Tuesday, December 22, 2015
Thursday, December 17, 2015
Rais Magufuli atengua uteuzi wa Dk. Hoseah
Rais Magufuli atengua uteuzi wa Dk. Hoseah
RAIS John Magufuli ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Dk Edward Hoseah. Aidha, ameamuru kusimamishwa kazi kwa watumishi waandamizi wanne wa taasisi hiyo kwa kukiuka maagizo yake.
Rais ametengua uteuzi huo wa Dk Hoseah, kutokana na kutoridhishwa na namna taasisi hiyo ilivyokuwa ikitekeleza wajibu wake katika kukabiliana na rushwa, hususan kwenye upotevu wa mapato ya serikali katika Bandari ya Dar es Salaam.
Akizungumza Ikulu, Dar es Salaam jana kwa niaba ya Rais, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue alisema kutokana na kutenguliwa kwa uteuzi huo, Rais Magufuli amemteua aliyekuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Valentino Mlowola kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru.
Balozi Sefue alibainisha kuwa Rais Magufuli amechukua hatua hiyo baada ya kujiridhisha kuwa utendaji kazi wa Takukuru chini ya Dk Hoseah, hauwezi kuendana na kasi anayoitaka.
“Eneo mojawapo la upotevu mkubwa wa mapato ya serikali ni bandarini na katika Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA, hivyo Mheshimiwa Rais amesikitishwa na kitendo cha taarifa za kuwepo kwa vitendo vya rushwa katika eneo hilo kwa muda mrefu, lakini kasi ya Takukuru kuchukua hatua haiendani na kasi anayoitaka,” alisisitiza Balozi Sefue.
Dk Hoseah alichaguliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru mwaka 2006, na hivyo amedumu katika wadhifa huo kwa takribani miaka tisa sasa. Alitanguliwa na Meja Jenerali mstaafu, Anatory Kamazima ambaye aliiongoza Takukuru kuanzia mwaka 1990 hadi 2006.
Wakurugenzi wengine waliowahi kuiongoza Takukuru ambayo awali ilikuwa ikijulikana kwa jina la Taasisi ya Kuzuia Rushwa (PCB) ni Geofrey Sawaya (1973 – 1974), S. Rutayangirwa (1974 – 1975) na Zakaria Maftah (1975 – 1990).
Kwa mujibu wa sheria, Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru huteuliwa na Rais, na anasaidiwa na Naibu Mkurugenzi Mkuu, wadhifa alionao Mlowola ambaye kabla ya uteuzi huo uliofanywa Oktoba 23, mwaka huu, alikuwa Mkurugenzi wa Intelijensia ya Makosa ya Jinai katika Jeshi la Polisi nchini.
Katika hatua nyingine, Rais Magufuli ameagiza kusimamishwa kazi mara moja kwa watumishi waandamizi wanne wa Takukuru waliosafiri nje ya nchi, licha ya Rais kupiga marufuku safari za nje kwa watumishi wa umma.
Watumishi hao ni Mkurugenzi Elimu kwa Umma, Mary Mosha, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Ekwabi Mujungu, Mkurugenzi wa Uhusiano, Doreen Kapwani na Katibu Muhtasi wa Mkurugenzi Mkuu, Rukia Nikitas ambao walisafiri nje ya nchi licha ya kunyimwa kibali cha safari kutoka kwa Rais ama Katibu Mkuu Kiongozi.
Kutokana na hatua hiyo ya Rais Magufuli, Balozi Sefue amewataka watumishi wengine wa umma, kutii agizo la Rais na kuonya kuwa atakayekiuka atachukuliwa hatua kali. Katika moja ya hatua za kubana matumizi ya serikali, Rais Magufuli alitangaza kufuta safari zote za nje kwa watumishi wa umma, isipokuwa kwa vibali maalumu.
Monday, December 14, 2015
Thursday, December 10, 2015
Rais Magufuli atangaza baraza la Mawaziri
Rais Magufuli Atangaza baraza la Mawaziri
Mawaziri Hao ni
Waziri- Augustino Mahiga, Naibu Waziri - Dk. Suzan Kolimba
Waziri-Nape Nnauye
Waziri -Sospeter Muhongo na Naibu Waziri-Medard Kalemani
Waziri -Jenista Mhagama
mawaziri wawili - Simbachawene na Kairuki
Waziri - January Makamba Naibu waziri Luhaga Mpina.
Waziri ni Charles Kitwanga
Waziri wake ni Wiliam Lukuvi Naibu Angelina Mabula.
Waziri - Husein Mwinyi
Waziri - Harrison Mwakyembe
Waziri - January Makamba
Waziri- Mwigulu Nchemba Naibu Waziri- William Tate Ole Nashon
Waziri - Charles Mwijage
Waziri - Ummy Mwalimu - Naibu - Dk Hamis kigwangalla
Waziri - bado hajapatikana - Naibu Waziri -Stela manyanya
Waziri - bado hajapatikana na Naibu Waziri - Injinia Ramo Makani
Waziri - bado hajapatikana, Naibu Waziri - Dk. Ashantu Kijachi
Waziri - bado hajapatikana, Naibu Waziri -Edwin Ngonyani
Wednesday, December 02, 2015
Serikali yachunguza ufisadi wa dola mil 6
SERIKALI inachunguza ufisadi wa Dola za Marekani milioni sita, ambazo
Benki ya Stanbic Tanzania pamoja na Kampuni ya Egma ya nchini,
iliongeza katika malipo ya ada ya mkopo, ambao Serikali iliomba kwa
Benki ya Standard ya Uingereza mwaka 2013.
