Thursday, February 25, 2016

Gesi yagundulika bonde la mto Ruvu

TANZANIA imedhihirisha kuwa ni tajiri mkubwa wa rasilimali ya gesi asilia baada ya kugundulika kwa gesi nyingine katika bonde la mto Ruvu yenye ukubwa wa ujazo wa futi trilioni 2.17.
Ugunduzi huo wa gesi asilia umefanywa na Kampuni ya Dodsal Hydrocarbons and Power Tanzania Limited ambayo imekuwa inafanya shughuli za utafutaji wa gesi na mafuta katika Mkoa wa Pwani.
Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo, Pilavullathil Surendran alisema jana katika mkutano wa wawekezaji wa gesi na mafuta ulioandaliwa na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo kuwa, thamani ya gesi iliyoko katika eneo hilo inafikia Dola za Marekani bilioni sita sawa na Sh trilioni 12.
Ugunduzi huo mpya unafanya hadi sasa Tanzania kuwa na amana ya gesi yenye ukubwa wa futi za ujazo trilioni 57.27.
Kwa upande wake, Profesa Muhongo alithibitisha kugundulika kwa gesi hiyo tangu Julai mwaka jana, lakini akaeleza kuwa Serikali imechelewa kutangaza ugunduzi huo kama inavyoagizwa na Sheria ya Mafuta ya Mwaka 2015 kutokana na shughuli za uchaguzi.
“Sheria mpya inatutaka kabla ya waziri mwenye dhamana ya gesi kutangaza ugunduzi mpya wa gesi na mafuta ni lazima athibitishiwe na mamlaka ya udhibiti wa bidhaa za Petroli na Gesi (PURA). “Wizara yangu itawasiliana na mwanasheria mkuu wa serikali ili kupata ushauri wa kisheria kuhusu jambo hilo na bahati nzuri tayari PURA imeshaanza kushughulikia jambo hilo na naamini kuwa nitatangaza ugunduzi huo mpya hivi karibuni,” alifafanua Profesa Muhongo.
Licha ya ugunduzi huo mpya tayari gesi imegundulika katika maeneo ya kisiwa cha Songo Songo mkoani Lindi na eneo la Mnazi Bay huko Mtwara na katika Wilaya ya Mkuranga, Pwani pia kumegundulika kiasi kikubwa cha gesi.

Tuesday, February 23, 2016

Big game today arsenal vs barca

Bartomeu has praised Luis Suarez for the impact he has had on Barcelona following his £75m move from Liverpool two seasons ago.
"We are very happy with him," said Bartomeu. "We knew he was an incredible player and he has been better than expectations."
With fellow South Americans Lionel Messi and Neymar, Suarez has formed arguably the most potent strikeforce in world football.
"Right now, we are happy because we have the best players in the world," said Bartomeu.
"Messi is with us, Neymar is an incredible player of the future, but Suarez brought the balance to them. Together, this trident is incredible.
"The fans of Barcelona have never seen players do this."
#



  • Arsenal's Arsène Wenger says Barcelona are "not far" from being perfect
  • The Spanish side are 32 matches unbeaten, winning 13 of the last 14
  • Wenger: "We must take our chances"
  • Barcelona won in England at this stage of the competition in 2014 and 2015
  • Lionel Messi has never scored past Petr Čech in six previous games
 Possible lineups
Arsenal: Čech; Bellerín, Mertesacker, Koscielny, Monreal; Ramsey, Coquelin; Walcott, Özil, Sánchez; Giroud.
Out: Arteta (unspecified), Cazorla (knee), Gabriel (hamstring), Wilshere (calf/shin), Rosický (thigh)
Misses next match if booked: Özil, Giroud, Campbell
Barcelona: Ter Stegen; Dani Alves, Piqué, Mascherano, Alba; Rakitić, Busquets, Iniesta; Messi, Suárez, Neymar.
Out: Rafinha (knee), Arda Turan (suspended)
Misses next match if booked: Piqué

