Tuesday, December 22, 2015
Thursday, December 17, 2015
Rais Magufuli atengua uteuzi wa Dk. Hoseah
Rais Magufuli atengua uteuzi wa Dk. Hoseah
RAIS John Magufuli ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Dk Edward Hoseah. Aidha, ameamuru kusimamishwa kazi kwa watumishi waandamizi wanne wa taasisi hiyo kwa kukiuka maagizo yake.
Rais ametengua uteuzi huo wa Dk Hoseah, kutokana na kutoridhishwa na namna taasisi hiyo ilivyokuwa ikitekeleza wajibu wake katika kukabiliana na rushwa, hususan kwenye upotevu wa mapato ya serikali katika Bandari ya Dar es Salaam.
Akizungumza Ikulu, Dar es Salaam jana kwa niaba ya Rais, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue alisema kutokana na kutenguliwa kwa uteuzi huo, Rais Magufuli amemteua aliyekuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Valentino Mlowola kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru.
Balozi Sefue alibainisha kuwa Rais Magufuli amechukua hatua hiyo baada ya kujiridhisha kuwa utendaji kazi wa Takukuru chini ya Dk Hoseah, hauwezi kuendana na kasi anayoitaka.
“Eneo mojawapo la upotevu mkubwa wa mapato ya serikali ni bandarini na katika Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA, hivyo Mheshimiwa Rais amesikitishwa na kitendo cha taarifa za kuwepo kwa vitendo vya rushwa katika eneo hilo kwa muda mrefu, lakini kasi ya Takukuru kuchukua hatua haiendani na kasi anayoitaka,” alisisitiza Balozi Sefue.
Dk Hoseah alichaguliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru mwaka 2006, na hivyo amedumu katika wadhifa huo kwa takribani miaka tisa sasa. Alitanguliwa na Meja Jenerali mstaafu, Anatory Kamazima ambaye aliiongoza Takukuru kuanzia mwaka 1990 hadi 2006.
Wakurugenzi wengine waliowahi kuiongoza Takukuru ambayo awali ilikuwa ikijulikana kwa jina la Taasisi ya Kuzuia Rushwa (PCB) ni Geofrey Sawaya (1973 – 1974), S. Rutayangirwa (1974 – 1975) na Zakaria Maftah (1975 – 1990).
Kwa mujibu wa sheria, Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru huteuliwa na Rais, na anasaidiwa na Naibu Mkurugenzi Mkuu, wadhifa alionao Mlowola ambaye kabla ya uteuzi huo uliofanywa Oktoba 23, mwaka huu, alikuwa Mkurugenzi wa Intelijensia ya Makosa ya Jinai katika Jeshi la Polisi nchini.
Katika hatua nyingine, Rais Magufuli ameagiza kusimamishwa kazi mara moja kwa watumishi waandamizi wanne wa Takukuru waliosafiri nje ya nchi, licha ya Rais kupiga marufuku safari za nje kwa watumishi wa umma.
Watumishi hao ni Mkurugenzi Elimu kwa Umma, Mary Mosha, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Ekwabi Mujungu, Mkurugenzi wa Uhusiano, Doreen Kapwani na Katibu Muhtasi wa Mkurugenzi Mkuu, Rukia Nikitas ambao walisafiri nje ya nchi licha ya kunyimwa kibali cha safari kutoka kwa Rais ama Katibu Mkuu Kiongozi.
Kutokana na hatua hiyo ya Rais Magufuli, Balozi Sefue amewataka watumishi wengine wa umma, kutii agizo la Rais na kuonya kuwa atakayekiuka atachukuliwa hatua kali. Katika moja ya hatua za kubana matumizi ya serikali, Rais Magufuli alitangaza kufuta safari zote za nje kwa watumishi wa umma, isipokuwa kwa vibali maalumu.
Monday, December 14, 2015
Thursday, December 10, 2015
Rais Magufuli atangaza baraza la Mawaziri
Rais Magufuli Atangaza baraza la Mawaziri
Mawaziri Hao ni
Waziri- Augustino Mahiga, Naibu Waziri - Dk. Suzan Kolimba
Waziri-Nape Nnauye
Waziri -Sospeter Muhongo na Naibu Waziri-Medard Kalemani
Waziri -Jenista Mhagama
mawaziri wawili - Simbachawene na Kairuki
Waziri - January Makamba Naibu waziri Luhaga Mpina.
Waziri ni Charles Kitwanga
Waziri wake ni Wiliam Lukuvi Naibu Angelina Mabula.
Waziri - Husein Mwinyi
Waziri - Harrison Mwakyembe
Waziri - January Makamba
Waziri- Mwigulu Nchemba Naibu Waziri- William Tate Ole Nashon
Waziri - Charles Mwijage
Waziri - Ummy Mwalimu - Naibu - Dk Hamis kigwangalla
Waziri - bado hajapatikana - Naibu Waziri -Stela manyanya
Waziri - bado hajapatikana na Naibu Waziri - Injinia Ramo Makani
Waziri - bado hajapatikana, Naibu Waziri - Dk. Ashantu Kijachi
Waziri - bado hajapatikana, Naibu Waziri -Edwin Ngonyani
Wednesday, December 02, 2015
Serikali yachunguza ufisadi wa dola mil 6
SERIKALI inachunguza ufisadi wa Dola za Marekani milioni sita, ambazo
Benki ya Stanbic Tanzania pamoja na Kampuni ya Egma ya nchini,
iliongeza katika malipo ya ada ya mkopo, ambao Serikali iliomba kwa
Benki ya Standard ya Uingereza mwaka 2013.
Imesema inafanya uchunguzi wa ndani ili kubaini fedha hizo za kigeni zilizoingizwa kwenye akaunti ya Egma, zimekwenda wapi na kama zilitumika kuhonga, zimemhonga nani. Akizungumza na waandishi wa habari jana Ikulu Dar es Salaam, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue alisema hatua hiyo imekuja baada ya Taasisi ya Uchunguzi wa Makosa Makubwa ya Ufisadi ya Uingereza (SFO) kushinda kesi katika Mahakama ya Southwark Crown ya Uingereza dhidi ya Stanbic Tanzania inayomilikiwa na Standard Group.
“Sasa baada ya Taasisi ya SFO kushinda kesi, Tanzania tunarudi kufanya uchunguzi wa ndani kubaini hizo fedha dola milioni sita zilizoingizwa kwenye akaunti ya kampuni ya Egma na kutolewa zote muda mfupi zimekwenda wapi, na kama zilitumika kumhonga mtu, ni nani,” alifafanua Balozi Sefue.
Balozi Sefue aliwataja wamiliki wa Egma kuwa ni aliyekuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato (TRA), Harry Kitilya, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Soko la Mitaji Tanzania, Fratern Mboya na Mkurugenzi Gasper Njuu.
Alitoa mwito kwa wamiliki hao, kutoa ushirikiano wakati wa uchunguzi wa sakata hilo na kwamba mara baada ya uchunguzi kukamilika, iwapo kutabainika makosa ya rushwa au mengine, sheria itachukua mkondo wake.
“Ombi letu na ombi la Rais John Magufuli watu hawa wanatakiwa kutoa ushirikiano na pengine ameongezeka mmiliki kwenye kampuni hiyo, wahakikishe wanatoa ushirikiano,” alisisitiza Balozi Sefue. Akizungumzia sakata hilo, Balozi Sefue alisema sio jambo geni kama ambavyo baadhi ya vyombo vya habari nchini vimeripoti jana, na kwamba tangu mwaka 2013, Tanzania inalifahamu na ndiyo iliyolipeleka SFO kuchunguzwa.
Akifafanua, alisema katika mwaka 2012/13, serikali ilifanya utaratibu wa kawaida unaofanywa na nchi mbalimbali duniani wa kukopa kwenye taasisi za benki ambapo Benki ya Standard ilikubali kuikopesha.
Alisema katika mkopo huo, serikali ilihitaji Dola za Marekani milioni 600 kwa ajili ya kuendeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ambapo kwa kawaida benki husika huingia mkataba na benki nyingine inayopewa jukumu la kutoa mkopo huo.
Alisema katika mchakato huo, Benki ya Standard kupitia kampuni tanzu iliipa Benki ya Stanbic Tanzania kazi hiyo ambapo fedha hizo zilipatikana na kwamba katika mchakato wa mkopo huo, ada ya mkopo serikali ilitozwa asilimia 2.4 ya mkopo.
Aliyataja masharti mengine kwamba yalikuwa ni kulipa mkopo riba kwa miaka saba, na kwamba deni hilo litalipwa kwa miaka saba, ambapo linapaswa kumalizika mwaka 2019. Balozi Sefue alifafanua kwamba baada ya mkopo kutolewa nusu ya kwanza, Mtendaji Mkuu wa benki hiyo wakati huo, Bashir Awale alikuwa na matatizo na watumishi, na Benki Kuu (BoT) iliingilia kati na kufanya uchunguzi.
Katika uchunguzi huo, kulibainika kasoro nyingi zikiwemo ulipaji wa fedha kwenye kampuni bila maelezo ikiwemo Kampuni ya Egma ambayo ilibainika kulipwa Dola za Marekani milioni sita.
Alisema fedha hizo zilionekana zimeingizwa kwenye Egma na kutolewa zote bila kutozwa kodi, ambapo katika taarifa yao ya ukaguzi, BoT ililionesha hilo na mambo mengine yaliyobaini na kumkabidhi Mwenyekiti wa Benki ya Stanbic Tanzania.
Hata hivyo, baada ya taarifa hiyo kupokewa, mwenyekiti wa benki hiyo aliitisha mkutano wa Bodi ya benki na waliipitia taarifa hiyo ya BoT na taarifa kupeleka Kitengo ya Uchunguzi cha Kimataifa cha Intelijensia.
Alisema katika uchunguzi huo, ndipo ilibainika kwamba nchi ilitozwa ada zaidi, ambapo ada ya mkopo halali ilikuwa Dola za Marekani milioni 1.4, lakini Stanbic walichukua Dola za Marekani milioni 2.4.
Alisema fedha hizo zilizoamriwa na Mahakama nchini Uingereza kwamba Benki ya Standard iilipe Tanzania ni zile ambazo hazikupaswa kuchukuliwa, ambazo ni dola milioni sita na dola milioni moja ni faida.
Imesema inafanya uchunguzi wa ndani ili kubaini fedha hizo za kigeni zilizoingizwa kwenye akaunti ya Egma, zimekwenda wapi na kama zilitumika kuhonga, zimemhonga nani. Akizungumza na waandishi wa habari jana Ikulu Dar es Salaam, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue alisema hatua hiyo imekuja baada ya Taasisi ya Uchunguzi wa Makosa Makubwa ya Ufisadi ya Uingereza (SFO) kushinda kesi katika Mahakama ya Southwark Crown ya Uingereza dhidi ya Stanbic Tanzania inayomilikiwa na Standard Group.
“Sasa baada ya Taasisi ya SFO kushinda kesi, Tanzania tunarudi kufanya uchunguzi wa ndani kubaini hizo fedha dola milioni sita zilizoingizwa kwenye akaunti ya kampuni ya Egma na kutolewa zote muda mfupi zimekwenda wapi, na kama zilitumika kumhonga mtu, ni nani,” alifafanua Balozi Sefue.
Balozi Sefue aliwataja wamiliki wa Egma kuwa ni aliyekuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato (TRA), Harry Kitilya, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Soko la Mitaji Tanzania, Fratern Mboya na Mkurugenzi Gasper Njuu.
Alitoa mwito kwa wamiliki hao, kutoa ushirikiano wakati wa uchunguzi wa sakata hilo na kwamba mara baada ya uchunguzi kukamilika, iwapo kutabainika makosa ya rushwa au mengine, sheria itachukua mkondo wake.
“Ombi letu na ombi la Rais John Magufuli watu hawa wanatakiwa kutoa ushirikiano na pengine ameongezeka mmiliki kwenye kampuni hiyo, wahakikishe wanatoa ushirikiano,” alisisitiza Balozi Sefue. Akizungumzia sakata hilo, Balozi Sefue alisema sio jambo geni kama ambavyo baadhi ya vyombo vya habari nchini vimeripoti jana, na kwamba tangu mwaka 2013, Tanzania inalifahamu na ndiyo iliyolipeleka SFO kuchunguzwa.
Akifafanua, alisema katika mwaka 2012/13, serikali ilifanya utaratibu wa kawaida unaofanywa na nchi mbalimbali duniani wa kukopa kwenye taasisi za benki ambapo Benki ya Standard ilikubali kuikopesha.
Alisema katika mkopo huo, serikali ilihitaji Dola za Marekani milioni 600 kwa ajili ya kuendeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ambapo kwa kawaida benki husika huingia mkataba na benki nyingine inayopewa jukumu la kutoa mkopo huo.
Alisema katika mchakato huo, Benki ya Standard kupitia kampuni tanzu iliipa Benki ya Stanbic Tanzania kazi hiyo ambapo fedha hizo zilipatikana na kwamba katika mchakato wa mkopo huo, ada ya mkopo serikali ilitozwa asilimia 2.4 ya mkopo.
Aliyataja masharti mengine kwamba yalikuwa ni kulipa mkopo riba kwa miaka saba, na kwamba deni hilo litalipwa kwa miaka saba, ambapo linapaswa kumalizika mwaka 2019. Balozi Sefue alifafanua kwamba baada ya mkopo kutolewa nusu ya kwanza, Mtendaji Mkuu wa benki hiyo wakati huo, Bashir Awale alikuwa na matatizo na watumishi, na Benki Kuu (BoT) iliingilia kati na kufanya uchunguzi.
Katika uchunguzi huo, kulibainika kasoro nyingi zikiwemo ulipaji wa fedha kwenye kampuni bila maelezo ikiwemo Kampuni ya Egma ambayo ilibainika kulipwa Dola za Marekani milioni sita.
Alisema fedha hizo zilionekana zimeingizwa kwenye Egma na kutolewa zote bila kutozwa kodi, ambapo katika taarifa yao ya ukaguzi, BoT ililionesha hilo na mambo mengine yaliyobaini na kumkabidhi Mwenyekiti wa Benki ya Stanbic Tanzania.
