Wednesday, November 18, 2015

MAtokeo ya Michezo ya raundi ya pili ya kusaka tiketi ya kushiriki Kombe la Dunia

Matokeo ya Michezo ya raundi ya pili ya kusaka tiketi ya kushiriki Kombe la Dunia

Matokeo  ya mechi zilizochezwa Jumanne ni kama ifuatavyo:
Cameroon 0-0 Niger (Jumla 3-0)
Congo 2-1 Ethiopia (Jumla 6-4)
Nigeria 2-0 Swaziland (Jumla 2-0)
Ghana 2-0 Comoro (Jumla 2-0)
Misri 4-0 Chad (Jumla 4-1)
Ivory Coast 3-0 Liberia (Jumla 4-0)
Tunisia 2-1 Mauritania (Jumla 4-2)
Afrika Kusini 1-0 Angola (Jumla 4-1)
Burkina Faso 2-0 Benin (Jumla 3-2)
Senegal 3-0 Madagascar (Jumla 5-2)
Mali 2-0 Botswana (Jumla 3-2)
Tanzania 0-7 Algeria(jumla 2-9)
Kenya 0-2 Cape Verde(jumla 1-2)

DOWNLOAD INTRODUCTION TO COMPUTER

DOWNLOAD INTRODUCTION TO COMPUTER



Introduction to computer


Saturday, November 07, 2015

Taarifa..


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt John Pombe Magufuli leo
asubuhi katika Ikulu ya Dar es Salaam
amefanya kikao na Makatibu wakuu,
Manaibu Makatibu wakuu, Gavana wa
Benki Kuu Prof. Benno Ndulu na Kamishna
Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania
(TRA) ili kutoa uelekeo wa Serikali
anayoitaka mara baada ya kuapishwa.
“Nataka Serikali iendelee kwa nguvu zote
na katika kutekeleza dhana ya ‘HAPA KAZI
TU’ na viongozi kuzingatia na kukumbuka
ahadi nilizotoa ili zianze kuonekana na
kufanyiwa kazi mara moja” Rais Magufuli
amesema.
Katika Kikao chake, Rais ametoa
mwongozo na kusisitizia kuwa ni lazima
kila mtendaji Serikalini kuuzingatia,
kufuata sheria na taratibu ili taifa lisonge
mbele kwa ufanisi zaidi.
Katika kikao hicho Rais ameelekeza
mambo kadhaa ambayo watendaji hao
wanapaswa kuyasimamia, kuyawekea
mikakati na kuyapanga vizuri ili atakapo
teua Baraza lake la Mawaziri mambo hayo
yawe tayari ili Mawaziri watakaoteuliwa
waweze kuyasimamia bila kukosa.
Mambo hayo muhimu ni kama ifuatavyo:
Kuanzia mwezi Januari mwaka 2016,
wanafunzi wote wanaoanza shule
watasoma bure bila kulipa ada, Katika
jambo hili, Rais amewataka watendaji
kuanza kuliwekea mikakati tayari kwa
utekelezaji
Suala la mikopo ya wanafunzi nalo
lifanyiwe kazi na mipango yake ikamilike
kwa ajili ya utekelezaji mzuri zaidi
Amefuta safari zote za nje ya nchi kuanzia
leo hadi hapo atakapolitolea suala hilo
maamuzi mengine na kueleza kuwa
shughuli zote zinazotakiwa kufanywa nje
ya nchi zifanywe na kusimamiwa na
mabalozi wa Tanzania wanaowakilisha nchi
huko nje.
Pengine patokee jambo la dharura sana
na hata hilo lazima kibali kitolewe na Rais
au Katibu Mkuu Kiongozi. Badala yake
Rais amewataka watendaji hao kufanya
zaidi ziara za kwenda vijijini ili kuzijua na
kutatua kero za wananchi wa Tanzania.
Katika Kikao hicho, Rais amemtaka
Kamishna wa TRA, Ndugu Rished Bade
kusimamia kwa makini zoezi la ukusanyaji
wa mapato nchini na kuhakikisha kero
ndogo ndogo kwa wananchi lianze
kutekelezwa kama alivyo ahidi kwa
kufanyiwa kazi mapema zaidi.
Rais ameitaka TRA kukusanya mapato
hayo kutoka kwa wafanya biashara
wakubwa zaidi na wale wanaokwepa kodi
bila kuogopa mtu wala taasisi yoyote hapa
Tanzania na kusisitiza kuwa katika Serikali
hii wa kutoa maamuzi vinginevyo zaidi ya
haya ni yeye Rais ama Makamu wake.
Rais Magufuli pia ameagiza usimamizi
katika suala la manunuzi ambalo limekuwa
likitumika vibaya na kuwa mwanya wa
kuibia Serikali kwa watu kuongeza bei ya
vitu hata kama ni vya bei ndogo kabisa
katika jamii.
“Ikitokea suala hilo likagundulika kwa
watu kuongeza bei ya vitu, watendaji
watawajibishwa mara moja”. Rais
amesema, na kuwataka watendaji hao
kufanya kazi zao kwa kuzingatia Sheria na
taratibu zilizopo na kuzingatia maadili
mema ya kazi.
………………………MWISHO……………………
Imetolewa na Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais, Msaidizi
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
7 Novemba, 2015 