 Arsène Wenger, Arsenal manager
No team is perfect, but Barcelona are not far from it. We need to take our chances. We will have less of the ball than against Hull, but we have to make the most of it.
They have top strikers. Maybe they look like they are having a little bit less possession at the moment because they used to have Xavi in midfield. They have a team that can score at any moment. Even when they are being dominated they are still very dangerous. They did that in the final last year against Juventus when it was 1-1. They were suffering but they took their chances when they arrived.
Can Lionel Messi break his Petr Čech hoodoo?
I knew Luis Enrique as a player. He scored against us at Wembley in the Champions League. He has done a remarkable job because he arrived with scepticism around him and won the treble in his first year.
I remember we played the Champions League final against Barcelona in 2006 and Messi was injured for that game. It's remarkable that was ten years ago and what he has achieved in that time.
Luis Enrique, Barcelona coach
On paper this is one of the most attractive and appealing games if you like this kind of football. Arsenal are a good team, strong in the transition and with really good players up front. They will press high at times but I hope we can keep the ball in their half and impose our own game.
Being labelled favourites means nothing. We have to prove ourselves game after game and we are going to try to. If we get a good score tomorrow that would be fantastic, but we have a lot of confidence going into the second leg whatever happens.
I am delighted to have such a good front three, and also with the squad as a whole. They are all the chosen ones because they are fantastic. I’m absolutely delighted to be their manager. I just say 'abracadabra' and the magic sparks.

 Did you know?
Barcelona have won their two previous two-legged knockout ties against Arsenal, in 2009/10 (6-3 aggregate) and 2010/11 (4-3), and also beat the Gunners 2-1 in the 2006 final at the Stade de France. Current coach Luis Enrique scored in both encounters in the 1999/2000 first group stage, finding the net in the 1-1 Camp Nou draw and again in a 4-2 win at Wembley.

Kenyatta and Nkurunziza congratulate Museveni



Kampala.
Kenyan president Uhuru Kenyatta last Saturday became the first head of state to congratulate President Museveni, upon winning Thursday’s elections which effectively extends his grip on Uganda to 35 years.
Using his Facebook and Twitter accounts, Kenyatta said: “The people of Uganda have spoken, and they have spoken very clearly. We respect their choice of president Museveni.”
“I am very pleased to congratulate President Museveni on his re-election as President of Uganda.”
“Kenya values its close friendship with Uganda. That friendship is founded on a common history, a common culture, and common interests. In years past, we have worked closely together for the prosperity and freedom of our nations.”
President Kenyatta was 24 years when President Museveni, 71, took power in 1986 after a five-year guerilla war. He was voted Kenya’s president in March 2013.
Mr Kenyatta’s congratulatory message, however, attracted loathsome comments from the citizenry of both Kenya and Uganda.
Similarly, embattled Burundian president Pierre Nkurunziza took to Twitter to post: “I wish to hereby convey my warmest congratulations for Kaguta Museveni’s well-deserved re-election. May God bless #Uganda and #Burundi.”
The Burundian leader came under fire last year after he tinkered with the constitution, and extended his rule beyond the mandatory two terms, which has plunged the impoverished country into anarchy, which, according to UN, has left scores dead and displaced over 300,000 people.
President Museveni was tapped by the East African Community (EAC) and supported by the international community to lead the mediation process between Mr Nkurunziza and the opposition.

Thursday, February 18, 2016

Matokeo ya form four 2015/2016 yametoka rasmi leo.

Baraza la mtihani (NECTA) limetangaza Matokeo ya kidato cha nne leo, ambapo  ufaulu  unaelezwa kushuka  kwa 1.85%  toka  69.75%  mwaka 2014  hadi 67.91%  mwaka  2015.
kuangalia Matokeo bonyeza hapo chini

