops, smartphones and tablets? If the accused is Android based, would it be fair for the judge to be an iPad?"

More Than Human

The common feeling among drivers that their skills are superior to those of other drivers may play a large role in the public's attitude toward driverless vehicles.
"Safer operation is a selling point, but what is not generally reported is that autonomously driven vehicles will still be involved in collisions," Kelley's Nerad said. "Assessing fault will be an issue on those occasions, and that is just one of many issues that stand in the path of autonomous vehicle adoption."
The journey, deep into uncharted territory, has yielded new insights into the art of driving and has helped engineers emulate some of the behaviors that make human drivers so efficient -- when they aren't clogging up a city's arteries behind a traffic incident.
An exploration of those behaviors led to the right-turn procedure that the driverless car attempted when it pulled out in front of that bus. However, it's reasonable to expect that not every tactic tested will succeed without a stumble.
"Those of us who drive in urban traffic every day know that expecting a transit bus to yield even when the law says it should is expecting too much," said Nerad.
Further, "on top of the inane superiority complex in human drivers, there has been, historically, a fear of machines that 'display or achieve human-like qualities,'" King pointed out.
"The HAL computer is a classic example, but there are hundreds of others," he noted.
"A common attitude or conceit is that whatever the case, a person will always be a better, wiser and more empathetic decision maker," King said. "That applies to complex moral issues but can also relate to physical actions -- including driving."

Kampuni za simu nchini zapigwa faini ya mamilioni

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imetoza kampuni tano za simu za mkononi, faini ya Sh milioni 112.5 kutokana na kushindwa kutekeleza masharti na vigezo vya ubora wa huduma.
Ingawa haikuelezwa moja kwa moja vigezo vya ubora wa huduma walivyokiuka, TCRA imezungumzia malalamiko ya wateja ya kukatwa fedha na kampuni bila kupiga simu, na kukiri kukithiri kwa tatizo hilo. Ilisema wanatarajia kufunga mtambo utakaokuwa ukifuatilia bando katika simu za wateja, kukabili tatizo husika.
Kampuni zilizoadhibiwa kwa kukiuka Kanuni ya Ubora wa Huduma za Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta za mwaka 2011, ni Airtel Tanzania Limited, Benson Informatics Limited (Smart), MIC Tanzania Limited (Tigo), Vodacom Tanzania Limited na Zanzibar Telecom Limited (Zantel).
Akizungumza jana na waandishi wa habari, Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Dk Ally Simba alisema TCRA imebaini kampuni hizo hazitoi huduma bora. Ilibaini hilo baada ya kutathmini ubora wa huduma za mawasiliano (Sauti na data) zinazotolewa na kampuni hizo. Tathmini ililenga kupata uhalisia wanaoupata watumiaji wa huduma hizo.
“Kwa kuzingatia makampuni hayo kukubali kutotimiza vigezo vya ubora wa huduma wanazotoa na kuahidi kuboresha, Mamlaka imetoa adhabu kwa mujibu wa kanuni za ubora wa huduma kama ilivyoainishwa katika Kanuni 15 ya Kanuni ya Ubora wa Huduma,” alisema.
Alitaja kampuni na faini (kwa shilingi) wanazotakiwa kulipa ndani ya mwezi mmoja ni Airtel (Sh milioni 22.5), Benson Informatics Limited(Sh milioni 12.5), Tigo (Sh milioni 25), Vodacom (Sh milioni 27.5) na Zantel (Shmilioni 25).
“Endapo makampuni hayo yatashindwa kutoa faini hizo katika muda waliotakiwa kutoa au makosa hayo kujirudia rudia, watachukuliwa hatua kali zaidi, ikiwa ni pamoja na kufutiwa leseni,” alisema.
Dk Simba aliwasisitiza watoa huduma za simu za mikononi, kuhakikisha huduma hizo zinazingatia vigezo vilivyoainishwa kupitia Kanuni za Ubora wa Huduma na kuboresha huduma hizo katika kipindi cha miezi sita. Alisema mamlaka itaendelea kufanya uchunguzi wa ubora wa huduma za simu sehemu mbalimbali nchini, kila baada ya miezi mitatu.

Wednesday, March 02, 2016

EWURA imetangaza kushuka kwa bei ya mafuta nchini

MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetangaza kushuka kwa bei ya mafuta nchini kuanzia kesho Machi 2, 2016.
Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari ofisini kwake Dar es Salaam leo mchana, Mkurugenzi Mkuu wa  (EWURA), Felix Ngamlagosi alisema bei ya Petroli imeshuka sh. 31 kwa lita sawa na asilimia 1.70, Dizeli sh. 114 kwa lita sawa na asilimia 7.10 na mafuta ya taa kwa sh. 234 kwa lita sawa na asilimia 13.75 ikilinganishwa na mwezi uliopita.
Alisema hapa nchini kwa sasa Petroli itauzwa Sh. 1,811, Dizeli sh. 1,486 na mafuta ya taa sh. 1,465.
Alisema kupungua kwa bei hizo kwa soko la ndani  kumetokana na kuendelea kushuka kwa bei za mafuta katika soko la dunia.

Hata hivyo alisema hakutakuwa na mabadiliko yeyote ya bei ya petroli na dizeli kwa mkoa wa Tanga kwa mwezi huu na kwamba hiyo imetokana na kutopokea mafuta mapya kupitia Bandari ya mkoa huo katika kipindi cha Februari mwaka huu.
"Mamlaka inapenda kuujulisha umma kuwa bei hizi kikomo za mafuta kwa eneo husika zinapatikana vilevile kupitia upigaji wa simu ya mkononi kwa mitandao yote kwenda  namba  *152*00# na kisha kufuata maelekezo.

Aliongeza kuwa kwa mujibu wa sheria ya mafuta ya mwaka 2015, bei za bidhaa za mafuta zitaendelea kupangwa na soko hivyo Ewura itaendelea kutoa taarifa za bei kikomi lengo likiwa ni kuwasaidia wadau kufanya maamuzi stahiki kuhusu manunuzi ya bidhaa hiyo.
Aidha amevitaka vituo vyote vya mafuta nchini na kuchapisha bei za bidhaa za mafuta katika mabango yanayonekana bayana na yakionesha bei ya mafuta, punguzo, vivutio vya biashara au promosheni zinazotolewa na kituo husika.
Alisema wateja wanashauriwa kununua bidhaa za mafuta kutoka kwenye vituo vinavyouza mafuta kwa bei ndogo zaidi ili kushamirisha ushindani. Ni kosa kuuza mafuta bila kuweka mabango ya bei inayoonekana vizuri kwa wateja na adhabu itatolewa kwa kituo husika.
Alibainisha kuwa wanunuzi wanashauriwa kuhakikisha kuwa wanapata stakabadhi ya malipo inayoonesha jina la kituo, tarehe, aina ya mafuta kwa lita na kwamba stakabadhi ya malipo itatumika kama kidhibiti cha mnunuzi wa mafuta endapo kutajitokeza malalamiko ya ama kuuziwa mafuta kwa bei ya juu kuliko bei kikomo, au yenye kiwango cha ubora kisichofaa.