Hata hivyo, baada ya taarifa hiyo kupokewa, mwenyekiti wa benki hiyo aliitisha mkutano wa Bodi ya benki na waliipitia taarifa hiyo ya BoT na taarifa kupeleka Kitengo ya Uchunguzi cha Kimataifa cha Intelijensia.
Alisema katika uchunguzi huo, ndipo ilibainika kwamba nchi ilitozwa ada zaidi, ambapo ada ya mkopo halali ilikuwa Dola za Marekani milioni 1.4, lakini Stanbic walichukua Dola za Marekani milioni 2.4.
Alisema fedha hizo zilizoamriwa na Mahakama nchini Uingereza kwamba Benki ya Standard iilipe Tanzania ni zile ambazo hazikupaswa kuchukuliwa, ambazo ni dola milioni sita na dola milioni moja ni faida.
Wednesday, November 18, 2015
MAtokeo ya Michezo ya raundi ya pili ya kusaka tiketi ya kushiriki Kombe la Dunia
Matokeo ya Michezo ya raundi ya pili ya kusaka tiketi ya kushiriki Kombe la Dunia
Matokeo ya mechi zilizochezwa Jumanne ni kama ifuatavyo:Cameroon 0-0 Niger (Jumla 3-0)
Congo 2-1 Ethiopia (Jumla 6-4)
Nigeria 2-0 Swaziland (Jumla 2-0)
Ghana 2-0 Comoro (Jumla 2-0)
Misri 4-0 Chad (Jumla 4-1)
Ivory Coast 3-0 Liberia (Jumla 4-0)
Tunisia 2-1 Mauritania (Jumla 4-2)
Afrika Kusini 1-0 Angola (Jumla 4-1)
Burkina Faso 2-0 Benin (Jumla 3-2)
Senegal 3-0 Madagascar (Jumla 5-2)
Mali 2-0 Botswana (Jumla 3-2)
Tanzania 0-7 Algeria(jumla 2-9)
Kenya 0-2 Cape Verde(jumla 1-2)
Saturday, November 07, 2015
Taarifa..
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli leo asubuhi katika Ikulu ya Dar es Salaam amefanya kikao na Makatibu wakuu, Manaibu Makatibu wakuu, Gavana wa Benki Kuu Prof. Benno Ndulu na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ili kutoa uelekeo wa Serikali anayoitaka mara baada ya kuapishwa. “Nataka Serikali iendelee kwa nguvu zote na katika kutekeleza dhana ya ‘HAPA KAZI TU’ na viongozi kuzingatia na kukumbuka ahadi nilizotoa ili zianze kuonekana na kufanyiwa kazi mara moja” Rais Magufuli amesema. Katika Kikao chake, Rais ametoa mwongozo na kusisitizia kuwa ni lazima kila mtendaji Serikalini kuuzingatia, kufuata sheria na taratibu ili taifa lisonge mbele kwa ufanisi zaidi. Katika kikao hicho Rais ameelekeza mambo kadhaa ambayo watendaji hao wanapaswa kuyasimamia, kuyawekea mikakati na kuyapanga vizuri ili atakapo teua Baraza lake la Mawaziri mambo hayo yawe tayari ili Mawaziri watakaoteuliwa waweze kuyasimamia bila kukosa. Mambo hayo muhimu ni kama ifuatavyo: Kuanzia mwezi Januari mwaka 2016, wanafunzi wote wanaoanza shule watasoma bure bila kulipa ada, Katika jambo hili, Rais amewataka watendaji kuanza kuliwekea mikakati tayari kwa utekelezaji Suala la mikopo ya wanafunzi nalo lifanyiwe kazi na mipango yake ikamilike kwa ajili ya utekelezaji mzuri zaidi Amefuta safari zote za nje ya nchi kuanzia leo hadi hapo atakapolitolea suala hilo maamuzi mengine na kueleza kuwa shughuli zote zinazotakiwa kufanywa nje ya nchi zifanywe na kusimamiwa na mabalozi wa Tanzania wanaowakilisha nchi huko nje. Pengine patokee jambo la dharura sana na hata hilo lazima kibali kitolewe na Rais au Katibu Mkuu Kiongozi. Badala yake Rais amewataka watendaji hao kufanya zaidi ziara za kwenda vijijini ili kuzijua na kutatua kero za wananchi wa Tanzania. Katika Kikao hicho, Rais amemtaka Kamishna wa TRA, Ndugu Rished Bade kusimamia kwa makini zoezi la ukusanyaji wa mapato nchini na kuhakikisha kero ndogo ndogo kwa wananchi lianze kutekelezwa kama alivyo ahidi kwa kufanyiwa kazi mapema zaidi. Rais ameitaka TRA kukusanya mapato hayo kutoka kwa wafanya biashara wakubwa zaidi na wale wanaokwepa kodi bila kuogopa mtu wala taasisi yoyote hapa Tanzania na kusisitiza kuwa katika Serikali hii wa kutoa maamuzi vinginevyo zaidi ya haya ni yeye Rais ama Makamu wake. Rais Magufuli pia ameagiza usimamizi katika suala la manunuzi ambalo limekuwa likitumika vibaya na kuwa mwanya wa kuibia Serikali kwa watu kuongeza bei ya vitu hata kama ni vya bei ndogo kabisa katika jamii. “Ikitokea suala hilo likagundulika kwa watu kuongeza bei ya vitu, watendaji watawajibishwa mara moja”. Rais amesema, na kuwataka watendaji hao kufanya kazi zao kwa kuzingatia Sheria na taratibu zilizopo na kuzingatia maadili mema ya kazi. ………………………MWISHO…………………… Imetolewa na Premi Kibanga, Mwandishi wa Habari wa Rais, Msaidizi Ikulu, DAR ES SALAAM. 7 Novemba, 2015
Friday, November 06, 2015
Dkt.Magufuri aapisha rasmi jana
MHESHIMIWA Dkt John Pombe Joseph Magufuli ameapishwa kuwa Rais wa
Serikali ya Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kwa kipindi
cha miaka mitano ijayo.
Sherehe ya kuapishwa kwake imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa ndani na nje ya Tanzania. Sambamba na kuapishwa Rais Magufuli, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhus Hassan pia ameapishwa.
Sherehe ya kuapishwa kwake imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa ndani na nje ya Tanzania. Sambamba na kuapishwa Rais Magufuli, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhus Hassan pia ameapishwa.
Wednesday, November 04, 2015
Warais watakaokuja kwenye sherehe ya kuapisha JPM
MARAIS wanane wa Afrika ni miongoni mwa viongozi mbalimbali kutoka
nje ya nchi, watakaohudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Awamu ya
Tano wa Tanzania, Dk John Pombe Magufuli.
Rais Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Magufuli ataapishwa rasmi kuwa Rais wa Awamu ya Tano kesho kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam. Dk Magufuli (56) alitangazwa mshindi wa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka huu, baada ya kupata kura 8,882,935, sawa na asilimia 58.46 ya kura halali zilizopigwa, hivyo kumrithi Rais Jakaya Kikwete katika Ikulu ya Magogoni, ambayo tayari imeshakaliwa na marais wengine wanne.
Kwa mujibu wa taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa iliyotolewa jana Dar es Salaam, sherehe za uapisho zitahudhuriwa na Wakuu wa Nchi na Serikali kutoka mataifa mbalimbali, Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa na Kikanda na Wawakilishi mbalimbali kutoka nje ya nchi. Iliwataja miongoni mwa marais watakaohudhuria sherehe hizo ni Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe, Rais Yoweri Museveni wa Uganda, Rais Paul Kagame wa Rwanda na Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini.
Wengine ni Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya, Rais Filipe Nyusi wa Msumbiji na Rais Edgar Lungu wa Zambia. Taarifa ya Mambo ya Nje ilieleza kuwa Malawi itawakilishwa na Makamu wa Rais, Saulos Chilima wakati Namibia itawakilishwa na Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje, Netumbo Nandi-Ndaitwah. Aidha, Serikali ya China itawakilishwa na Makamu Mwenyekiti wa Chama Tawala.
“Vilevile nchi nyingine ambazo zimethibitisha kushiriki na zitawakilishwa na kati ya Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Spika au Balozi ni pamoja na Burundi, Comoro, Angola, Botswana, Lesotho, Madagascar na Mauritius. “Nyingine ni Norway, Oman, Sudan Kusini, Sweden, Umoja wa Falme za Kiarabu, Marekani, Uingereza, Shelisheli, Swaziland, Algeria, Misri, Benin, Denmark, Ethiopia, Finland, Ufaransa, Ghana, India, Japan, Kuwait, Uholanzi na Nigeria,” ilifafanua taarifa hiyo.
Ilieleza kuwa Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa na Kikanda, waliothibitisha kushiriki au kutuma wawakilishi wao ni Umoja wa Mataifa (UN), Umoja wa Afrika (AU), Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), Umoja wa Ulaya (EU) na Jumuiya ya Ukanda wa Nchi za Maziwa Makuu (ICGLR).
Wabunge wapya kuwasili Dar Katika hatua nyingine, wabunge wapya waliochaguliwa katika Uchaguzi Mkuu wanatarajiwa kuwasili Dar es Salaam leo kwa ajili ya kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais Mteule, Dk John Magufuli zitakazofanyika kesho.
Akizungumzia kuwasili kwa wabunge hao, Ofisa Habari Mwandamizi wa Bunge, Prosper Minja alisema wabunge hao wanatarajiwa kuwasili leo Dar es Salaam wakiwa na vyeti vyao vya kuteuliwa kuwa wabunge vinavyotolewa na Msimamizi wa Uchaguzi wa eneo husika.
“Tunategemea kesho (leo), wabunge wapya watawasili kwa ajili ya kuhudhuria sherehe ya kuapishwa kwa rais mteule na tunategemea waje na cheti hicho pamoja na kitambulisho kingine kinachomtambulisha,” alisema Minja.
Alisema mara baada ya wabunge hao kuwasili, wanatakiwa kwenda Ukumbi wa Karimjee kwa ajili ya kutambuliwa na kupewa kitambulisho cha siku ya sherehe za kuapishwa kwa Rais Mteule, Dk Magufuli.
Tamko la Jeshi la Polisi Wakati huo huo, Jeshi la Polisi nchini limejipanga kuhakikisha usalama na ulinzi unaimarishwa wakati wa kuelekea sherehe za kumwapisha Rais Mteule, Dk John Magufuli.
Akizungumza jana Dar es Salaam, Kamishna wa Oparesheni na Mafunzo, Makao Mkauu ya Polisi, Paul Chagonja alisema jeshi lake kwa kushirikiana na vyombo vingine vya usalama, litahakikisha kunakuwa na usalama wa raia na mali zao katika kuelekea sherehe za kumuapisha Rais Mteule.
“Niwaombe wananchi kutupa ushirikiano kwa kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi pindi waonapo vishawishi ama vitendo vyovyote vya uvunjifu wa sheria,” alisema Kamishna Chagonja. Aidha, Chagonja aliwataka wananchi kuendelea kuheshimu sheria za nchi na kujiepusha na vitendo vinavyoweza kuhatarisha usalama wa raia na mali zao.
“Jeshi la Polisi linawataka wananchi kote nchini kuendelea kuheshimu sheria za nchi na kujiepusha na vitendo vya aina yoyote ile ambavyo vinaweza kuhatarisha usalama wa raia na mali ikiwemo maandamano yanayopangwa bila kufuata taratibu,” alisema Chagonja na kuongeza: “Jeshi la Polisi halitasita kuchukua hatua kali kwa mtu au kikundi chochote kitakachoonesha viashiria vya uvunjifu wa sheria ama kutaka kuvuruga amani ya nchi yetu.”
Mbali ya kuwashukuru wananchi na wadau waliotoa ushirikiano kuhakikisha amani ya Watanzania inadumu katika kipindi cha uchaguzi na wakati huu wa kuelekea kuapishwa kwa Rais Mteule, alikiri jeshi hilo kuwashikilia watu kadhaa na baadhi yao kufikishwa mahakamani kutokana na kufanya makosa wakati wa uchaguzi.
Bila kutaja idadi, Chagonja alisema, “Ni kweli kuna watu kadhaa tumewakamata kwa makosa mbalimbali wakati wa uchaguzi, kuna wengine wamefikishwa mahakamani, na kuna wengine bado wanashikiliwa kwa mahojiano zaidi na wengine wamewekewa dhamana.” Imeandikwa na Ikunda Eric na Anastazia Anyimike.
Rais Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Magufuli ataapishwa rasmi kuwa Rais wa Awamu ya Tano kesho kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam. Dk Magufuli (56) alitangazwa mshindi wa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka huu, baada ya kupata kura 8,882,935, sawa na asilimia 58.46 ya kura halali zilizopigwa, hivyo kumrithi Rais Jakaya Kikwete katika Ikulu ya Magogoni, ambayo tayari imeshakaliwa na marais wengine wanne.
Kwa mujibu wa taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa iliyotolewa jana Dar es Salaam, sherehe za uapisho zitahudhuriwa na Wakuu wa Nchi na Serikali kutoka mataifa mbalimbali, Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa na Kikanda na Wawakilishi mbalimbali kutoka nje ya nchi. Iliwataja miongoni mwa marais watakaohudhuria sherehe hizo ni Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe, Rais Yoweri Museveni wa Uganda, Rais Paul Kagame wa Rwanda na Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini.
Wengine ni Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya, Rais Filipe Nyusi wa Msumbiji na Rais Edgar Lungu wa Zambia. Taarifa ya Mambo ya Nje ilieleza kuwa Malawi itawakilishwa na Makamu wa Rais, Saulos Chilima wakati Namibia itawakilishwa na Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje, Netumbo Nandi-Ndaitwah. Aidha, Serikali ya China itawakilishwa na Makamu Mwenyekiti wa Chama Tawala.
