Friday, March 13, 2015

The list of the Top 10 greatest Hollywood Actors


The list of the Top 10 greatest Hollywood Actors in 2015 famous all over world are as follows:

1. GEORGE CLOONEY :
This Hollywood actor was a super star who managed to win many hearts within a shorter time. He is now ranking among the biggest actors of the film industry and has an appealing as well as cool looking appearance. As history says about him, George Clooney was a television actor in the past times and then became a film star. He has also received many golden awards and therefore successfully turned to be a super star even in the recent time. This genius actor was a nominee of various other actors as well.
  



2. JUDE LAW :
The Hollywood superstar JUDE LAW was also famous by the name of DAVID JUDE HEYWORTH LAW and was born in the year of 1972 in the month of December. He ranks among the successful actor who proved that he was not only a successful actor, but also an eminent producer along with a superb ability to direct the films. The initial entry that he made in the industry was through the theatre during the year of 1987 and therefore has received the various appreciations from his diehard fans.






3. ROBERT PATTINSON :
This Hollywood actor ROBERT PATTINSON is Hollywood’s best find and is also a well capturing hero of the Hollywood with superb personality. He reigns over and therefore dominates millions of hearts. The lists of his fans include mostly female fans that too all around the globe. This success in his carrier is highly influential which has made him a wonderful hero of the era. He is one such Hollywood actor who knows the art well about how to give life to a movie and reach the hearts of millions of audiences with his creative acting skill.






4. TOM HANKS :
 Tom Hanks is not only a superb actor of the present era but also an amazing adorable director of the age. He is well known for his friendly personality throughout his circles. He was endowed with a bunch of awards.










5. MARK WAHLBERG :
MARK WAHLBERG was a friendly hero who was basically into a music world. He managed to give us a lot of movies as well as sung beautiful songs with super hit movies as well.










6. LEONARDO DICAPRIO :
America has given birth to a talented actor who is a mature as well as cool looking actor. He started his carrier with the movie Titanic. At the age of 40 also he is yet handsome and extremely youthful.
7. JONNY DEPP :
 JONNY DEPP is that name which has created a charm over the crazy fans. He is extremely talented actor of his era and among the highest paid Heroes entertaining with amazing movies.
8. WILL SMITH : He entered into the career initially with television shows and now is ranking among the best actors and highest paid too.
9. TOM CRUISE :
 This cool looking hero of the era is widely known for his creamy personality which has impressed many eyes and satisfied hearts of millions of audience. This Hollywood actor can change the fate of any movie in which he casts.
10. BRATT PITT :
He is a fantastic Hollywood actor who has presented the world with many catchy movies which earned a lot of success. He is presently an award-winning producer of the age.
Hollywood actors have come down in this industry with the motive to produce greatest movies which remains as an icon for all. The above listed stars know well about how to capture the heart of audiences.