Imesema inafanya uchunguzi wa ndani ili kubaini fedha hizo za kigeni zilizoingizwa kwenye akaunti ya Egma, zimekwenda wapi na kama zilitumika kuhonga, zimemhonga nani. Akizungumza na waandishi wa habari jana Ikulu Dar es Salaam, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue alisema hatua hiyo imekuja baada ya Taasisi ya Uchunguzi wa Makosa Makubwa ya Ufisadi ya Uingereza (SFO) kushinda kesi katika Mahakama ya Southwark Crown ya Uingereza dhidi ya Stanbic Tanzania inayomilikiwa na Standard Group.
“Sasa baada ya Taasisi ya SFO kushinda kesi, Tanzania tunarudi kufanya uchunguzi wa ndani kubaini hizo fedha dola milioni sita zilizoingizwa kwenye akaunti ya kampuni ya Egma na kutolewa zote muda mfupi zimekwenda wapi, na kama zilitumika kumhonga mtu, ni nani,” alifafanua Balozi Sefue.
Balozi Sefue aliwataja wamiliki wa Egma kuwa ni aliyekuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato (TRA), Harry Kitilya, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Soko la Mitaji Tanzania, Fratern Mboya na Mkurugenzi Gasper Njuu.
Alitoa mwito kwa wamiliki hao, kutoa ushirikiano wakati wa uchunguzi wa sakata hilo na kwamba mara baada ya uchunguzi kukamilika, iwapo kutabainika makosa ya rushwa au mengine, sheria itachukua mkondo wake.
“Ombi letu na ombi la Rais John Magufuli watu hawa wanatakiwa kutoa ushirikiano na pengine ameongezeka mmiliki kwenye kampuni hiyo, wahakikishe wanatoa ushirikiano,” alisisitiza Balozi Sefue. Akizungumzia sakata hilo, Balozi Sefue alisema sio jambo geni kama ambavyo baadhi ya vyombo vya habari nchini vimeripoti jana, na kwamba tangu mwaka 2013, Tanzania inalifahamu na ndiyo iliyolipeleka SFO kuchunguzwa.
Akifafanua, alisema katika mwaka 2012/13, serikali ilifanya utaratibu wa kawaida unaofanywa na nchi mbalimbali duniani wa kukopa kwenye taasisi za benki ambapo Benki ya Standard ilikubali kuikopesha.
Alisema katika mkopo huo, serikali ilihitaji Dola za Marekani milioni 600 kwa ajili ya kuendeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ambapo kwa kawaida benki husika huingia mkataba na benki nyingine inayopewa jukumu la kutoa mkopo huo.
Alisema katika mchakato huo, Benki ya Standard kupitia kampuni tanzu iliipa Benki ya Stanbic Tanzania kazi hiyo ambapo fedha hizo zilipatikana na kwamba katika mchakato wa mkopo huo, ada ya mkopo serikali ilitozwa asilimia 2.4 ya mkopo.
Aliyataja masharti mengine kwamba yalikuwa ni kulipa mkopo riba kwa miaka saba, na kwamba deni hilo litalipwa kwa miaka saba, ambapo linapaswa kumalizika mwaka 2019. Balozi Sefue alifafanua kwamba baada ya mkopo kutolewa nusu ya kwanza, Mtendaji Mkuu wa benki hiyo wakati huo, Bashir Awale alikuwa na matatizo na watumishi, na Benki Kuu (BoT) iliingilia kati na kufanya uchunguzi.
Katika uchunguzi huo, kulibainika kasoro nyingi zikiwemo ulipaji wa fedha kwenye kampuni bila maelezo ikiwemo Kampuni ya Egma ambayo ilibainika kulipwa Dola za Marekani milioni sita.
Alisema fedha hizo zilionekana zimeingizwa kwenye Egma na kutolewa zote bila kutozwa kodi, ambapo katika taarifa yao ya ukaguzi, BoT ililionesha hilo na mambo mengine yaliyobaini na kumkabidhi Mwenyekiti wa Benki ya Stanbic Tanzania.
Hata hivyo, baada ya taarifa hiyo kupokewa, mwenyekiti wa benki hiyo aliitisha mkutano wa Bodi ya benki na waliipitia taarifa hiyo ya BoT na taarifa kupeleka Kitengo ya Uchunguzi cha Kimataifa cha Intelijensia.
Alisema katika uchunguzi huo, ndipo ilibainika kwamba nchi ilitozwa ada zaidi, ambapo ada ya mkopo halali ilikuwa Dola za Marekani milioni 1.4, lakini Stanbic walichukua Dola za Marekani milioni 2.4.