“Vilevile nchi nyingine ambazo zimethibitisha kushiriki na zitawakilishwa na kati ya Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Spika au Balozi ni pamoja na Burundi, Comoro, Angola, Botswana, Lesotho, Madagascar na Mauritius. “Nyingine ni Norway, Oman, Sudan Kusini, Sweden, Umoja wa Falme za Kiarabu, Marekani, Uingereza, Shelisheli, Swaziland, Algeria, Misri, Benin, Denmark, Ethiopia, Finland, Ufaransa, Ghana, India, Japan, Kuwait, Uholanzi na Nigeria,” ilifafanua taarifa hiyo.
Ilieleza kuwa Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa na Kikanda, waliothibitisha kushiriki au kutuma wawakilishi wao ni Umoja wa Mataifa (UN), Umoja wa Afrika (AU), Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), Umoja wa Ulaya (EU) na Jumuiya ya Ukanda wa Nchi za Maziwa Makuu (ICGLR).
Wabunge wapya kuwasili Dar Katika hatua nyingine, wabunge wapya waliochaguliwa katika Uchaguzi Mkuu wanatarajiwa kuwasili Dar es Salaam leo kwa ajili ya kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais Mteule, Dk John Magufuli zitakazofanyika kesho.
Akizungumzia kuwasili kwa wabunge hao, Ofisa Habari Mwandamizi wa Bunge, Prosper Minja alisema wabunge hao wanatarajiwa kuwasili leo Dar es Salaam wakiwa na vyeti vyao vya kuteuliwa kuwa wabunge vinavyotolewa na Msimamizi wa Uchaguzi wa eneo husika.
“Tunategemea kesho (leo), wabunge wapya watawasili kwa ajili ya kuhudhuria sherehe ya kuapishwa kwa rais mteule na tunategemea waje na cheti hicho pamoja na kitambulisho kingine kinachomtambulisha,” alisema Minja.
Alisema mara baada ya wabunge hao kuwasili, wanatakiwa kwenda Ukumbi wa Karimjee kwa ajili ya kutambuliwa na kupewa kitambulisho cha siku ya sherehe za kuapishwa kwa Rais Mteule, Dk Magufuli.
Tamko la Jeshi la Polisi Wakati huo huo, Jeshi la Polisi nchini limejipanga kuhakikisha usalama na ulinzi unaimarishwa wakati wa kuelekea sherehe za kumwapisha Rais Mteule, Dk John Magufuli.
Akizungumza jana Dar es Salaam, Kamishna wa Oparesheni na Mafunzo, Makao Mkauu ya Polisi, Paul Chagonja alisema jeshi lake kwa kushirikiana na vyombo vingine vya usalama, litahakikisha kunakuwa na usalama wa raia na mali zao katika kuelekea sherehe za kumuapisha Rais Mteule.
“Niwaombe wananchi kutupa ushirikiano kwa kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi pindi waonapo vishawishi ama vitendo vyovyote vya uvunjifu wa sheria,” alisema Kamishna Chagonja. Aidha, Chagonja aliwataka wananchi kuendelea kuheshimu sheria za nchi na kujiepusha na vitendo vinavyoweza kuhatarisha usalama wa raia na mali zao.
“Jeshi la Polisi linawataka wananchi kote nchini kuendelea kuheshimu sheria za nchi na kujiepusha na vitendo vya aina yoyote ile ambavyo vinaweza kuhatarisha usalama wa raia na mali ikiwemo maandamano yanayopangwa bila kufuata taratibu,” alisema Chagonja na kuongeza: “Jeshi la Polisi halitasita kuchukua hatua kali kwa mtu au kikundi chochote kitakachoonesha viashiria vya uvunjifu wa sheria ama kutaka kuvuruga amani ya nchi yetu.”
Mbali ya kuwashukuru wananchi na wadau waliotoa ushirikiano kuhakikisha amani ya Watanzania inadumu katika kipindi cha uchaguzi na wakati huu wa kuelekea kuapishwa kwa Rais Mteule, alikiri jeshi hilo kuwashikilia watu kadhaa na baadhi yao kufikishwa mahakamani kutokana na kufanya makosa wakati wa uchaguzi.
Bila kutaja idadi, Chagonja alisema, “Ni kweli kuna watu kadhaa tumewakamata kwa makosa mbalimbali wakati wa uchaguzi, kuna wengine wamefikishwa mahakamani, na kuna wengine bado wanashikiliwa kwa mahojiano zaidi na wengine wamewekewa dhamana.” Imeandikwa na Ikunda Eric na Anastazia Anyimike.
Friday, October 30, 2015
Kutangazwa rasmi mshindi wa urais 2015 kutokaa ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar Es Salaam
Kutangazwa rasmi mshindi wa urais 2015 kutokaa ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar Es Salaam,mh magufuri amepewa cheti.hafla hiyo iliyojumuisha watu mbalimbali wakiwemo jaji mkuu mstaafu mh warioba..na wasimamizi wa uchaguzi wa nje akiwemo mh rais wa nigeria obasanjo.
Thursday, October 29, 2015
Dr. John Pombe Magufuli (CCM) ametangazwa mshindi wa kiti cha Urais Tanzania 2015
Breaking Dr. John Pombe Magufuli (CCM) ametangazwa mshindi wa kiti cha Urais Tanzania 2015, kapata 58%, E. Lowassa 39%
TAARIFA YA CCM KWA VYOMBO VYA HABARI, OKTOBA 28, 2015
TAARIFA YA CCM KWA VYOMBO VYA HABARI, OKTOBA 28, 2015
CCM inapenda kutoa taarifa ifuatayo kwa wana-CCM na kwa umma: MALALAMIKO YA CCM KUHUSU MATOKEO KWENYE BAADHI YA MAJIMBO Chama cha Mapinduzi hakijaridhishwa na utaratibu wa kukusanya na kujumlisha matokeo kwenye baadhi ya majimbo. Katika majimbo manne kumekuwa na ukiukwaji mkubwa wa utaratibu wa uchaguzi, hasa katika kujumlisha matokeo, uliopelekea wabunge wa upinzani kutangazwa washindi. Majimbo hayo ni Iringa Mjini, Mikumi, Ndanda na Kawe. Wasimamizi wa uchaguzi katika majimbo haya wamevuruga uchaguzi. Kutokana na utata uliokuwa umejitokeza wakati wa zoezi la kujumlisha kura, CCM iliomba kura zihesabiwe upya lakini ikanyimwa haki hiyo ya msingi ambayo iko kwenye sheria. Kwenye baadhi ya majimbo, ikiwemo Nyamagana, wapinzani walipewa haki ya kura kuhesabiwa upya. Kwa msingi huo, CCM imeamua kwenda mahakamani kupinga matokeo ya uchaguzi katika majimbo haya. Tunataka sote tujiridhishe kwamba utashi wa wananchi umeheshimiwa. Bado tunaendelea kukusanya taarifa za maeneo mengine kama kulikuwa na ukiukwaji mkubwa uliobadilisha matakwa ya wapiga kura. Hata hivyo, tunakiri kwamba kwenye maeneo mengi tulikopoteza viti vya Ubunge, tumepoteza kihalali, hatuna malalamiko, tunaheshimu maamuzi ya wananchi, na tutafanya tathmini baada ya uchaguzi ili tubaini makosa na kuyarekebisha. MAONI YA WAANGALIZI WA UCHAGUZI CCM imepokea maoni ya awali ya waangalizi wa uchaguzi. Tumefarijika kwamba karibu wote wametoa kauli ya pamoja kwamba uchaguzi huu ulikuwa wa haki na huru, uliofanyika kwa uwazi na kwa amani – na kwamba changamoto zilizojitokeza ni ndogo na zimetokea katika maeneo machache kiasi zisingeweza kubadilisha matokeo ya uchaguzi yanayotangazwa sasa. Tumepokea mapendekezo waliyoyatoa kwa wadau mbalimbali kuhusu namna ya kuboresha mchakato wa uchaguzi kwa miaka ijayo, na hivyo kuimarisha demokrasia nchini mwetu. Kwa kauli za waangalizi hawa, kwamba, kwa jinsi uchaguzi ulivyoendeshwa, matokeo yanayotangazwa sasa ni kielelezo sahihi cha utashi wa Watanzania kuhusu viongozi wanaowataka. MALALAMIKO YA UKAWA Tumesikia malalamiko ya viongozi wa UKAWA kupitia mkutano wao na waandishi wa habari jana. Tumeshangazwa na kauli kwamba hawakubali matokeo ya Urais yanayotangazwa na Tume. Hata hivyo, matokeo ya Ubunge wanayakubali na, kule wanakoshinda, wanayasheherekea. Tunashangazwa kwasababu Tume iliyoandaa uchaguzi wa Rais ni hiyo hiyo iliyoandaa uchaguzi wa Wabunge, wasimamizi ni walewale, vituo ni vilevile, na sheria na taratibu zilizotumika ni zilezile. Hata fomu ya matokeo walizosaini wakala wao kwenye vituo vya kupiga kura, zimegawanywa katika sehemu (columns) tatu: Urais, Ubunge na Udiwani. Mawakala wao walisaini fomu hizo kwenye vituo vya kupiga kura. Wameanza kuwa na matatizo na matokeo haya baada ya kuona mwelekeo wa kushindwa. Kama mwelekeo ungekuwa tofauti, wangekuwa na imani na Tume, wasimamizi na taratibu zote. Tunaomba ifike pahala sasa kwamba, katika kuijenga demokrasia yetu na kuliimarisha taifa letu, tuanze utamaduni mpya wa anayeshindwa kunyanyua simu kumpigia anayeshinda na kumpongeza. Nafasi ya mwisho aliyonayo Mgombea wa UKAWA kuendelea kujijengea heshima katika jamii yetu, na kuwa mwanademokrasia, ni kwa kufanya hivyo siku Dkt. Magufuli atakapotangazwa mshindi. Kwetu sisi CCM, kuchagua wagombea bora na kuwanadi na kutengeneza sera bora na kuzinadi, pamoja na rekodi yetu katika uongozi wa nchi, ndio njia zetu pekee za ushawishi. Katika uchaguzi huu, wananchi wamefanya maamuzi yao kwa uhuru na utashi, ikiwemo kuwaangusha mawaziri sita ambao tuliwasimamisha kama wagombea wetu katika majimbo mbalimbali. Nguvu na utashi wa wananchi umejidhihirisha katika uchaguzi huu. Mchakato wa uchaguzi sasa unakaribia kufikia ukingoni, tutawapata madiwani, wabunge na Rais, tunapaswa kuendelea na maisha na tuwape nafasi watutumikie. Jitihada tunazoziona sasa za viongozi wa UKAWA za kuendeleza siasa za uchaguzi kwenye mitaa ya miji yetu kwa njia za vurugu na maandamano hazikubaliki hata kidogo. Tunalaani kitendo cha wafuasi wa UKAWA kuchoma ofisi za CCM katika Wilaya ya Mbozi. Amani ya nchi hii ina thamani kuliko hitaji la madaraka la mtu yoyote. Wenzetu wa UKAWA wana haki ya kulalamika lakini hawana haki ya kuiingiza nchi yetu machafukoni kwa kuwakusanya vijana na kuwaingiza mitaani wafanye vurugu na kuhatarisha maisha, kuharibu mali na kusimamisha shughuli za watu wengine. Tunawaomba Watanzania waendelee na shughuli zao kama kawaida huku kila mmoja akitambua wajibu wake wa kuilinda amani ya nchi yetu. January Makamba Mjumbe wa Kamati ya Kampeni ya CCM 28.10.2015
Wednesday, October 28, 2015
Uchaguzi wa Zanzibar wafutwa
Mwenyekiti wa tume ya taifa ya uchaguzi zanzibar (zec) jecha salim jecha ametangaza kufutwa kwa uchaguzi wa wa serikali ya mapinduzi zanzibar kwahiyo uchaguzi utafanyika baada ya siku 90.
Monday, October 26, 2015
Wednesday, October 14, 2015
Wanafunzi wa vyuo-NEC
TUME ya taifa ya Uchaguzi sasa imethibitisha kuwa wanafunzi wa Vyuo vikuu hawatapiga kura katika uchaguzi mkuu ujao. Akizungumza katika kipindi cha kikaangoni kinachorushwa na EATV, jana Emmanuel Kawishe amesema kuwa wanafunzi hao hawataweza kupiga kura kuchagua diwani,mbunge au Rais kwa kuwa sheria inasema kila mtu atapiga kura pale alipojiandikishia. “Sheria ya uchaguzi kifungu cha 61(3)a kuwa kila aliyejiandikisha atapiga kura alipojiandikisha” alisema Kawishe. Aidha amefafanua kuwa vituo vyote vya kupigia kura vitafunguliwa saa 1 asubuhi na vitafungwa saa kumi jioni hivyo kuwatahadharisha wapiga kura wote kuwepo kituoni kabla muda wa kufunga. Taarifa ya kutopiga kura kwa wanafunzi wa vyuo vikuu imekuwa rasmi huku viongozi wa Wanafunzi vyuo vikuu wakihangaika kupeleka shauri mahakamani ili serikali ifungue vyuo kwa wakati na kuwapa wao fursa ya kupiga kura. Hii ni mara ya pili kwa Vyuo vikuu kufunguliwa baada ya Oktoba, kwa mara ya kwanza ilifanyika vile vile mwaka 2010 kwa kisingizio cha mikopo ya Elimu ya juu. Ushahidi kutoka kwa wanafunzi mbalimbali waliowahi kunufaika na mikopo wanasema serikali haijawahi kutoa mikopo kwa wakati licha ya sababu za mara kwa mara kuahirisha kufungua vyuo wakati wa Uchaguzi. Mapema mwaka huu, Shirikisho la wanafunzi wa wanachadema wa Vyuo vikuu (Chaso) kupitia Kaimu Mratibu wao Wilfred Mwalusanya aliitaka NEC kueleza utaratibu wa kuwaandisha wanavyuo ili wakati wa kupiga kura waweze kushiriki. Tayari tuhuma zimeanza kutolewa na wadau mbalimbali kuwa tume imetumiwa na serikali ya CCM ili kuinusuru sababu wanavyuo wamehamasika kuelekea uchaguzi mkuu mwaka huu.