 Angalia Matokeo hapa

Wednesday, February 17, 2016

Bodi ya Mikopo (HESLB) yatumbuliwa

WAZIRI wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako amesitisha ajira ya Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), George Nyatega kwa tuhuma za udhaifu katika fedha za mikopo zaidi ya Sh bilioni 3.2.
Pia amewasimamisha kazi wakurugenzi watatu wa Fedha na Utawala, Urejeshaji Mikopo na Upangaji na Utoaji Mikopo katika HESLB kwa tuhuma za udhaifu huo wa mikopo ya Sh 3,234,452,259.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Profesa Ndalichako alisema hatua hiyo, imechukuliwa baada ya kuridhika na kuona utendaji usioridhisha kwenye taasisi hiyo, kiasi cha kuwapo matatizo mengi yanayojirudiarudia kwa wateja wao, ikiwamo ucheleweshaji wa mikopo bila sababu ya msingi.
Profesa Ndalichako alisema pia uongozi wa bodi hiyo, umeshindwa kutoa majibu ya Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, alipoagizwa na Wizara Januari mwaka huu.
“Majibu yaliyowasilishwa na Bodi Februari 1, mwaka huu yanadai kuwa taarifa ya mkaguzi haikukidhi viwango na kwamba ilijikita katika ‘operational audit’, wakati kazi hiyo hufanywa na mkaguzi wao wa ndani. Pia walikiri baadhi ya udhaifu kama kusajili mara mbili ambao ulitokana na kuwa wakati huo walikuwa hawajaanza kutumia mfumo wa kompyuta,” alieleza Waziri wa Elimu.
Aliongeza: “Kwa mamlaka niliyopewa kwa mujibu wa Kifungu D.5(3) cha Kanuni za Kudumu kinachohusu uteuzi wa maofisa wa juu wa taasisi za serikali na Kifungu D.12 kinachoruhusu utoaji wa taarifa za Mtendaji na Kifungu F.50(1) kinachohusu usitishaji wa mkataba na kile cha Bodi ya Mikopo Kifungu cha 11(3), nimesitisha mkataba wa ajira wa George Nyatega,” alieleza Profesa Ndalichako.
Alisema kutokana na kusitisha ajira ya kiongozi huyo, Bodi inatakiwa kumlipa mshahara wa mwezi mmoja kama notisi kulingana na Kifungu 50(3)(a) cha Kanuni za Kudumu. Nyatega alikuwa astaafu Agosti 31, mwaka huu baada ya kuwa aliongezewa mkataba wa miaka miwili baada ya kustaafu Machi 2014, na kuongezewa mkataba kuanzia Septemba 2014.
Alisema pia amewasimamisha kazi Mkurugenzi wa Fedha na Utawala, Yusufu Kisare, Mkurugenzi wa Urejeshaji Mikopo Juma Chagonja na Mkurugenzi wa Upangaji na Utoaji Mikopo, Onesmo Laizer na kuwa wizara itateua maofisa watakaoshika nafasi hizo hadi uchunguzi utakapokamilika na wakurugenzi hao kuchukuliwa hatua stahiki.
“Namwagiza Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali ahakiki maelezo na nyaraka zilizowasilishwa na Bodi ya Mikopo pamoja na kufanya ukaguzi maalumu kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2013 hadi sasa ukaguzi uanze mara moja,” alieleza Profesa Ndalichako.
Akifafanua zaidi kuhusu malipo yasiyo sahihi, alisema: “baadhi ya wanafunzi ambao walikwenda kusoma Algeria wamekuwa wakiendelea kulipwa fedha wakati mkataba wao wa mkopo wa miaka minne umekwisha, lakini wamelipwa hadi miaka saba kinyume cha utaratibu.”
Alisema ukaguzi huo wa mwaka 2013, umebainisha kuwa wanafunzi 23 walipata mikopo kupitia vyuo viwili tofauti na walilipwa jumla ya Sh 153,999,590 katika chuo kimoja na Sh 147,541,460 katika chuo cha pili ambazo zimelipwa miaka mitatu mfululizo.
Waziri alisema pia wanafunzi 169 walilipwa mikopo kupitia vyuo viwili tofauti ambapo Sh 658,047,570 zililipwa katika chuo cha kwanza na Sh 665,135,716 chuo cha pili zilizolipwa kwa miaka miwili mfululizo.
Alisema pia wanafunzi 343 wasiokuwa na usajili kwenye vyuo husika walilipwa Sh 342,468,500 huku wanafunzi 55 walioacha masomo walilipwa Sh 136,232,800.
“Jumla ya Sh 159,664,500 zililipwa kwa wanafunzi 306 zaidi ya kiwango kilichobainishwa kwenye vipengele namba 4.3 na 4.3.2 cha miongozo ya upangaji na ukopaji ya mwaka 2008/2009 na 2009/2010 na vipengele no 4.6 na 4.3.1 cha miongozo ya upangaji na ukopeshaji mikopo ya mwaka 2008.2009 na 2009/2010 hadi 2010/2011."
Alifafanua kuwa pia wanafunzi 77 walipatiwa mikopo kwenye vyuo vya ndani na nje ya nchi kwa wakati mmoja.
Wanafunzi hao walitumiwa Sh 467,620,654 kwa vyuo vya nje na Sh 123,047,119 ya vyuo vya ndani huku wanafunzi 19,348 walipatiwa mikopo bila kupitishwa na Kamati ya Mikopo wakati wanafunzi 54,299 walipangiwa mikopo wakati hawakuwa wameomba.
Alisema kuwa pia Bodi ilipeleka Sh 207,052,650 kwenye vituo sita vya elimu ya juu na kutochukuliwa na wanafunzi husika na fedha hizo hazikurejeshwa Bodi kinyume cha Hati ya Makubaliano (MOU) kifungu 3.3.4(b) na (c).
“Ukaguzi utakwenda mpaka kwenye vyuo, endapo tutabaini vyuo kiwe cha umma au binafsi wamehusika kushirikiana na watendaji wa Bodi kuhujumu fedha tutachukua hatua za kisheria dhidi yao. “Nazionya taasisi zilizo chini ya wizara, sitakuwa tayari kuona wanafunzi wanakaa chini, hawana madarasa halafu kuna taasisi zinahujumu hata senti tano, tutaendelea kuzifuatilia kwa karibu,” alionya Profesa Ndalichako.
Katika hatua nyingine, Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) limekanusha taarifa zilizosambazwa jana katika mitandao ya kijamii kuwa limezuia matokeo hadi yasahihishwe upya, kuwa si za kweli na kwamba mchakato wa kutunuku uko katika hatua nzuri; kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Necta, John Nchimbi.