Friday, November 06, 2015

Dkt.Magufuri aapisha rasmi jana

MHESHIMIWA Dkt John Pombe Joseph Magufuli ameapishwa kuwa Rais wa Serikali ya Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.

Sherehe ya kuapishwa kwake imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa ndani na nje ya Tanzania. Sambamba na kuapishwa Rais Magufuli, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhus Hassan pia ameapishwa.

Wednesday, November 04, 2015

Warais watakaokuja kwenye sherehe ya kuapisha JPM

MARAIS wanane wa Afrika ni miongoni mwa viongozi mbalimbali kutoka nje ya nchi, watakaohudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Awamu ya Tano wa Tanzania, Dk John Pombe Magufuli.
Rais Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Magufuli ataapishwa rasmi kuwa Rais wa Awamu ya Tano kesho kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam. Dk Magufuli (56) alitangazwa mshindi wa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka huu, baada ya kupata kura 8,882,935, sawa na asilimia 58.46 ya kura halali zilizopigwa, hivyo kumrithi Rais Jakaya Kikwete katika Ikulu ya Magogoni, ambayo tayari imeshakaliwa na marais wengine wanne.
Kwa mujibu wa taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa iliyotolewa jana Dar es Salaam, sherehe za uapisho zitahudhuriwa na Wakuu wa Nchi na Serikali kutoka mataifa mbalimbali, Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa na Kikanda na Wawakilishi mbalimbali kutoka nje ya nchi. Iliwataja miongoni mwa marais watakaohudhuria sherehe hizo ni Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe, Rais Yoweri Museveni wa Uganda, Rais Paul Kagame wa Rwanda na Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini.
Wengine ni Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya, Rais Filipe Nyusi wa Msumbiji na Rais Edgar Lungu wa Zambia. Taarifa ya Mambo ya Nje ilieleza kuwa Malawi itawakilishwa na Makamu wa Rais, Saulos Chilima wakati Namibia itawakilishwa na Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje, Netumbo Nandi-Ndaitwah. Aidha, Serikali ya China itawakilishwa na Makamu Mwenyekiti wa Chama Tawala.
“Vilevile nchi nyingine ambazo zimethibitisha kushiriki na zitawakilishwa na kati ya Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Spika au Balozi ni pamoja na Burundi, Comoro, Angola, Botswana, Lesotho, Madagascar na Mauritius. “Nyingine ni Norway, Oman, Sudan Kusini, Sweden, Umoja wa Falme za Kiarabu, Marekani, Uingereza, Shelisheli, Swaziland, Algeria, Misri, Benin, Denmark, Ethiopia, Finland, Ufaransa, Ghana, India, Japan, Kuwait, Uholanzi na Nigeria,” ilifafanua taarifa hiyo.
Ilieleza kuwa Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa na Kikanda, waliothibitisha kushiriki au kutuma wawakilishi wao ni Umoja wa Mataifa (UN), Umoja wa Afrika (AU), Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), Umoja wa Ulaya (EU) na Jumuiya ya Ukanda wa Nchi za Maziwa Makuu (ICGLR).