TAMKO RASMI LA BALOZI JUMA V. MWAPACHU.
TAMKO RASMI LA BALOZI JUMA V. MWAPACHU. NAJIVUA UANACHAMA WA CCM
Ndugu zangu, Kesho ni siku muhimu katika kalenda ya Taifa letu. Tunamkumbuka marehemu Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliyetutoka miaka 16 iliyopita. Nadhani ni siku mwafaka kwangu kufanya maamuzi magumu katika maisha yangu ambayo yanahusu uanasiasa wangu. Mimi ni mwanachama wa CCM tangu mwaka 1967 wakati nilipojiunga na TANU Youth League. Nimepata fursa ya kuwa kiongozi ndani ya Chama hiki. Lakini kuanzia kesho mimi si mwanachama wa CCM tena. Natoa maelezo yafuatayo: Kwa kipindi chapata mwezi na nusu hivi sasa mmekuwa mkisoma makala zangu kuhusu msimamo na mwelekeo wangu katika masuala ya siasa za hapa nchini hususan kuhusu uchaguzi mkuu na mstakabali wa demokrasia nchini mwetu. Nyote mnatambua kwamba kuanzia mchakato wa kumpata mgombe wa Urais ndani ya CCM kule Dodoma, ambako nilipiga kambi, sijayumba katika msimamo wangu kwamba Edward Ngoyai Lowassa ndiye chaguo langu katika kampeni za kumpata Rais mpya wa Taifa letu. Chaguo langu si ndoto wala mlipuko wa mapenzi juu ya Lowassa. Nimemfahamu Lowassa tangu miaka ya 90 nikiwa cadre wa Chama cha Mapinduzi kwa mahusisho katika majukumu ya Kic,ssa amejaaliwa nuru na uwezo wa kuongoza na wa kupendwa na watu. Ni msikivu pamoja na kwamba ni kiongozi asiyependa ukiritimba na utovu wa nidhamu, iwe kwa upande wa watumishi au wananchi wenyewe. Kubwa kwake ni ucha Mungu wake ambao unamsaidia sana katika uongozi unaojali na kuheshimu utu, ukweli na uwazi. Wanaodhani au kutaharuki kwamba eti anaweza au ana hulka ya kulipiza kisasi kwa jambo lolote lile ni waongo; wanajilinda. Lowassa ni chaguo la wengi na CCM, katika busara yake ya kumuengua katika mchakato wa kumpata mgombea wa Urais, kimedhihirisha kutokuwa Chama kinachoendeshwa kwa misingi ya demokrasia. Dalili za Chama hiki kupoteza lengo la kuwa Chama cha watu, na kuwa cha viongozi wachache zilianza siku nyingi na hasa katika kipindi cha uongozi wa Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete. CCM kimebadilika na kuwa Chama cha makundi na migawanyiko yakupambana, si kwa malengo ya itikadi na ujenzi wa Chama, bali ya kumalizana na kutaka kufukuzana. Lowassa angeweza kufukuzwa miaka mingi tu iliyopita! Aliweza kushinda vita hivyo kutokana na kupendwa na wengi ndani ya CCM. Hivyo, kujitoa kwake uanachama wa CCM hivi karibuni ni sahihi kabisa kwasababu CCM si Chama tena cha watu. Kimetekwa. Na mimi nakubaliana na msimamo wa Lowassa na hao waliyofuata kutoka nadani ya CCM. Niliwahi kuandika makala katika ukurasa huu nikimnukuu mshairi mmoja wa Uingereza aliyeandika kwamba, ‘there comes a time when the door opens and allows the future in’. Mlango huo sasa umefunguka usoni mwangu na huu uamuzi wangu maana yake ni kukubali kwamba wakati mpya umewadia; ni wakati wa mabadiliko. Kuendelea kujihisi kwamba ningali mwana CCM wa kadi ni kukubali kujidanganya mwenyewe. Si sawa. Kama marehemu Baba wa Taifa alivyowahi kusema, ‘CCM si mama yangu’. Hivyo ndugu zangu, kuanzia kesho mimi si mwana CCM tena. Nitarejesha rasmi kadi yangu kupitia ofisi ya CCM ya kata yangu Mikocheni, Dar-es-Salaam. Kwa sasa sijaamua kujiunga na Chama kingine. Mwenyezi Mungu anilinde.
Thursday, October 08, 2015
Bado masaa kadhaa Fainali ya BSS..
FAINALI YA BSS ITAFANYIKA KESHO KWA MUJIBU WA VIONGOZI WA BSS
![]() |
| Angel kato mshiriki katika fainali ya bss |
![]() |
| Frida amani mshiriki wa Fainali ya BSS |
![]() |
| Nasibu fonabo mshiriki wa Fainali ya bss |
maelfu wajitokeza kumuaga Mchungaji Mtikila
RAIS Jakaya Kikwete ameongoza mamia ya waombolezaji pamoja na viongozi wa kitaifa, katika kumuaga Mwenyekiti wa Chama cha DP, Mchungaji Christopher Mtikila aliyekufa kwa ajali hivi karibuni mkoani Pwani.
Katika shughuli hiyo, viongozi wengi waliohudhuria walimuelezea Mtikila kuwa ni mwanaharakati wa mageuzi, aliyeipigania Tanganyika mpaka kifo chake, lakini pia alisimamia na kuheshimu taratibu za kisheria na kutaka mabadiliko bila uoga.
Rais Kikwete alifika katika shughuli hiyo ya kumuaga Mtikila iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana, akiambatana na Makamu wa Rais, Dk Mohammed Gharib Bilal na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi.
Viongozi wengine waliohudhuria shughuli hiyo ni Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi, Msajili wa zamani wa vyama hivyo, John Tendwa na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Philip Mangula.
Pia walikuwepo Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa, Peter Mziray ambaye ni Mwenyekiti wa chama cha PPT-Maendeleo, Makamu Mwenyekiti wa Chadema, Profesa Abdallah Safari na Naibu Katibu Mkuu wa TLP, Dotnata Rwechungura.
Akizungumza katika shughuli hiyo ya kumuaga Mtikila ambaye jeneza lake lilifunikwa kwa bendera ya Tanganyika, Msajili wa Vyama vya Siasa, Mutungi aliwataka watanzania kumuenzi mchungaji huyo kwa matendo yake ya kuchukia vurugu na badala yake aliamini zaidi katika sheria.
“Mchungaji Mtikila atakumbukwa kwa misimamo yake mikali. Alipenda kusimamia kile anachokiamini. Lakini kubwa zaidi alitoa mchango katika nyanja ya Sheria, kwa sasa huwezi kuzungumzia masuala ya sheria hususani haki za binadamu bila kumtaja Mtikila,” alisema Mutungi.
Alisema kupitia sekta ya Sheria, mwanaharakati huyo alifanikisha mabadiliko kadhaa, ikiwemo kuingizwa kwenye Katiba kwa kifungu kinachoruhusu mgombea binafsi, lakini pia alifanikisha kubadilishwa kwa kifungu kinachohusu maandamano.
“Huyu alikuwa ni mpambanaji, alifungua kesi nyingi kwa kuwa aliamini katika kufuata sheria na si kuandamana au kufanya vurugu. Naomba tumuenzi kwa kutopenda kushinikiza fujo na maandamano, vyombo vya sheria vipo kama kuna tatizo tuvitumie kutafuta haki,” alisisitiza.
Kwa upande wake, Dk Bilal alimtaja Mchungaji Mtikila kuwa alikuwa ni mtu jasiri, aliyeshirikiana na wenzake bila kujali tofauti za mitazamo waliyonayo. “Mimi nilimfahamu Mtikila kupitia uanaharakati wake wa kutaka mabadiliko, ni kweli alikuwa anataka sana kuirejesha Tanganyika, lakini pamoja na tofauti za fikra zetu, alikuwa anakuja hadi ofisini kwangu kipindi kile nilikuwa Katibu Mkuu Wizara ya Sayansi, Mawasiliano na Teknolojia na tulikuwa tunazungumza sana,” alisema.
Aliwataka watanzania kuiga mfano wa matendo ya Mtikila, kwani kwa sasa nchi inataka watu kama hao wenye mawazo mapya na hawaogopi kuyatoa na kuyatetea bila kudharau mawazo na fikra za wengine.
Maalim Seif, kwa upande wake, alisema alifahamiana na Mtikila kupitia harakati zake za kisiasa na kubainisha kuwa ni mtu anayejiamini, asiye uoga na mwenye kuajimini na kusimamia kile anachokiamini.
Mziray alisema anaipongeza Serikali kwa kitendo chake cha kushirikiana na familia ya Mtikila kwa hali na mali, bila kujadili kuwa ni mwanaharakati wa mabadiliko, jambo alilosisitiza kuwa hiyo ndio Tanzania inayotakiwa kwa sasa.
Makamu Mwenyekiti wa DP, Peter Mwagila alibainisha kuwa chama hicho kimepata pigo na pengo kubwa kwa kuondokewa na mwenyekiti wao, ambaye pia pamoja na kuwa muasisi wa chama hicho, ni mwanaharakati wa mageuzi aliyepigania nchi yake ya Tanganyika.
“Mtikila ndoto zake zilikuwa ni kurejeshwa kwa Tanganyika ambayo iliondolewa kwenye ramani ya dunia tangu mwaka 1962, alitaka kuwepo na Rais wa Tanganyika, Katiba, wabunge na mamlaka zote za nchi ya Tanganyika. Lakini pia alipinga rushwa, ufisaidi na kuwachukia viongozi wanaojilimbikizia mali,” alisema.
Alisema chama hicho kitahakikisha kinaendeleza na kusimamia harakati zote zilizoanzishwa na Mtikila ikiwemo kuidai Tanganyika. Msemaji wa familia ya mchungaji huyo, Peter Mayani, wakati akisoma wasifu wa Mtikila, alisema mwanaharakati huyo alibobea katika fani za sheria, uchumi na masoko na aliwahi kuajiriwa Mahakama Kuu na Shirika la Ndege la Afrika Mashariki, ambalo alilitumia kutoroshea wanaharakati wa chama cha Frelimo.
Alisema Mtikila aliokoka rasmi mwaka 1983 na kuanzisha Kanisa la Pentekoste la Full Salvation na mwaka 1990 alianza harakati za ukombozi, zilizoshinikiza kuanzishwa kwa vyama vingi mwaka 1992. Pia alianzisha chama cha DP, ambacho kilichelewa kupata usajili wake hadi mwaka 2000.
Mtikila baada ya kuagwa alisafirishwa kwenda kijijini kwao Milo, wilayani Ludewa mkoani Njombe ambako anatarajiwa kuzikwa leo. Marehemu ameacha mjane Georgia Mtikila. Askofu wa Kanisa la Ufunuo, Nabii Paul Bendera, aliwataka watanzania kutambua kuwa wote ni wageni duniani na kwamba kila mtu bila kujali ni nani duniani na ana cheo gani iko siku yake atakufa.
“Kwa sasa hali imekuwa ngumu na mbaya nawaomba ndugu zangu tuwe makini, lakini kubwa zaidi kila mtu amheshimu maisha ya mwenzake tuweke upendo na amani mbele na hii iwe ndio kipaumbele chetu. Naomba Serikali nayo iongeze juhudi za kuwalinda wananchi wake,” alisisitiza.
Mchungaji Daudi Mwaijojele, alitumia fursa hiyo kuwataka watanzania kuacha uchafu na kumrejea Mungu, ili kutengeneza maisha yao ya baadaye pindi watakapokufa. “Nawaomba acheni uchangudua, ufisadi na michepuko tena hiyo michepuko ndio inaleta magonjwa kama vile Ukimwi majumbwani na kusambaratisha familia,” alisema.
Mtikila alikufa kwa ajali ya gari aina ya Toyota Corolla, lenye namba za usajili T 189 AGM maeneo ya Msolwa wilayani Bagamoyo, mkoani Pwani. Alikuwa akitokea Njombe kwenda Dar es Salaam.
Monday, September 28, 2015
Marekan yaridhia Mabilioni
MCC Yaiondolea vikwazo Tanzania
![]() |
| Rais Jakaya M.Kikwete |
Habari hizo njema zilitangazwa juzi kwa Rais Jakaya Kikwete na Mtendaji Mkuu wa MCC, Dana J. Hyde katika mkutano uliofanyika katika Hoteli ya JW Marriot Essex House, New York, na kuhudhuriwa na watumishi waandamizi wa MCC akiwamo Kamran Khan, Makamu wa Rais wa Operesheni za MCC.
Rais Kikwete yuko New York kuhudhuria shughuli za mwaka huu za Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. “Hongera Mheshimiwa Rais kwa sababu nchi yako, Tanzania, imetimiza masharti yote ya kupata fedha nyingine chini ya mpango wa MCC - 2 ikiwa ni pamoja na uongozi wa MCC kuridhika kuwa Tanzania inachukua hatua za dhati kupambana na rushwa,” Hyde alimwambia Rais Kikwete na viongozi wengine wa Tanzania akiwamo Waziri wa Fedha wa Zanzibar, Yusuf Omar Mzee.
Hyde alimwambia Rais Kikwete kuwa Bodi ya MCC, katika mkutano wake wa Septemba 17, mwaka huu na chini ya Mwenyekiti wake, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, John Kerry, imeafiki kuhusu kipengele pekee kilichokuwa kimebakia katika masharti ya kupata fedha za MMC kuwa ni kweli Tanzania inakabiliana ipasavyo na rushwa na kuchukua hatua stahiki kukabiliana na tatizo hilo.
MCC ilitoa taarifa ya kuthibitisha kuwa Tanzania imetimiza masharti ya kuiwezesha kufaulu kupata raundi ya pili ya fedha za maendeleo na pia ilitoa taarifa ya kuthibitisha kuwa ni kweli Bodi ya MCC imeridhishwa na hatua zinazochukuliwa na Tanzania katika kukabiliana na rushwa.
Tofauti na fedha nyingi zinazotolewa na wafadhili wengi duniani, fedha za MCC hazitakiwi kurudishwa na nchi inayopewa fedha hizo na pia nchi husika hupewa uhuru wa kuchagua aina ya miradi ya maendeleo ambayo inaitaka igharimiwe na fedha hizo.