Alisema fedha hizo zilizoamriwa na Mahakama nchini Uingereza kwamba Benki ya Standard iilipe Tanzania ni zile ambazo hazikupaswa kuchukuliwa, ambazo ni dola milioni sita na dola milioni moja ni faida.
Imesema inafanya uchunguzi wa ndani ili kubaini fedha hizo za kigeni zilizoingizwa kwenye akaunti ya Egma, zimekwenda wapi na kama zilitumika kuhonga, zimemhonga nani. Akizungumza na waandishi wa habari jana Ikulu Dar es Salaam, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue alisema hatua hiyo imekuja baada ya Taasisi ya Uchunguzi wa Makosa Makubwa ya Ufisadi ya Uingereza (SFO) kushinda kesi katika Mahakama ya Southwark Crown ya Uingereza dhidi ya Stanbic Tanzania inayomilikiwa na Standard Group.
“Sasa baada ya Taasisi ya SFO kushinda kesi, Tanzania tunarudi kufanya uchunguzi wa ndani kubaini hizo fedha dola milioni sita zilizoingizwa kwenye akaunti ya kampuni ya Egma na kutolewa zote muda mfupi zimekwenda wapi, na kama zilitumika kumhonga mtu, ni nani,” alifafanua Balozi Sefue.
Balozi Sefue aliwataja wamiliki wa Egma kuwa ni aliyekuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato (TRA), Harry Kitilya, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Soko la Mitaji Tanzania, Fratern Mboya na Mkurugenzi Gasper Njuu.
Alitoa mwito kwa wamiliki hao, kutoa ushirikiano wakati wa uchunguzi wa sakata hilo na kwamba mara baada ya uchunguzi kukamilika, iwapo kutabainika makosa ya rushwa au mengine, sheria itachukua mkondo wake.
“Ombi letu na ombi la Rais John Magufuli watu hawa wanatakiwa kutoa ushirikiano na pengine ameongezeka mmiliki kwenye kampuni hiyo, wahakikishe wanatoa ushirikiano,” alisisitiza Balozi Sefue. Akizungumzia sakata hilo, Balozi Sefue alisema sio jambo geni kama ambavyo baadhi ya vyombo vya habari nchini vimeripoti jana, na kwamba tangu mwaka 2013, Tanzania inalifahamu na ndiyo iliyolipeleka SFO kuchunguzwa.
Akifafanua, alisema katika mwaka 2012/13, serikali ilifanya utaratibu wa kawaida unaofanywa na nchi mbalimbali duniani wa kukopa kwenye taasisi za benki ambapo Benki ya Standard ilikubali kuikopesha.
Alisema katika mkopo huo, serikali ilihitaji Dola za Marekani milioni 600 kwa ajili ya kuendeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ambapo kwa kawaida benki husika huingia mkataba na benki nyingine inayopewa jukumu la kutoa mkopo huo.
Alisema katika mchakato huo, Benki ya Standard kupitia kampuni tanzu iliipa Benki ya Stanbic Tanzania kazi hiyo ambapo fedha hizo zilipatikana na kwamba katika mchakato wa mkopo huo, ada ya mkopo serikali ilitozwa asilimia 2.4 ya mkopo.
Aliyataja masharti mengine kwamba yalikuwa ni kulipa mkopo riba kwa miaka saba, na kwamba deni hilo litalipwa kwa miaka saba, ambapo linapaswa kumalizika mwaka 2019. Balozi Sefue alifafanua kwamba baada ya mkopo kutolewa nusu ya kwanza, Mtendaji Mkuu wa benki hiyo wakati huo, Bashir Awale alikuwa na matatizo na watumishi, na Benki Kuu (BoT) iliingilia kati na kufanya uchunguzi.
Katika uchunguzi huo, kulibainika kasoro nyingi zikiwemo ulipaji wa fedha kwenye kampuni bila maelezo ikiwemo Kampuni ya Egma ambayo ilibainika kulipwa Dola za Marekani milioni sita.
Alisema fedha hizo zilionekana zimeingizwa kwenye Egma na kutolewa zote bila kutozwa kodi, ambapo katika taarifa yao ya ukaguzi, BoT ililionesha hilo na mambo mengine yaliyobaini na kumkabidhi Mwenyekiti wa Benki ya Stanbic Tanzania.
Hata hivyo, baada ya taarifa hiyo kupokewa, mwenyekiti wa benki hiyo aliitisha mkutano wa Bodi ya benki na waliipitia taarifa hiyo ya BoT na taarifa kupeleka Kitengo ya Uchunguzi cha Kimataifa cha Intelijensia.
Alisema katika uchunguzi huo, ndipo ilibainika kwamba nchi ilitozwa ada zaidi, ambapo ada ya mkopo halali ilikuwa Dola za Marekani milioni 1.4, lakini Stanbic walichukua Dola za Marekani milioni 2.4.
Alisema fedha hizo zilizoamriwa na Mahakama nchini Uingereza kwamba Benki ya Standard iilipe Tanzania ni zile ambazo hazikupaswa kuchukuliwa, ambazo ni dola milioni sita na dola milioni moja ni faida.
Subscribe to:
Comments (Atom)