Wabunge wapya kuwasili Dar Katika hatua nyingine, wabunge wapya waliochaguliwa katika Uchaguzi Mkuu wanatarajiwa kuwasili Dar es Salaam leo kwa ajili ya kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais Mteule, Dk John Magufuli zitakazofanyika kesho.
Akizungumzia kuwasili kwa wabunge hao, Ofisa Habari Mwandamizi wa Bunge, Prosper Minja alisema wabunge hao wanatarajiwa kuwasili leo Dar es Salaam wakiwa na vyeti vyao vya kuteuliwa kuwa wabunge vinavyotolewa na Msimamizi wa Uchaguzi wa eneo husika.
“Tunategemea kesho (leo), wabunge wapya watawasili kwa ajili ya kuhudhuria sherehe ya kuapishwa kwa rais mteule na tunategemea waje na cheti hicho pamoja na kitambulisho kingine kinachomtambulisha,” alisema Minja.
Alisema mara baada ya wabunge hao kuwasili, wanatakiwa kwenda Ukumbi wa Karimjee kwa ajili ya kutambuliwa na kupewa kitambulisho cha siku ya sherehe za kuapishwa kwa Rais Mteule, Dk Magufuli.
Tamko la Jeshi la Polisi Wakati huo huo, Jeshi la Polisi nchini limejipanga kuhakikisha usalama na ulinzi unaimarishwa wakati wa kuelekea sherehe za kumwapisha Rais Mteule, Dk John Magufuli.
Akizungumza jana Dar es Salaam, Kamishna wa Oparesheni na Mafunzo, Makao Mkauu ya Polisi, Paul Chagonja alisema jeshi lake kwa kushirikiana na vyombo vingine vya usalama, litahakikisha kunakuwa na usalama wa raia na mali zao katika kuelekea sherehe za kumuapisha Rais Mteule.
“Niwaombe wananchi kutupa ushirikiano kwa kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi pindi waonapo vishawishi ama vitendo vyovyote vya uvunjifu wa sheria,” alisema Kamishna Chagonja. Aidha, Chagonja aliwataka wananchi kuendelea kuheshimu sheria za nchi na kujiepusha na vitendo vinavyoweza kuhatarisha usalama wa raia na mali zao.
“Jeshi la Polisi linawataka wananchi kote nchini kuendelea kuheshimu sheria za nchi na kujiepusha na vitendo vya aina yoyote ile ambavyo vinaweza kuhatarisha usalama wa raia na mali ikiwemo maandamano yanayopangwa bila kufuata taratibu,” alisema Chagonja na kuongeza: “Jeshi la Polisi halitasita kuchukua hatua kali kwa mtu au kikundi chochote kitakachoonesha viashiria vya uvunjifu wa sheria ama kutaka kuvuruga amani ya nchi yetu.”
Mbali ya kuwashukuru wananchi na wadau waliotoa ushirikiano kuhakikisha amani ya Watanzania inadumu katika kipindi cha uchaguzi na wakati huu wa kuelekea kuapishwa kwa Rais Mteule, alikiri jeshi hilo kuwashikilia watu kadhaa na baadhi yao kufikishwa mahakamani kutokana na kufanya makosa wakati wa uchaguzi.
Bila kutaja idadi, Chagonja alisema, “Ni kweli kuna watu kadhaa tumewakamata kwa makosa mbalimbali wakati wa uchaguzi, kuna wengine wamefikishwa mahakamani, na kuna wengine bado wanashikiliwa kwa mahojiano zaidi na wengine wamewekewa dhamana.” Imeandikwa na Ikunda Eric na Anastazia Anyimike.