Miongoni mwa wajumbe wengine wa Bodi ya MCC ni Waziri wa Fedha wa Marekani ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Bodi, Mwakilishi wa Biashara wa Marekani duniani, Mwendeshaji Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID), nafasi ambayo kwa sasa anaikaimu Alfonsi Lenhardt, Mtendaji Mkuu wa MCC, Hyde na Rais wa Taasisi ya International Republican Institute (IRI), Balozi Mark Green.
Mabalozi Lenhardt na Green walikuwa mabalozi wa Marekani katika Tanzania wakati wa majadiliano, upitishaji na utekelezaji wa MCC–1. Hyde alisema sasa linalobakia ni kwa wajumbe wa Bodi kupelekewa muhtasari wa kuidhinisha mabilioni hayo kwa Tanzania ambayo chini ya mpango wa uwekezaji wa MCC–2 yatakwenda katika kuboresha huduma za umeme nchini Tanzania ikiwa ni pamoja na kusambaza umeme katika vijiji vingi zaidi.
Kiasi cha asilimia 46 ya Watanzania kwa sasa wanapata umeme kutoka asilimia 10 ya mwaka 2005 na sehemu kubwa ya asilimia hiyo imetokana na msaada wa MCC-1. Chini ya Mpango huo wa pili wa MCC, Tanzania itapatiwa Dola za Marekani milioni 472.8 (sawa na Sh bilioni 992.80).
Kwa kutilia maanani kiasi cha dola milioni 698 (sawa na Sh trilioni 1.46) ambazo zilitolewa chini ya MCC-1, Tanzania itakuwa imepata jumla ya dola za Marekani trilioni 2.45 za maendeleo kutoka Marekani katika kipindi cha miaka 10 tu iliyopita. Fedha za MCC-2 zitaanza kutolewa mwakani, 2016.
Kiasi kilichotolewa kwa Tanzania wakati wa MCC-1 ndicho kilikuwa kiasi kikubwa zaidi ambacho kimepata kutolewa na Marekani chini ya mpango huo, na kwa kupita MCC-2, Tanzania itakuwa ni nchi ambayo itakuwa imepata kiasi kikubwa cha fedha za maendeleo chini ya MCC duniani. Fedha zilizotolewa chini ya MCC -1 zilitumika kujenga Barabara za Tunduma-Sumbawanga, Tanga-Horohoro na Namtumbo-Songea- Mbinga.
Aidha, fedha hizo zilitumika kujenga upya mfumo wa huduma za maji kwa ajili ya miji ya Dar es Salaam na Morogoro na zilitumika kusambaza umeme katika vijiji vya mikoa 10 ya Tanzania Bara.
Fedha hizo vile vile zilitumika kutandaza njia ya pili ya kusafirisha umeme chini ya Bahari ya Hindi kati ya Tanzania Bara na Tanzania Visiwani na pia zilitumika kujenga barabara zote kuu za Kisiwa cha Pemba na baadhi ya barabara za Unguja kwa kiwango cha lami.
Friday, September 18, 2015
Mabasi Yaendayo Haraka kuanza kazi oktoba 2
HATIMAYE mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (BRT) katika jiji la Dar es Salaam unatarajiwa kuanza Oktoba 2 mwaka huu kwa njia moja.
Aidha, wamiliki wa magari, pikipiki na baiskeli ambao watakutwa wakitumia barabara ya mabasi ya haraka, kama maegesho watapewa adhabu kali ya faini au kifungo gerezani.
Hayo yalibainishwa jana na Ofisa wa Fidia wa Wakala wa Usafiri Haraka wa Mabasi (DART), Deo Mutasingwa baada ya wafanyakazi wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) kufanya ziara ya kujionea jinsi huduma hiyo itakavyotolewa.
Alisema huduma hiyo ambayo ni ya muda na kufanywa kwa kipindi cha miaka mwili, itakayofanywa na Kampuni ya UDA, itaanza Oktoba 2 mwaka huu kwanjia moja ya kutoka Kimara hadi Kivukoni yenye urefu wa kilomita 20.9.
Alisema kwa njia za barabara ya Msimbazi kutoka Faya hadi Kariakoo-Gerezani na sehemu ya barabara ya Kawawa kuanzia Magomeni hadi eneo la makutano ya Morocco jijini Dar es Salaam, itaanza kutumika baada ya miundombinu yake kukamilika.
Alisema katika mradi huo wa muda wa miaka miwili, mabasi 100 yatakayoendeshwa na madereva 200 yanatarajiwa kuwasili nchini wiki ijayo.
Aidha, Mutasingwa alisema wenye magari, pikipiki baiskeli ambao watakutwa wakitumia barabara hizo au kuegesha vyombo vyao watatozwa faini ya kati ya sh 250,000 hadi sh 300,000 au kifungo cha miaka miwili jela au adhabu zote kwa pamoja.
“ Tumekuwa na changamoto kwa watumiaji wengine wa barabara, jambo ambalo linaleta uharibifu na pia kuingilia safari. Tumeshazungumza na wenzetu wa halmashauri kushughulikia hili, hivyo kuanzia mwezi ujao atakayekutwa akitumia barabara hizo au kupaki chombo chake adhabu kali itakuwa juu yake,” alisema.
Alipoulizwa suala la nauli, alisema hilo liko kwenye mchakato kati ya DART, wamiliki wa mabasi na walaji lengo ni kuja na nauli ambayo haitamuumiza mwananchi lakini pia yule anayeendesha apate faida.
Alisema wakati utoaji wa huduma hiyo utakapokuwa kamili, watanzania takribani 300,000 watahudumiwa kwa siku.
Msimamizi wa Mifumo wa DART, Junn Mlingi alisema vituo vikuu vya mabasi vitakuwa na miundombinu ya kumwezesha mtumiaji yeyote kama ni mgeni, mlemavu wa viungo kuona au kusikia kuweza kupata huduma hiyokwani kutakuwa na matangazo ya sauti na maandishi.
Alisema mabasi hayo yatakuwa yakiendeshwa kwa kilomita 50 kwa saa kwa mwendo wa kasi na kilomita 24 kwa saa kwa mwendo wa wastani.“
Tuesday, September 08, 2015
Dk John Magufuli jinsi alivyoshambulia jukwaa Morogoro
MGOMBEA Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha
Mapinduzi (CCM), Dk John Magufuli, amesema Serikali atakayoiongoza
itajenga viwanda vikubwa, vya kati na vidogo ili kuongeza ajira na
mapato ya Serikali, huku akiwaahidi wakazi wa Morogoro kufufua viwanda
vyao.
Amesema hayo katika Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro katika moja ya mikutano mikubwa ya kampeni za uchaguzi, uliorushwa moja kwa moja na televisheni mbalimbali nchini.
Akizungumza katika mkutano huo, Dk Magufuli alisema mbali na kujenga viwanda, pia Serikali hiyo itatoa Sh milioni 50 kwa kila mtaa na kijiji kwa ajili ya wanawake na vijana kukuza mitaji yao ya biashara na kuanzisha biashara mpya, huku akiwahakikishia kutobughudhiwa.
Kuhusu elimu na afya, Dk Magufuli alisema kuanzia mwakani wanafunzi kutoka darasa la awali mpaka kidato cha nne, hawatalipa ada ya shule kwa kuwa Serikali atakayoiongoza itatoa huduma hiyo bure. Pia, alisema atashusha bei ya vifaa vya ujenzi ili wananchi wanaofanya kazi na biashara na kujipatia kipato halali, wajenge nyumba kwa gharama nafuu.
Kabla ya Dk Magufuli kuhutubia, Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete alipanda jukwaani na kusema akistaafu kwa kumkabidhi nchi Dk Magufuli, atalala usingizi.
Rais Kikwete alisema hakwenda mkoani huko kuhudhuria mikutano ya Dk Magufuli, bali alikwenda kuhudhuria kikao cha mkakati cha Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), kilichofanyika mkoani humo.
Kwa mujibu wa Rais Kikwete, kwa kuwa mgombea huyo alikuwa na ratiba ya kuhutubia mkutano katika uwanja huo, akaona ni vyema na yeye ahudhurie mkutano huo.
Alipopewa nafasi ya kumkaribisha mgombea huyo, Rais Kikwete alitumia fursa hiyo kuzungumza kidogo kilichofanyika Dodoma, wakati wa mchakato wa kumpata mgombea urais wa chama hicho.
Alisema walitumia muda mrefu kujadili kila mgombea kati ya wagombea 38 waliojitokeza kuwania nafasi hiyo, mpaka wakapata wagombea watano akiwemo Dk Magufuli, Balozi Amina Salum Ali, Dk Asha-Rose Migiro, Bernard Membe na January Makamba.
Baada ya hapo, alisema walikwenda katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM ambako wafuasi wa mmoja wa wagombea ambaye hakuingia katika tano bora, Edward Lowassa, walipewa nafasi kubwa ya kuzungumza baada ya mgombea huyo kutopenya tano bora.
Kwa mujibu wa Kikwete, walizungumza yote na sababu ya kupata wagombea hao na sifa zao dhidi ya za wenzao na wakaafikiana na kupiga kura, ambapo Lowassa ambaye baadaye alitoka na kuhamia Chadema, alipiga kura.
Baada ya hapo walipatikana watatu, Magufuli, Balozi Amina na Dk Migiro ambapo katika Mkutano Mkuu, alipita Magufuli ambaye alisema ana kila sifa ya kuwa rais na kuongeza kuwa wananchi walisema yeye Kikwete ni mpole, hivyo baada ya kupata rais mpole, Tanzania inahitaji rais mkali.
Rais Kikwete alisema kampeni zinavyokwenda, anaona baada ya Uchaguzi Mkuu vyama vya upinzani vilivyojiunga katika mwavuli wa Ukawa, vitageuka jina na kuwa Ukiwa
Amesema hayo katika Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro katika moja ya mikutano mikubwa ya kampeni za uchaguzi, uliorushwa moja kwa moja na televisheni mbalimbali nchini.
Akizungumza katika mkutano huo, Dk Magufuli alisema mbali na kujenga viwanda, pia Serikali hiyo itatoa Sh milioni 50 kwa kila mtaa na kijiji kwa ajili ya wanawake na vijana kukuza mitaji yao ya biashara na kuanzisha biashara mpya, huku akiwahakikishia kutobughudhiwa.
Kuhusu elimu na afya, Dk Magufuli alisema kuanzia mwakani wanafunzi kutoka darasa la awali mpaka kidato cha nne, hawatalipa ada ya shule kwa kuwa Serikali atakayoiongoza itatoa huduma hiyo bure. Pia, alisema atashusha bei ya vifaa vya ujenzi ili wananchi wanaofanya kazi na biashara na kujipatia kipato halali, wajenge nyumba kwa gharama nafuu.
Kabla ya Dk Magufuli kuhutubia, Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete alipanda jukwaani na kusema akistaafu kwa kumkabidhi nchi Dk Magufuli, atalala usingizi.
Rais Kikwete alisema hakwenda mkoani huko kuhudhuria mikutano ya Dk Magufuli, bali alikwenda kuhudhuria kikao cha mkakati cha Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), kilichofanyika mkoani humo.
Kwa mujibu wa Rais Kikwete, kwa kuwa mgombea huyo alikuwa na ratiba ya kuhutubia mkutano katika uwanja huo, akaona ni vyema na yeye ahudhurie mkutano huo.
Alipopewa nafasi ya kumkaribisha mgombea huyo, Rais Kikwete alitumia fursa hiyo kuzungumza kidogo kilichofanyika Dodoma, wakati wa mchakato wa kumpata mgombea urais wa chama hicho.
Alisema walitumia muda mrefu kujadili kila mgombea kati ya wagombea 38 waliojitokeza kuwania nafasi hiyo, mpaka wakapata wagombea watano akiwemo Dk Magufuli, Balozi Amina Salum Ali, Dk Asha-Rose Migiro, Bernard Membe na January Makamba.
Baada ya hapo, alisema walikwenda katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM ambako wafuasi wa mmoja wa wagombea ambaye hakuingia katika tano bora, Edward Lowassa, walipewa nafasi kubwa ya kuzungumza baada ya mgombea huyo kutopenya tano bora.
Kwa mujibu wa Kikwete, walizungumza yote na sababu ya kupata wagombea hao na sifa zao dhidi ya za wenzao na wakaafikiana na kupiga kura, ambapo Lowassa ambaye baadaye alitoka na kuhamia Chadema, alipiga kura.
Baada ya hapo walipatikana watatu, Magufuli, Balozi Amina na Dk Migiro ambapo katika Mkutano Mkuu, alipita Magufuli ambaye alisema ana kila sifa ya kuwa rais na kuongeza kuwa wananchi walisema yeye Kikwete ni mpole, hivyo baada ya kupata rais mpole, Tanzania inahitaji rais mkali.
Rais Kikwete alisema kampeni zinavyokwenda, anaona baada ya Uchaguzi Mkuu vyama vya upinzani vilivyojiunga katika mwavuli wa Ukawa, vitageuka jina na kuwa Ukiwa
Flaviana Matata ateuliwa kuwa Balozi wa hiyari wa Utalii nchini Marekani

Mwanamitindo wa Kimataifa anaefanyia kazi zake za nchini Marekani Flaviana Matata amechagulia na
Wizara ya Maliasili kuwa Balozi wa Hiyari ‘Good Will Ambassador’ kwa kipindi cha miaka mitatu kwa dhumuni la kutangaza vivutio vya utalii vya Tanzania ndani na nje ya nchi.