Uganda Prime Minister Assures Citizens of Peaceful Election

Ugandan Prime Minister Ruhakana Rugunda has assured Ugandans that Thursday’s presidential and parliamentary elections will be peaceful. He urged all registered Ugandans to turn out in droves. The prime minister’s appeal comes as fears mount that Thursday’s vote could turn violent. But Rugunda said there is no cause to alarm. “I personally encourage and the government encourages all the registered voters to turn out in big numbers to ensure that they vote for party and candidates of their choice and for parties of their own choice,” he said. The reassurances...

Wednesday, February 03, 2016

Vyama vitakavyoshiriki uchaguzi marudio Zanzibar

    VYAMA vitano vya siasa vitashiriki katika uchaguzi wa marudio wa Zanzibar, utakaofanyika Machi 20 mwaka huu, uliotangazwa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC). Vyama hivyo ni Chama Cha Mapinduzi (CCM), ADC, CCK, TLP na SAU.
Hatua hiyo inatokana na vyama vitatu vya siasa Zanzibar vya CCK, SAU na TLP, kutangaza kuwa wagombea wake, watashiriki katika uchaguzi huo wa Machi 20. Taarifa ya viongozi wa vyama vya CCK, SAU na TLP, iliyosomwa kwa pamoja katika Ukumbi wa Culture eneo la Mji Mkongwe mjini hapa jana, ilisema wagombea wa vyama hivyo vitatu, watashiriki uchaguzi huo.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka jana, ulifutwa baada ya kujitokeza kwa kasoro mbalimbali, zilizoonesha wazi kwamba hauwezi tena kuwa huru na haki. Wagombea wa vyama hivyo vya siasa, waliotangaza kushiriki katika uchaguzi huo ni Ali Khatib kutoka CCK, Issa Mohamed Zonga kutoka SAU na Hafidh Hassan Simai kutoka TLP.
Mgombea wa CCK, Ali Khatib Ali alisema kwamba tayari wamejipanga vizuri kwa ajili ya uchaguzi huo na kuwataka wanachama na wafuasi wake na wananchi, kuitumia fursa hiyo ya kidemokrasia kuchagua viongozi watakaoongoza nchi. “Tangazo la Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) limetutaka kurudia uchaguzi kwa sababu ule wa awali umefutwa kwa hivyo hatuna sababu ya kususia uchaguzi huo na tunachofanya kwa sasa ni kuwataka wanachama wetu na wafuasi kujitayarisha kwa uchaguzi wa marudio,” alisema Ali.
Jumapili iliyopita, Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein alisema chama hicho kipo tayari kwa uchaguzi wa marudio Machi 20 kwa lengo la kuhakikisha kinashika dola. Akihutubia mamia ya wanachama wao katika viwanja vya Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui wakati wa kuzindua maadhimisho ya miaka 39 ya CCM, Dk Shein alisema maamuzi ya kurudiwa kwa Uchaguzi Mkuu, yamefanywa na ZEC ambayo ndiyo chombo halali kwa mujibu wa Katiba cha kushughulikia masuala yote ya uchaguzi nchini.
Aliwataka wanachama na wafuasi wao kujipanga vizuri na kushiriki uchaguzi huo kikamilifu, kwani kwa mujibu wa Katiba ya CCM ni kushinda chaguzi zote zinazofanyika nchini ili kushika dola na kuwatumikia wananchi. “Hayo ndiyo maamuzi ya chama chetu tuliyokubaliana kushiriki Uchaguzi Mkuu wa marudio baada ya kufutwa kwa ule wa Oktoba 25 mwaka jana kwa hivyo wanachama na wafuasi jitayarisheni kushiriki kikamilifu kwa ajili ya kushika dola,” alisema Dk Shein.