Tuesday, March 03, 2015

Rais Kikwete aongoza kumuaga Marehemu Komba Karimjee



RAIS Jakaya Kikwete jana ameongoza mamia ya wakazi wa Dar es Salaam waliojitokeza kuaga mwili wa Mbunge wa Mbinga Magharibi, Kapteni John Komba aliyefariki Jumamosi jioni katika Hospitali ya TMJ ikielezwa kuwa kaondoka kama moto wa kiberiti.
Tukio hilo lilifanyika jana Dar es Salaam katika viwanja vya Karimjee, na kuwakutanisha viongozi mbalimbali wa serikali wakiwemo Makamu wa Rais, Marais wastaafu akiwemo Benjamin Mkapa na Ali Hassan Mwinyi, mawaziri mbalimbali, manaibu mawaziri, viongozi wa vyama vya upinzani, mwanasheria mkuu, viongozi wa dini na wabunge.
Katika tukio hilo lililojaa simanzi na vilio vilitawala, huku baadhi ya nyimbo alizokuwa ameziimba marehemu, Kapteni Komba zikiimbwa na baadhi ya wasanii wakati wa kuaga.
Akizungumza katika tukio hilo, Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii, Said Mtanda alisema msiba wa Kapteni Komba ni pigo lisilozibika kamwe na siku alipofariki alimpigia simu wakazungumza kwa saa nne kuhusu safari ya kamati hiyo kuelekea nchini Ethiopia kikazi.
Tulipanga mambo mengi yakiwemo namna tutakavyotekeleza majukumu na jinsi ya kwenda Ethiopia… wajumbe wa kamati ilikuwa waondoke Machi mosi…lakini saa kumi jioni nikapokea ujumbe kuwa Komba amefariki,” alisema Mtanda na kuongeza kuwa alikuwa amali na rasilimali kwa familia, Chama Cha Mapinduzi na hata kwa wananchi wake jimboni.
Alisema Kapteni Komba alisimamia haki za wazee na kwamba Kamati itaendelea kusimamia yote yaliyoasisiwa na Mbunge huyo wa Mbinga ambaye pia alikuwa Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo.
Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Abdulrahman Kinana alisema Kapteni Komba alikuwa muimarishaji na mkuzaji wa CCM katika maeneo mbalimbali kwa kupitia nyimbo zake.
Wakati wa msiba wa Nyerere atakumbukwa kwa ujasiri wake na msimamo wake kwani alitunga nyimbo nyingi zenye kuwaliwaza Watanzania,”alisema Kinana na kuongeza kuwa vishindo pamoja na sauti yake vimezimika.
Alisema kifo chake kimeleta pengo kubwa kwa CCM, wasanii huku daima akikumbukwa kwani wakati wa uhai wake aligusa maisha ya walio wengi akiwa mwanajeshi, mwalimu, msanii na hata mwanasiasa.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Uratibu na Bunge, Jenista Mhagama alisema serikali itaendelea kutekeleza mipango ya Maendeleo iliyokuwa ikitekelezwa katika jimbo la Mbinga Magharibi kama ilivyokuwa imepangwa katika jimbo hilo.
Alisema Komba atakumbukwa kwa ucheshi, msimamo katika masuala mbalimbali pia mchango wake kupitia vipaji alivyokuwa navyo.
Spika wa Bunge, Anne Makinda alisema kifo cha Komba kaondoka na moto wa kiberiti, akiondoka na talanta zake, jambo linalosababisha wengi kutokuamini ambapo Mungu haachi kutoa mafundisho.
Alisema Kapteni Komba ilikuwa aende nchini Ethiopia na wenzake na kabla ya mauti kumkuta alikuwa akiandika nyimbo.
Kifo kitampata kila yeyote…angejua na kupewa hata muda kidogo angesema wale wote waliomkosea anaomba wamsamehe…na pia sisi tunapaswa kumsamehe,” alisema Makinda na kuongeza kuwa wakati mwingine watu hutumia midomo isivyo na ikumbukwe kuwa kila mmoja anatoka kwa Mungu.
Alisema Kapteni Komba alitekeleza wajibu wake kama binadamu na amekwenda kupeleka hesabu yake ya aliyoyafanya duniani huku CCM ikiamini kuwa Mungu atawapa Mbunge mwingine katika jimbo hilo.
Kiongozi wa Upinzani Bungeni, aliyewakilishwa na Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari alisema pamoja na itikadi zao bungeni lakini umoja wao ni nguzo kuu.
Alisema kifo ni safari ya kila mmoja, na kila binadamu anapaswa kutambua kuwa maisha ni mafupi na kujifunza kutenda mema kuanzia ngazi ya familia na hata kwa taifa.
Mweyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku alisema Kapteni Komba alikuwa na utendaji ulio bora alifanya hivyo bungeni akiwa na uwezo wa kusimanga viongozi bila kuwaudhi.
Alisema alikuwa mkweli akistahili kukumbukwa kwa uongozi alioutoa kupitia kipaji chake cha kuimba na baadaye katika Bunge na zaidi katika kusaidia CCM.