Flaviana ambaye juzi alikuwa mmoja kati ya shuhuda wa kushuhudia wizara ya maliasili na utalii wakizindua rasmi tangazo litakalokuwa linatangaza vivutio vya Tanzania nje ya anchi alitawazwa leo hii na katibu mkuu Dr Adelhelm James Meru aliyemkabidhi kwa niaba ya Waziri , Mheshimiwa Lazaro Nyalandu huku Kaimu Mkurugenzi Madam Devota Mdachi akishuhudia
Monday, August 31, 2015
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa akimnadi Mgombea Ubunge wa Jimbo la Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa wakati wa Mkutano wa Kampeni,
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akiwahutubia maelfu ya wananchi wa Iringa Mjini waliofurika kwenye Uwanja wa Sabasaba Gangilonga, Agosti 30, 2015. Katika Hotuba yake Mh. Lowassa alizungumzia namna atakavyotoa kipaumbele kwa wakulima ambapo amesema atafuta ushuru wa mazao kwa wakulima na kufuta kodi kwa vifaa vya michezo na burudani ili vijana waweze kunufaika na vipaji vyao
CHAMA cha ACT Wazalendo kimezindua kampeni zake jijini Dar es Salaam
CHAMA cha ACT Wazalendo kimezindua kampeni zake jijini Dar es Salaam

CHAMA cha ACT Wazalendo kimezindua kampeni zake jijini Dar es Salaam kwa kuahidi kitakapopewa ridhaa ya kuongoza nchi, kitaunda serikali ya Umoja wa Kitaifa. Aidha katika uzinduzi huo ambao viongozi mbalimbali wa chama hicho walihutubia, Mgombea Urais wa chama hicho Anna Mghwira alisema wananchi wakimpa ridhaa, waziri mkuu wake atakuwa Zitto Kabwe.
“Nitakapounda serikali, katika katiba, mtu wa kwanza kusaidiana na
rais licha ya makamu, ni Zitto Kabwe, atakuwa Waziri Mkuu katika
serikali ya kwanza,” alisema Anna Mghwira ambaye pia alisema atahusisha
viongozi waadilifu kutoka CCM, Chadema na vyama vyote vya siasa na
taasisi zote kiraia.
Akihutubia mkutano huo uliofanyika viwanja vya Mbagala Zakhem,
mgombea huyo, katika kuelekeza nia yake ya kuunda serikali hiyo ya
umoja, alisema linapokuja suala la kitaifa, hakuna haja ya kuangalia
masuala ya itikadi. “Mimi ni mama, hukusanya watoto wake.
Hata mama wa vifaranga hukusanya vifaranga pamoja na kuviweka kwenye mbawa zake…mimi nina mbawa za moyo…nitaunda serikali ya umoja wa kitaifa itakayotokana na sekta binafsi lakini kutoka watu wazalendo, wenye utu, waadilifu, taasisi za kijamii, mashirika ya kidini, makundi ya umma ili kuunda taswira ya nchi yetu.”
Mghwira alisema taifa linahitaji mabadiliko si ya tu kifikra na kisera, bali pia ya kijinsia kwa kumchagua yeye kuwa Rais wa nchi. Alisema chama chake kinatilia mkazo utu, uzalendo na uadilifu.
Makao makuu Dodoma Aidha alisema, Serikali itakapoundwa itaapishwa Dodoma na watahakikisha wanarudisha kazi kubwa aliyoifanya Rais wa Kwanza, Julius Nyerere ya kuifanya Dodoma kuwa makao makuu ya nchi na serikali lakini siyo makao makuu ya chama.
Alisema kuweka mji huo makao makuu, maana yake ni kuleta watu wote
kutoka pande zote za nchi. Vipaumbele Alitaja vipaumbele vyake ni kuwa
na mfumo imara na endelevu wa hifadhi ya jamii unaojengea uwezo wananchi
kukabiliana na majanga. Alisema asilimia sita pekee ya Watanzania
wanafaidika.
“Tutatumia hifadhi ya jamii kama nyenzo ya kukuza akiba nchini ili kuwe na vyanzo vya mitaji ya uwekezaji wa ndani…tutapanua hifadhi ya jamii kufikia makundi yote katika jamii ikiwamo wakulima, wafugaji, mama lishe na bodaboda,” alisema. Kipaumbele kingine alichoahidi ni uchumi shirikishi wenye kuzalisha ajira nyingi na bora.
Alisema watu wengi hawana uhakika na maisha yao kimapato. Aidha alisema, watajikita kwenye uwekezaji wa kilimo na kusimamia uzalishaji wake. Aidha, aliahidi kuhakikisha ardhi na mashamba yote yaliyo chini ya mashirika ya umma, yanachukuliwa na kuwekwa chini ya uzalishaji mdogo.
Kwa upande wa viwanda, alisema atahakikisha bidhaa zinazozalishwa nchini zinaongeza mapato ya fedha za kigeni. Chama hicho kupitia kwa mgombea, kimesema kitaweka msukumo kwenye bidhaa za nguo na vitakuwapo viwanda vya kuongeza thamani ya mazao ya kilimo na mifugo.
Vipaumbele vingine ni kuhakikisha madini, mafuta na gesi, vinakuwa mali ya wananchi kikatiba. Kuhusu Katiba Mpya, alisema wataruhusu Tume ya Jaji Warioba imalize kazi ya katiba ilikoishia. Mgombea huyo aliendelea kutaja vipambele vyake kuhakikisha anaboresha huduma za afya ikiwamo kudhibiti vifo vya mama na mtoto.
Aliahidi kuondoa tatizo la watoto wa mitaani. Misamaha ya kodi kwa mujibu wake, haitazidi asilimia moja ya pato la taifa na wakati huo huo atadhibiti mianya ya ukwepaji kodi hususani kwa kampuni za kigeni.
Sifa za rais Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Kitila Mkumbo, alishauri wananchi kuangalia wagombea urais kama wanalinda haki za walio wengi au ni mateka wa matajiri. Mkumbo alisema, kiongozi mkuu wa nchi, kwa maana ya rais, ana kazi kuu nne ambazo ni fikra na kutoa dira ya nchi jambo ambalo anapaswa kuwa na uwezo wa kufikiri.
“Tatizo ni kufikiri na kutoa dira ya nchi…tunataka rais atakayetoa misingi ya nchi, atatuletea sera..,” alisema Kitila. Alisema kazi ya pili ya rais, ni kuwa mlinzi mkuu wa tunu za taifa huku akisisitiza katika tunu ya umoja, wananchi kuepuka mgombea mwenye tabia za kidini, kikabila na kikanda.
“Rais ndiye mlinzi wa usawa katika taifa…,” alisema na kushauri wananchi kuangalia wanaogombea kama wanaelekea kulinda haki za walio wengi au ni mateka wa matajiri. Alitaja tunu nyingine ni muungano kwa kusema anayeomba urais na kutaka kucheza na muungano lazima akataliwe.
Kuhusu uadilifu, alisema inapaswa aingie rais atakayekoleza vita ya ufisadi . “Kama kuna mtu anataka urais hata kutamka neno ufisadi anaogopa, huyu hatufai hata kidogo,” alisema Kitila.
Akizungumzia demokrasia, alisema nchi imepiga hatua katika demokrasia ambayo inahitaji rais atakayeipeleka mbele. Vile vile alisema katika kuchagua, ni lazima kuangalia mgombea ndani ya chama chake alipatikanaje.
“Kazi nyingine ya rais lazima awe mfano wa binadamu bora katika jamii. Hatumaanishi malaika, tunamaanisha kwamba popote atakapoenda, akisimama wajue huyu ni Mtanzania, awe sura ya utaifa,” alisema na kusisitiza sifa nyingine ya rais itokane na uadilifu wa chama chake.
Kitila alisisitiza, “Mtu asiye mlaghai lazima aliyotuambia jana, na leo yafanane. Akihubiri maji lakini yeye anakunywa wiski, yeye ni mlaghai. Akituambia ni nyeusi jana, leo nyekundu, kesho nyeupe, huyo ni mlaghai.” Alisisitiza kuwa ACT Wazalendo inazingatia misingi na sera huku akibeza vyama vingine kwamba vinauza mbwembwe na ulaghai.
Ukawa wasutwa Kwa upande wake, Meneja wa Kampeni, Habib Mchange, aliisuta Chadema na CUF kupitia viongozi wao akirejea mkutano wa Mwembe Yanga mwaka 2007, walipotaja orodha ya waliowatuhumu kuwa mafisadi papa. “Kipindi kile hawakuwa na Ukawa bali walikuwa na ushirikiano.
Walitaja watu wanaofilisi taifa hili ambao ni watu kumi na moja…kati ya watu hao waliotajwa kuwa ni mafisadi, namba tisa alikuwa ni Lowassa,” alisema Mchange. “Tulikubaliana 2007 kwamba tunapambana na CCM na wana mafisadi. Leo naomba mtafakari…ili tusiwe wajanja wajanja lazima tuseme ukweli.
Unayosema jana ndo hayohayo uyaseme leo,” alisema. Akinyoshea CCM pia vidole, Mchange alilinganisha mgombea wa Ukawa sawa na chupa yenye sumu iliyobandikwa jina la maji. Alinadi chama chake akisisitiza wananchi wakiamini kwa kuwa kimekuja katikati ya sumu mbili za CCM na Ukawa.
Amshangaa Sumaye, Lowassa Mchange alisema anachoona ni kwamba, ufisadi uliokuwa CCM, umezaliana na kutanuka na hatimaye kuhamia Ukawa. “Jana (juzi) Sumaye ametulaghai… Anasema anashangaa kwa nini CCM inaendelea kuaminiwa,” alisema.
Alikumbusha kuhusu mjadala wa kununua ndege ya rais ambayo ilipigiwa kelele, kwamba wakati huo Sumaye ndiye alikuwa Waziri Mkuu. Pia kuhusu ahadi ya Lowassa ya kumwachia huru mwanamuziki Nguza Viking maarufu kama Babu Seya, Mchange alieleza kushangazwa naye kutokana na kile alichosema, wakati anafungwa, ndiye alikuwa Waziri Mkuu.
Mchange alikuwa mkali zaidi katika hotuba yake hasa alipokuwa anazungumzia ufisadi na wizi. “ Kumbe unaruhusiwa kuwaibia Watanzania ukiwa CCM ukirudi upinzani ni msafi. Mwizi ni mwizi tu.
Fisadi ni fisadi tu…Wanatudanganya kwamba kuna Ukawa…waongo. Ukawa wanatafuta rais tu. Ukawa huku chini kwa wapiga kura haupo,” alisema Mchange. Alihoji ni namna gani mgombea urais ataweza kunadi wagombea wa vyama vinavyounda Ukawa ambao wamegoma kuachiana majimbo hususani Jimbo la Tabora Mjini, Serengeti na Segerea.
“Sasa tuwaulize Ukawa Lowassa akipita Tabora mjini atamnadi nani?,” alisema akimaanisha mgombea wa CUF na Chadema wanaogombea jimbo hilo. Zitto Kabwe Alisema ACT Wazalendo wanarejesha miiko ya uongozi.
Alisisitiza kuhusu utaratibu wa chama chake wa kiongozi kutangaza mali na madeni yake. Zitto alisema kila chama kinachogombea, kinasema kitapambana na rushwa na ufisadi bila kueleza ni namna gani watapambana tofauti na ACT Wazalendo ambacho kimesema kitapambana kwa kurejesha miiko ya uongozi.
Alihoji ni namna gani mawaziri wakuu wastaafu wanatamba kuleta mabadiliko. Zitto alimsuta Sumaye akisema, wakati ATCL inauzwa aliyekuwa Waziri Mkuu ni Sumaye na wakati huo huo na mwaka 2007 ilipotaka kufufuliwa wakapewa Wachina ambao walisababisha hasara kwa taifa aliyekuwa Waziri Mkuu alikuwa Lowassa.
Zitto alikosoa pia kauli ya Magufuli juu ya ahadi yake ya kuanzisha mahakama ya kupambana na rushwa, akisema kwenye katiba mpya, kulikuwa na kipengele cha kuipa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mamlaka ya kukamata na kushitaki wala rushwa lakini CCM waliikataa.
Kuhusu ufisadi, Zitto alisema hakuna chama cha siasa chenye uwezo wa kupambana nao isipokuwa ACT Wazalendo. Akitumia kete ya jinsi kumnadi mgombea, Zitto alisema, ni wakati wa Watanzania kumpa mwanamke uongozi wa nchi ikizingatiwa miaka yote, imekuwa ikiongozwa na wanaume.

| Mwana muziki Bwana misosi, akitoa burudani katika uzinduzi wa kampeni wa Chama cha ACT-Wazalendo uliofanyika viwanja vya Zakhem Mbagala Dar es Salaam jana. |
| Mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Anna Mghwira akihutubia katika uzinduzi wa kampeni ya chama hizo uliofanyika viwanja vya Zakhem Mbagala jijini Dar es Salaam jana. |
| Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Kabwe Zitto, akigawa ilani ya chama hicho kwa mgombea urais na mwenza wake |
| Mshauri wa Chama cha ACT-Wazalendo, Profesa Kitila Mkumbo akihutubia kwenye uzinduzi huo. |
CHAMA cha ACT Wazalendo kimezindua kampeni zake jijini Dar es Salaam kwa kuahidi kitakapopewa ridhaa ya kuongoza nchi, kitaunda serikali ya Umoja wa Kitaifa. Aidha katika uzinduzi huo ambao viongozi mbalimbali wa chama hicho walihutubia, Mgombea Urais wa chama hicho Anna Mghwira alisema wananchi wakimpa ridhaa, waziri mkuu wake atakuwa Zitto Kabwe.
Hata mama wa vifaranga hukusanya vifaranga pamoja na kuviweka kwenye mbawa zake…mimi nina mbawa za moyo…nitaunda serikali ya umoja wa kitaifa itakayotokana na sekta binafsi lakini kutoka watu wazalendo, wenye utu, waadilifu, taasisi za kijamii, mashirika ya kidini, makundi ya umma ili kuunda taswira ya nchi yetu.”
Mghwira alisema taifa linahitaji mabadiliko si ya tu kifikra na kisera, bali pia ya kijinsia kwa kumchagua yeye kuwa Rais wa nchi. Alisema chama chake kinatilia mkazo utu, uzalendo na uadilifu.
Makao makuu Dodoma Aidha alisema, Serikali itakapoundwa itaapishwa Dodoma na watahakikisha wanarudisha kazi kubwa aliyoifanya Rais wa Kwanza, Julius Nyerere ya kuifanya Dodoma kuwa makao makuu ya nchi na serikali lakini siyo makao makuu ya chama.