Katika hatua nyingine, Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) Mkoa wa Dar es Salaam limevisihi vyama vya siasa vya Zanzibar kikiwemo Chama cha Wananchi (CUF), ambacho kimetangaza kususia uchaguzi wa marudio, kushiriki uchaguzi huo kwa maslahi ya Taifa. Aidha, limeitaka ZEC kuhakikisha inasimamia uchaguzi huo kwa haki, uadilifu na umakini mkubwa huku wakimuogopa Mungu na kutambua kuwa kama hawatatenda haki, wataulizwa katika siku za mwisho.
Hayo yalielezwa na Shehe wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Salum wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana. Alieleza kuwa Baraza hilo, haliwezi kukaa kimya kana kwamba suala la Zanzibar haliwahusu Watanzania Bara, bali linawahusu Watanzania wote kwa kuwa ni ndugu wa damu. “Sisi Bakwata Mkoa wa Dar es Salaam tunaunga mkono hatua ya ZEC kufanya uchaguzi wa marudio...vile vile tunakiomba chama cha CUF ambacho kimetangaza kususia uchaguzi huo na vyama vingine vyote, viache kususia bali vijipange kwa ajili ya kushiriki.
“Lakini pia tunawaomba ZEC kulisimamia zoezi hilo kwa haki na umakini mkubwa kwa maslahi ya taifa... pia wamuogope Mungu wakumbuke hii dunia tunapita, wasipotenda haki wataulizwa na Mwenyezi Mungu kwanini walisimamia batili,” alisema Shehe Salum. Aidha, alisema barua aliyoipokea kutoka kwa Amir wa Uamsho, Sheikh Farid Hadi Ahmad ambaye yuko gerezani, imeeleza kuwa anaunga mkono suala la kufanya uchaguzi wa marudio kwa kuwa ndiyo njia pekee ya kumaliza mgogoro huo, na kuwa hakuna njia mbadala.
Alisema katika barua hiyo, Shehe Farid aligusia mambo matatu ambapo hata hivyo mambo mengine mawili ambayo yameandikwa katika barua hiyo, hakuyataja yalizungumzia nini. Aliwataka Wazanzibari kuhakikisha wanadumisha amani na utulivu walionao na kulinda umoja na mshikamano, kwani amani itakapovurugika, haitaishia Zanzibar pekee, bali itagusa hadi Bara hivyo wanatakiwa kuwa watulivu.
Aidha, Bakwata imepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano ya Rais John Magufuli kutokana na hatua mbalimbali inazozichukua, zenye lengo la kuimarisha nidhamu, hasa kwa watumishi wa umma na serikali. Shehe Salum alisema hatua hizo, zimeanza kuleta tija kubwa kwa taifa kwani hata pato la serikali limekuwa likiongezeka mwezi hadi mwezi.
Aidha, baraza hilo limeiomba serikali kuendelea kutatua changamoto mbalimbali hasa zilizoko ndani ya Jiji la Dar es Salaam, ikiwemo kulipa umuhimu unaostahili Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART), kwani suala la foleni linachangia kuzorotesha uchumi wa Taifa kutokana na kuwa wafanyakazi wengi wanategemea usafiri wa daladala.
“Aidha, tunapongeza dhamira yake ya kubana matumizi ya serikali na badala yake kuelekeza fedha kwenye huduma za jamii na tayari tumeshaanza kunufaika na huduma hizo,” alisema. Alisema huduma hizo ni pamoja na elimu bure kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha nne, kwani linalopaswa kupongezwa kwa kuwa ada za shule na gharama za kuandikisha watoto zilikuwa ni mzigo kwa wananchi wengi.
“Ni muhimu Serikali kuwasaidia wawekezaji wa ndani kama hawa Simon Group, wamefanya kazi nzuri na kama kuna masharti magumu wamewekewa serikali ione namna ya kuwasaidia kwa kuwa wananchi wanahitaji usafiri huo wa mabasi ya mwendo kasi ili waondokane na adha ya foleni, walete ufanisi katika kazi zao.
Ndivyo wanavyofanya duniani kote wawekezaji wa ndani wanasaidiwa,” alisema Shehe wa Mkoa. Imeandikwa na Katuma Masamba, Dar na Khatib Suleiman, Zanzibar