“Tutatumia hifadhi ya jamii kama nyenzo ya kukuza akiba nchini ili kuwe na vyanzo vya mitaji ya uwekezaji wa ndani…tutapanua hifadhi ya jamii kufikia makundi yote katika jamii ikiwamo wakulima, wafugaji, mama lishe na bodaboda,” alisema. Kipaumbele kingine alichoahidi ni uchumi shirikishi wenye kuzalisha ajira nyingi na bora.
Alisema watu wengi hawana uhakika na maisha yao kimapato. Aidha alisema, watajikita kwenye uwekezaji wa kilimo na kusimamia uzalishaji wake. Aidha, aliahidi kuhakikisha ardhi na mashamba yote yaliyo chini ya mashirika ya umma, yanachukuliwa na kuwekwa chini ya uzalishaji mdogo.
Kwa upande wa viwanda, alisema atahakikisha bidhaa zinazozalishwa nchini zinaongeza mapato ya fedha za kigeni. Chama hicho kupitia kwa mgombea, kimesema kitaweka msukumo kwenye bidhaa za nguo na vitakuwapo viwanda vya kuongeza thamani ya mazao ya kilimo na mifugo.
Vipaumbele vingine ni kuhakikisha madini, mafuta na gesi, vinakuwa mali ya wananchi kikatiba. Kuhusu Katiba Mpya, alisema wataruhusu Tume ya Jaji Warioba imalize kazi ya katiba ilikoishia. Mgombea huyo aliendelea kutaja vipambele vyake kuhakikisha anaboresha huduma za afya ikiwamo kudhibiti vifo vya mama na mtoto.
Aliahidi kuondoa tatizo la watoto wa mitaani. Misamaha ya kodi kwa mujibu wake, haitazidi asilimia moja ya pato la taifa na wakati huo huo atadhibiti mianya ya ukwepaji kodi hususani kwa kampuni za kigeni.
Sifa za rais Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Kitila Mkumbo, alishauri wananchi kuangalia wagombea urais kama wanalinda haki za walio wengi au ni mateka wa matajiri. Mkumbo alisema, kiongozi mkuu wa nchi, kwa maana ya rais, ana kazi kuu nne ambazo ni fikra na kutoa dira ya nchi jambo ambalo anapaswa kuwa na uwezo wa kufikiri.
“Tatizo ni kufikiri na kutoa dira ya nchi…tunataka rais atakayetoa misingi ya nchi, atatuletea sera..,” alisema Kitila. Alisema kazi ya pili ya rais, ni kuwa mlinzi mkuu wa tunu za taifa huku akisisitiza katika tunu ya umoja, wananchi kuepuka mgombea mwenye tabia za kidini, kikabila na kikanda.
“Rais ndiye mlinzi wa usawa katika taifa…,” alisema na kushauri wananchi kuangalia wanaogombea kama wanaelekea kulinda haki za walio wengi au ni mateka wa matajiri. Alitaja tunu nyingine ni muungano kwa kusema anayeomba urais na kutaka kucheza na muungano lazima akataliwe.
Kuhusu uadilifu, alisema inapaswa aingie rais atakayekoleza vita ya ufisadi . “Kama kuna mtu anataka urais hata kutamka neno ufisadi anaogopa, huyu hatufai hata kidogo,” alisema Kitila.
Akizungumzia demokrasia, alisema nchi imepiga hatua katika demokrasia ambayo inahitaji rais atakayeipeleka mbele. Vile vile alisema katika kuchagua, ni lazima kuangalia mgombea ndani ya chama chake alipatikanaje.
“Kazi nyingine ya rais lazima awe mfano wa binadamu bora katika jamii. Hatumaanishi malaika, tunamaanisha kwamba popote atakapoenda, akisimama wajue huyu ni Mtanzania, awe sura ya utaifa,” alisema na kusisitiza sifa nyingine ya rais itokane na uadilifu wa chama chake.
Kitila alisisitiza, “Mtu asiye mlaghai lazima aliyotuambia jana, na leo yafanane. Akihubiri maji lakini yeye anakunywa wiski, yeye ni mlaghai. Akituambia ni nyeusi jana, leo nyekundu, kesho nyeupe, huyo ni mlaghai.” Alisisitiza kuwa ACT Wazalendo inazingatia misingi na sera huku akibeza vyama vingine kwamba vinauza mbwembwe na ulaghai.
Ukawa wasutwa Kwa upande wake, Meneja wa Kampeni, Habib Mchange, aliisuta Chadema na CUF kupitia viongozi wao akirejea mkutano wa Mwembe Yanga mwaka 2007, walipotaja orodha ya waliowatuhumu kuwa mafisadi papa. “Kipindi kile hawakuwa na Ukawa bali walikuwa na ushirikiano.
Walitaja watu wanaofilisi taifa hili ambao ni watu kumi na moja…kati ya watu hao waliotajwa kuwa ni mafisadi, namba tisa alikuwa ni Lowassa,” alisema Mchange. “Tulikubaliana 2007 kwamba tunapambana na CCM na wana mafisadi. Leo naomba mtafakari…ili tusiwe wajanja wajanja lazima tuseme ukweli.
Unayosema jana ndo hayohayo uyaseme leo,” alisema. Akinyoshea CCM pia vidole, Mchange alilinganisha mgombea wa Ukawa sawa na chupa yenye sumu iliyobandikwa jina la maji. Alinadi chama chake akisisitiza wananchi wakiamini kwa kuwa kimekuja katikati ya sumu mbili za CCM na Ukawa.
Amshangaa Sumaye, Lowassa Mchange alisema anachoona ni kwamba, ufisadi uliokuwa CCM, umezaliana na kutanuka na hatimaye kuhamia Ukawa. “Jana (juzi) Sumaye ametulaghai… Anasema anashangaa kwa nini CCM inaendelea kuaminiwa,” alisema.
Alikumbusha kuhusu mjadala wa kununua ndege ya rais ambayo ilipigiwa kelele, kwamba wakati huo Sumaye ndiye alikuwa Waziri Mkuu. Pia kuhusu ahadi ya Lowassa ya kumwachia huru mwanamuziki Nguza Viking maarufu kama Babu Seya, Mchange alieleza kushangazwa naye kutokana na kile alichosema, wakati anafungwa, ndiye alikuwa Waziri Mkuu.
Mchange alikuwa mkali zaidi katika hotuba yake hasa alipokuwa anazungumzia ufisadi na wizi. “ Kumbe unaruhusiwa kuwaibia Watanzania ukiwa CCM ukirudi upinzani ni msafi. Mwizi ni mwizi tu.
Fisadi ni fisadi tu…Wanatudanganya kwamba kuna Ukawa…waongo. Ukawa wanatafuta rais tu. Ukawa huku chini kwa wapiga kura haupo,” alisema Mchange. Alihoji ni namna gani mgombea urais ataweza kunadi wagombea wa vyama vinavyounda Ukawa ambao wamegoma kuachiana majimbo hususani Jimbo la Tabora Mjini, Serengeti na Segerea.
“Sasa tuwaulize Ukawa Lowassa akipita Tabora mjini atamnadi nani?,” alisema akimaanisha mgombea wa CUF na Chadema wanaogombea jimbo hilo. Zitto Kabwe Alisema ACT Wazalendo wanarejesha miiko ya uongozi.
Alisisitiza kuhusu utaratibu wa chama chake wa kiongozi kutangaza mali na madeni yake. Zitto alisema kila chama kinachogombea, kinasema kitapambana na rushwa na ufisadi bila kueleza ni namna gani watapambana tofauti na ACT Wazalendo ambacho kimesema kitapambana kwa kurejesha miiko ya uongozi.
Alihoji ni namna gani mawaziri wakuu wastaafu wanatamba kuleta mabadiliko. Zitto alimsuta Sumaye akisema, wakati ATCL inauzwa aliyekuwa Waziri Mkuu ni Sumaye na wakati huo huo na mwaka 2007 ilipotaka kufufuliwa wakapewa Wachina ambao walisababisha hasara kwa taifa aliyekuwa Waziri Mkuu alikuwa Lowassa.
Zitto alikosoa pia kauli ya Magufuli juu ya ahadi yake ya kuanzisha mahakama ya kupambana na rushwa, akisema kwenye katiba mpya, kulikuwa na kipengele cha kuipa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mamlaka ya kukamata na kushitaki wala rushwa lakini CCM waliikataa.
Kuhusu ufisadi, Zitto alisema hakuna chama cha siasa chenye uwezo wa kupambana nao isipokuwa ACT Wazalendo. Akitumia kete ya jinsi kumnadi mgombea, Zitto alisema, ni wakati wa Watanzania kumpa mwanamke uongozi wa nchi ikizingatiwa miaka yote, imekuwa ikiongozwa na wanaume.
Thursday, August 27, 2015
Lionel Messi named UEFA Best Player in Europe
Lionel Messi named UEFA Best Player in Europe over Cristiano Ronaldo Lionel Messi was named the UEFA Best Player in Europe for the 2014-15 season for helping Barcelona to a Treble of trophies. The Argentine star defeated the other finalists, his Barcelona teammate Luis Suarez and Real Madrid's Cristiano Ronaldo, who won the award a year ago, after a live vote of journalists. Messi received the accolade after Thursday's Champions League group stage draw was made, as the holders were placed against Bayer Leverkusen, Roma and BATE Borisov. The four-time FIFA world player of the year scored 58 goals in all competitions while leading Barcelona to titles in La Liga, the Copa del Rey and the Champions League. Ronaldo scored 61 goals, but Real Madrid failed to win any major trophies. Suarez, who scored the decisive second goal in the 3-1 final win over Juventus, reached the shortlist despite starting his season in late-October. The Uruguay forward served a FIFA ban for biting at the 2014 World Cup. Messi's contribution to Barca's Champions League-winning campaign was recognised, with Messi having finished as joint top-scorer in the competition with 10 goals -- alongside Ronaldo and a third Barca attacker in Neymar. Asked for the secret behind his excellent 2014-15 campaign, the 28- year-old said he was only able to win individual awards because of the support given by his teammates and the wider Blaugrana family. "This prize brings me a lot of joy," Messi said. "It was an incredible year for us. I don't know about secrets, but there is a united dressing room which was able to have an incredible year. "It came out as we wanted, and we achieved our objectives. I want to thank all my teammates. We all represent something. If not for all of them, not Barca, nor I, would be here." Messi last won the award in 2011, the first year that Europe's governing body awarded the honour. Since then Barca's Andres Iniesta, Bayern Munich's Franck Ribery and Ronaldo have been the winners. Earlier in the day, Messi's solo goal against Bayern Munich in last year's Champions League semifinal first leg was voted last year's competition's best goal by users on UEFA's website, winning with 39 percent of the vote. "I only found out about the best goal prize when I arrived here," Messi said. "I did not know anything. Without my teammates I would not be here." Frankfurt forward Celia Sasic won the UEFA Best Women's Player in Europe award. Sasic, who led the Women's Champions League in scoring last season and recently retired, beat Dzsenifer Marozsan and Amandine Henry to land the award.
Monday, August 17, 2015
Zitto aongoza wagombea ubunge ACT-Wazalendo
CHAMA cha ACT Maendeleo kimetoa rasmi majina ya wagombea wake watakaokiwakilisha chama hicho, katika nafasi za ubunge na uwakilishi kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu, huku Kiongozi Mkuu wa chama hicho, Kabwe Zitto akiwania ubunge jimbo la Kigoma mjini.
Kwa mujibu wa taarifa ya chama hicho kwa vyombo vya habaeri, pamoja na Zitto pia kimewateua wabunge wengine waliokuwemo kwenye Bunge lililopita ambao ni Moses Machali, anayewania jimbo la Kasulu Mjini, Anna Mallack Mpanda vijijini na Chiku Abwao Iringa Mjini.
Machali katika Bunge lililopita alikuwa mbunge wa Kasulu mjini kupitia NCCR-Mageuzi wakati Mallack na Abwao walikuwa wabunge wa viti maalum kupitia Chadema, wabunge wote hao wamehama vyama hivyo na kujiunga na chama hicho cha ACT.
Wagombea wengine waliopitishwa na chama hicho kukiwakilisha katika nafasi ya ubunge ni Eva Kaka (Bahi), Christina Kamunya (Dodoma Mjini), Said Njuki (Kondoa), Demi Mchuki (Kondoa Mjini) na Fataha Ibrahim (Kondoa Kusini).
Baadhi ya wagombea wengine ni Maulid Mataka (Kongwa), Batulo Ibrahim (Arumeru Mashariki), Estomih Mallah (Arusha Mjini), Alex Kisanga (Karatu), Ojung Saitabau (Arumeru Magharibi), Geovan Meleki (Rombo), Fadhili Fadhili (Mwanga) na Lilian Mduma (Same Magharibi).
Aidha chama hicho pia kimemteua Hassan Rashid kuwania jimbo la Same Mashariki, Goodluck Mollel (Moshi Vijijini), Nuru Mohammed (Hai), Buni Ramole (Moshi Mjini), Msumba Mngumi (Mlalo), Ally Tendeza (Mkinga), Mikidadi Hamisi (Bumbuli) na Zaina Bongi (Korogwe Vijijini).
Katika jimbo la Korogwe Mjini chama hicho kimemteua Mohammed Mwalimu kuwania nafasi hiyo, Zuberi Ngoda (Muheza), Ahmad Kidege (Tanga Mjini), Bakari Mrisho (Handeni Vijijini), Ramadhani Mwalekwa (Handeni Vijijini), Charles Mtuu (Handeni Mjini) na Onesmo Mwakyombo (Mikumi).
Jimbo la Morogoro Kusini chama hicho kimemteua Hamimu Muhongo kuwania nafasi hiyo, Jafari Chamkua (Morogoro Kusini Mashariki), Isaya Maputa (Ulanga Mashariki), Selemani Msindi (Morogoro Mjini), Athuman Adam (Mvomero) na Hidaya Sanga (Malinyi).
Wengine ni Mwinyi Madega (Gairo), Hassan Mbaruku (Kilosa Kati), Saidi Saidi (Bagamoyo), Gasper Shoo (Chalinze), Rose Mkonyi (Kibaha Vijijini), Mohammed Massaga (Kisarawe), Kunje Ngombale-Mwiru (Mkuranga), Habibu Amiri (Rufiji) na Ahmad Kigomba (Mafia).
Wagombea wengine wa chama hicho walioteuliwa ni Habibu Mchange (Kibaha Mjini), Janeth Rite (Kawe), Dickson Nghilly (Kibamba), Mohammed Mwikongi (Segerea), Ally Shaabani (Ukonga), Mohammed Ngulangwa (Temeke), DianaRose Joseph (Kigamboni) na Maftah Sudi (Kilwa Kusini).
Aidha jimbo la Nachingwea ACT imemteua Mosha Emmanuel kuwania nafasi hiyo, Pilima Sijaona (Newala Vijijini), Lulindi ni Francis Ngaweje, Mtwara Mjini yupo Bakari Mtila, Tunduru Kusini amesimamishwa na Ally Abdallah, Songea Mjini yupo Emmanuel Ndomba, Namtumbo ameteuliwa Boniface Thawe na katika Jimbo la Madaba yupo Kuhani Loston.
Wagombea wengine ni Raymond Ndomba (Nyasa), Mwanahamisi Mayinga (Kalenga), William Kasika (Isimani), Daniel Mwangili (Mufindi Kaskazini), James Kitime (Mafinga Mjini), Salim Nyemolelo (Mufindi Kusini), Taji Mtuga (Kilolo), Michael Nyilawila (Songwe), Hosea Mwanjoje (Mbeya Vijijini) na Samwel Motto (Kyela).
Pia Frank Magoba aliteuliwa na chama hicho kuwania jimbo la Rungwe, Gwandumi Mwakatobe (Busekelo), Julius Philipo (Mbozi), Rosemary Mwashamba (Vwawa), Lusekelo Asheri (Mbeya Mjini), Lucy Okeyo (Momba), Reddy Makubha (Tunduma), Paul Mbogho (Singida Vijijini), Kapalatu Salim (Manyoni Magharibi) na John Mottee (Manyoni Mashariki).
Jimbo la Singida Mjini anayewania nafasi hiyo kupitia chama hicho ni Anna Mghwira, Joram Ntandu (Singida Magharibi), Devatus Munna (Singida Mashariki), Henry Mollo (Mkalama), John Patrick (Nzega Vijijini), Abdallah Kondo (Nzega Mjini), Peter Kabuya (Bukene), Tito Alex (Igunga), Leopald Mahona (Manonga), Kirungi Kirungi (Kaliua), Msafiri Mtemelwa (Urambo), Godwin Kayoka (Ulyankulu), Kansa Mbarouk (Tabora Kaskazini) na Bakari Mtongwa (Igalula).
Kwa upande wa Zanzibar chama hicho kimesimamisha wabunge na wawakilishi katika majimbo yote na baadhi ya walioteuliwa kuwania nafasi hizo ni Masoud Suleiman Bakari (Konde), Juma Hamad Juma (Micheweni), Hamad Shehe Tahir (Tumbe) na Mbarouk Ali Khamis (Wingwi).
Wengine ni Suleiman Ali Hassan (Gando), Ali Makame Issa (Kojani), Salim Sheha Salim (Mtambwe), Husna Salim Omar (Mgogoni), Hassan Abdalla Omar (Wete), Asha Bakari Mohammed (Chake), Ridhiwan Khamis Nasib (Chonga) na Ali Salum Humud (Ole).
Monday, August 10, 2015
Thursday, August 06, 2015
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF, Profesa Ibrahim Lupumba amejiuzulu nafasi ya Mwenyekiti chama hicho
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF, Profesa Ibrahim Lupumba amejiuzulu nafasi ya Mwenyekiti chama hicho kwa madai kuwa UKAWA wameshindwa kusimamia makubaliano waliyokuwa wameyafikia, hivyo yeye atabaki kuwa mwanachama wa kawaida wa CUF.....Taarifa kwa kina itakufia hapahapa endelea kutembelea Mtandao huu
Tuesday, July 28, 2015
lowasa ajiunga rasmi na chadema
HABARI HATIMAYE EDWARD LOWASSA AJIUNGA RASMI CHADEMA NA AKABIDHIWA KADI
Lowassa: Namshukuru mke wangu Regina, wanangu na wanafamilia katika kipindi hiki kigumu kilichojitokeza. Lowassa: Nawashukuru wanaCCM waliojitokeza kuniunga mkono wakati nikitafuta wadhamini. Lowassa: Kilichotokea Dodoma, ni kupora madarakani ya kamati kuu, waswahili wanasema kubaka madaraka. Lowassa: Chuki na roho mbaya zilitawala licha ya mimi kuwa mgombea mwenye ushawishi na anayekubali zaidi kuliko wote Lowassa:Kwa mantiki hii nitakuwa mnafiki kama nitaendelea kudanganya nafsi yangu na Watanzania kuwa bado nina imani na CCM Lowassa: Sijakurupuka kwa uamuzi huu, nawaomba watanzania wajiunge na UKAWA katika Safari ya Matumaini. Lowassa: Wanaoogopa kisasi wamefanya madhambi gani? Waulizeni..mimi ni Mkristo,sina kisasi..waende wakatubu kwa Mungu wao Lowassa: CCM Si baba yangu wala Mama yangu. Watanzania kama wameyakosa mabadiliko ndani ya CCM, basi watayapata nje ya CCM. Lowassa hatimaye amemaliza rasmi kujiunga na CHADEMA na watu sasa wanashangilia wakiimba 'Tunaimani na Lowassa,
Friday, July 24, 2015
Kenya kicks off biggest ever security operation for Barack Obama welcome
Kenya kicks off biggest ever security operation for Barack Obama welcome
The biggest security operation in Kenya’s history is under way as the vulnerable east African nation prepares to welcome its “son”, Barack Obama, for the first time since he reached the White House.
The US president was due to touch down on Air Force One on Friday
evening for a weekend programme in the capital, Nairobi, that includes
an international business summit, dinner with his Kenyan counterpart, Uhuru Kenyatta, and a major public address.
Kenya is treating the visit as a chance to shine, akin to an Olympics or a football World Cup, and is all too aware how catastrophic another terrorist attack would be for its image. Three months ago Islamist militants murdered 148 people at a university in Garissa, while an attack on Nairobi’s Westgate shopping mall left at least 67 people dead less than two years ago.
Hundreds of US security personnel have arrived in Kenya in recent weeks and three hotels have been examined by the secret service, according to local media.
Osprey tilt-rotor aircraft, usually stationed at the US military base in Djibouti, flew over Nairobi this week alongside a White Hawk helicopter with presidential insignia, Agence France-Presse reported. Other military helicopters have been flown in reportedly from a US special forces facility at Kenya’s Manda Bay base, from which raids on al-Shabaab militants in Somalia are launched.
“Nairobi is seen as the second most important US embassy in the world after Moscow because of both Somalia and its proximity to the Middle East,” an American source said. “There are so many missions going on that we don’t even hear about.”
Kenya’s civil aviation authority announced that national airspace would be closed for 50 minutes on arrival and 40 minutes on departure, inadvertently revealing the schedule of the president, who will travel without his family.
Obama will then be chauffeured in his bomb-proof limousine, dubbed “the Beast”. The $1.5m (£970,000) car has 20cm-thick steel plates, 13cm-thick bulletproof glass, kevlar-reinforced tyres and a presidential blood bank in the boot.
Around 10,000 police officers – roughly a quarter of the national force – were being deployed in the capital and several major roads would be closed to all but emergency and security vehicles. The move prompted many people to stay at home and numerous banks and schools to shut early on Friday.
Evans Kidero,
the governor of Nairobi county, said: “Security is both visible and
invisible. It’s something we’ve been working on even before Obama is
coming.”
Kidero’s belated attempt to beautify the city by planting grass has been mocked on social media, with Twitter users adopting the hashtag #KideroGrass. “In African culture when you’re receiving an important visitor, when your in-laws are coming, the house must be spruced,” he explained. “Actually we plant grass every year but our people are so indisciplined they walk on them, they kill them. I’m just appealing that they should keep off my grass.”
But security concerns are thought to have played a part in the decision for Obama not to travel to his father’s grave and meet family members in the village of Kogelo. One relative, Said Obama, said: “I would have wished that he visit here but to me the most important fact is he’s coming to Kenya. He’s wearing several hats: he’s a family member and he’s the president of the United States. I know if he doesn’t come to Kogelo, his spirit will be there with us.”
The 49-year-old half-brother of the president’s father, said Barack Obama senior and junior shared a similar intelligence and deep baritone voice. “I’m feeling proud of Barack,” he said. “He has never failed us. He has put our name on the map.”
Obama himself talked recently about the heavy security restrictions compared with previous trips to his ancestral home, most recently as a senator in 2006. “I will be honest with you, visiting Kenya as a private citizen is probably more meaningful to me than visiting as president, because I can actually get outside of the hotel room or a conference centre,” he said.
The 53-year-old president, who once shot down conspiracy theories that he had actually been born in Kenya by publicly producing his birth certificate from Hawaii, is expected to spend time with family members who will travel to Nairobi, according to White House officials.
Securing the tour is unchartered territory since no sitting US president has previously visited Kenya or Ethiopia, to which Obama flies on Sunday. Both countries are seen as vital allies in the African theatre of the “war on terror”.
At a press conference at Nairobi’s state house, where the Kenyan and US flags currently fly alongside bunting, Kenyatta highlighted the threat. “Our country has endured the attacks of depraved, ideological criminals,” he said. “We have fought them unrelentingly, and they know, as well as we do, that they will lose.”
Kenya is treating the visit as a chance to shine, akin to an Olympics or a football World Cup, and is all too aware how catastrophic another terrorist attack would be for its image. Three months ago Islamist militants murdered 148 people at a university in Garissa, while an attack on Nairobi’s Westgate shopping mall left at least 67 people dead less than two years ago.
Hundreds of US security personnel have arrived in Kenya in recent weeks and three hotels have been examined by the secret service, according to local media.
Osprey tilt-rotor aircraft, usually stationed at the US military base in Djibouti, flew over Nairobi this week alongside a White Hawk helicopter with presidential insignia, Agence France-Presse reported. Other military helicopters have been flown in reportedly from a US special forces facility at Kenya’s Manda Bay base, from which raids on al-Shabaab militants in Somalia are launched.
“Nairobi is seen as the second most important US embassy in the world after Moscow because of both Somalia and its proximity to the Middle East,” an American source said. “There are so many missions going on that we don’t even hear about.”
Kenya’s civil aviation authority announced that national airspace would be closed for 50 minutes on arrival and 40 minutes on departure, inadvertently revealing the schedule of the president, who will travel without his family.
Obama will then be chauffeured in his bomb-proof limousine, dubbed “the Beast”. The $1.5m (£970,000) car has 20cm-thick steel plates, 13cm-thick bulletproof glass, kevlar-reinforced tyres and a presidential blood bank in the boot.
Around 10,000 police officers – roughly a quarter of the national force – were being deployed in the capital and several major roads would be closed to all but emergency and security vehicles. The move prompted many people to stay at home and numerous banks and schools to shut early on Friday.
Advertisement
Kidero’s belated attempt to beautify the city by planting grass has been mocked on social media, with Twitter users adopting the hashtag #KideroGrass. “In African culture when you’re receiving an important visitor, when your in-laws are coming, the house must be spruced,” he explained. “Actually we plant grass every year but our people are so indisciplined they walk on them, they kill them. I’m just appealing that they should keep off my grass.”
But security concerns are thought to have played a part in the decision for Obama not to travel to his father’s grave and meet family members in the village of Kogelo. One relative, Said Obama, said: “I would have wished that he visit here but to me the most important fact is he’s coming to Kenya. He’s wearing several hats: he’s a family member and he’s the president of the United States. I know if he doesn’t come to Kogelo, his spirit will be there with us.”
The 49-year-old half-brother of the president’s father, said Barack Obama senior and junior shared a similar intelligence and deep baritone voice. “I’m feeling proud of Barack,” he said. “He has never failed us. He has put our name on the map.”
Obama himself talked recently about the heavy security restrictions compared with previous trips to his ancestral home, most recently as a senator in 2006. “I will be honest with you, visiting Kenya as a private citizen is probably more meaningful to me than visiting as president, because I can actually get outside of the hotel room or a conference centre,” he said.
The 53-year-old president, who once shot down conspiracy theories that he had actually been born in Kenya by publicly producing his birth certificate from Hawaii, is expected to spend time with family members who will travel to Nairobi, according to White House officials.
Securing the tour is unchartered territory since no sitting US president has previously visited Kenya or Ethiopia, to which Obama flies on Sunday. Both countries are seen as vital allies in the African theatre of the “war on terror”.
At a press conference at Nairobi’s state house, where the Kenyan and US flags currently fly alongside bunting, Kenyatta highlighted the threat. “Our country has endured the attacks of depraved, ideological criminals,” he said. “We have fought them unrelentingly, and they know, as well as we do, that they will lose.”
Barack Obama
will touch down in his father’s ancestral home this week for the first
time since becoming US president, where he is expected to be greeted by
his counterpart Uhuru Kenyatta and thousands of expectant Kenyans.
The main purpose of the visit is a global entrepreneurship summit, but there have been calls
for him to address everything from al-Shabaab to gay rights by those
who are frustrated by the vagueness of his African policy so far.Adekeye Adebajo wrote in a recent article that the president’s track record on Africa is more style than substance, arguing that although Obama “clearly identifies with the continent” he has failed to translate this into meaningful action.
In Nairobi, there were accusations that the capital was being whitewashed in a last-minute attempt to clean-up the streets for his trip. Last week, Robert Alai, a influential blogger based in the city, tweeted a picture that appeared to show street kids being rounded up, whilst AFP reported that children were being kept out of the city centre.
Subscribe to:
Comments (Atom)






















